* ~ * I Can't Wait * ~*

Mzee ES, emphasis yangu iko kwenye "regime" not individuals. Nitakuwa mwongo nikidai kuwa wana CCM wote ni corrupt, na nitakuwa msaliti wa ukweli nikisema kuwa Tanzania hatuna viongozi wazuri kwenye chama tawala.

Tatizo letu kubwa ni regime not individual leaders or politicians. Now, this regime is a system of political power and administration that is carried out by the ruling party. Tatizo letu hili ambao mara nyingi Tanzania unajulikana kama "system" ni kuwa kwa kujikita muda mrefu madarakani imeanza kupoteza mwelekeo wake.

Exposed! - Tukio la Mkataba wa Buzwagi, Ununuzi wa Rada, Dege la Rais, Mikataba mibovu mingine n.k imeonesha the nature of the regime!

Challenged - uwepo wa forum hii ya JF na nyingine, maandishi ya magazetini, na kuthubutu kuweka mikataba ya usiri hadharani, "system" imekuwa challenged. Na itaendelea kuwa challenged until it starts responding to the needs of the times! Sasa hivi bado haijatishwa kuwa it'll be replaced that is why they still believe the can do anything, anyhow, for any reason.

Changed! - This system ultimately will be changed. The regime must fall either due to an implosion (the cheche za kina Butiku na Bilali zikiwafikia wana CCM wengi zaidi) or by an external force that is strong enough than the opposing force. Wanaweza kufanya kile ambacho China imeweza kufanya nacho ni kujibadili bila kubadili misingi ya mfumo huo. Na nina uhakika wataweza kufanya zaidi ya kile ambacho China, Burma, na Vietnam vimeshindwa kufanya, nacho ni kuamua kutengeneza mazingira ya kushindwa kwao.

Nijibu swali lako moja ni haki gani ambazo wananchi wa TAnzania hawana ambazo serikali ya CCM imeiondoa arbitrary nayo ni haki ya kuchaguliwa na kuchagua mtu ambaye hayuko katika chama cha siasa. Huu ni uamuzi ambao Mwalimu aliuita ni wa kipumbavu!
 
Kwa kweli kinachotokea sasa hivi Tanzania ni Mwangi wa haki usikikao kwa kishindo, na sauti yake ni kali kiasi kwamba mafisadi hata wazibe masikio yao namna gani bado wataendelea kusikia kelele na mayowe ya mnyonge.

Nani kasema chozi la mnyonge linadondoka bure?.
Chozi la mnyonge ni kengele ya tahadhari!. Wenye akili ya kusoma hulka ya mwanadamu hulitambua hili.

Iwapo waliopewa dhamana ya uongozi wa Taifa letu watashindwa kukisikiliza kilio hiki,wakashindwa kuisimamia misingi ya haki za watu wake, wakatwaa urithi wa watoto wake na kuutapanya kwa maslahi ya watu wachache, basi nachelea kusema kwamba ufisadi utazidi kupiga upondo ukiusukumiza Mtumbwi wa Tanzania katika kina kirefu sana, kina ambacho urefu wake ni mkubwa kuliko bahari ya pasifiki
wakija kutahamaki ala! loh salale tufani la ghadhabu ya Mtanzania inakuja kwa kasi ya ajabu.

Ni wakati muafaka kwa mamlaka kufanya kitu muafaka kabisa, muda unapowadia na haki inapotaka ichukue nafasi yake hakuna wa kuizuia. infact konzi ya dhalimu katu haiwezi kuvunja mwamba wa haki hata siku moja!.
 
yaani mmeshindwa kusubiri? Hiyo haraka ya nini. Unajua mafisadi huwa na papara na haraka tu. Mmeambiwa msubiri, hamtaki. Subirini na wakati ukifika basi mambo yatakwenda vizuri. Kwanini hamtaki kusubiri? jamani haraka haraka haina baraka. Halafu hilo shairi mbona limekaa kishari shari hivi?

Asante.
 

Kwa hiyo wao kufanya haraka kutumaliza hadi tufe tuishilie mbali ni halali, huku sisi tukiendelea kusubiri ili tuvute heri na tuvumilie ili tule mbivu huku wao wakisema Chukua Chako Mapema (CCM) wakiimba wimbo wa Chelewa Chelewa, Mtoto Utakuta si Wako Tena (CCM-UWT).... Shari shari wanaleta wao, sisi tunapiga kelele za mayowe, jamani WEZIIIIIIII, Uwiiiii, wezi wamevamia.... kuna majambaziiiiii, wamepora BoT..... wamepora wanyama wetu..... wanepora misitu yetu, haoooooo, wamehamia katika madini wanazoa haoooo, jamani tuwakamate tuwaponde mawe na kuwafunga matairi shingoni na kuwachoma moto kama wale vibaka wa manzese ambao wamelala na kushinda njaa na sasa wanasema "HATUNA CHA KUPOTEZA afadhali kufa ama kwenda jela ambako angalao nitakula mlo mmoja kwa siku".......SHARI WAO NDIO WAMETUVAMIA, tuwaache watuue sisi na watoto wetu na kupora mali zetu? Tuwache wabake dada, wake zetu na mama zetu? HATUKUBALI
 

R.I.P LD
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…