KIBONG'OTO
Member
- Jan 19, 2013
- 12
- 0
- Thread starter
-
- #41
wakuu naombeni ushauri kuna mpenzi wangu tuna muda wa miezi mitatu sasa katika mahusiano yetu, ila simuelewi nikimpigia simu anachelewa kupokea au asipokee kabisa ni kimuuliza tatizo nini anatoa sababu zisizo za msingi, mara nyingi mi ndo mpigaji sana wa simu na nikikaa kimya kuto kumpigia hanitafuti, kuna siku nilimuuliza bado ananipenda akanijibu yuko njia panda na hajielewi na muda mwingi simu yake inakuwa busy sana nikimpigia wakati wa usiku, wakuu naomba mnisaidie nifanyeje? Bado namhitaji
Nashukuru sana wakuu kwa ushauri wenu nitaufanyie kazi na nimefikia maamuzi bola niachane naye naona kama napoteza muda kuwa na mtu ambaye hana upendo na mimi na nikiendelea kuwa nae ataniletea matatizo na jambo linaweza kuniathiri sana katika shughuli zangu binafsi na nimeona bola nianzishe maisha yangu peke yangu na naamini bila yeye sito shindwa maisha.
i' ve got u...
Yuko njia panda maana anawaalinganisha na bado anaona wote mnapungua kwenye mzani kwa upande mmoja na wote anawahitaji kwa upande mwingine. Hajafahamu kama ni yupi hasa anayemfaa maana hamsomeki vizuri. Hata hivyo, mwenzako anakuzidi points kidogo sana kwa ratio ya 52:48 hivi. Haoni future kila anapowatazama. Ni km anaogopa kusitisha mahusiano na wewe kwa kuhofia huko anakotaka kwenda hakuna guarantee ya wazi. Hata hivyo, ni vema ukae nae na umsaidie kuamua kistaarbu kuwa unamsaidia aende njia ipi kwa kujitoa mapema. Itakusaidia japo utaamia kwa muda!Usipofanya hivyo tarajia maumivu zaidi bila shaka!
dah, yaani wewe jamaa ushapewa jibu huelewi. Kusoma hujui na picha je?
Mwenzako ndio hivyo tena amekuambia kistaarabu kwamba huna chako. Kafanya hivyo kwa vitendo (kwa kutopokea simu na kutokupigia simu) na pia kwa maneno (kwa kukujibu yupo njiapanda)
kwangu mimi huyu mdada ni mstaarabu sana lakini wewe ndio huelewi wala husomeki. Kama unadhani unampenda labda kaa chini tena tafakari kwa nini hujawa chagua la kwanza kwake , je una mapungufu yepi. Kama yanarekebisha basi jitahidi
otherwise tafuta ustaarabu mwingine kiongozi
haupo peke ako hapo yani ukiona msichana anajibu hivyo ujue mpo zaidi ako na wote anawapenda so anashindwa kuamua
heee...mweee! hapo penye red patamu! ukipiga simu anapochelewa kupokea au hapokei kabisa basi fahamu kuwa wakati huo huwa yuko na jamaa 6X6 na wako kazini so don't disturb...men at work! umeelewa? :bowl:
Ondoka mapema au kama vipi mtumie kingono ila usiwekeze moyo wako kimawazo utakesha.
Shauriro ukiona dalili kama hizo jaribu kutafuta hifadhi kwingine coz karibia unaenda kuumizwa.
Kaka hapo ni Code red tayari,hamisha mawazo yako kabisaaaa na tafuta pa kujihifadhi afu mchukulie poa.Kashakuacha huyo
mie siwezi msema sana huyo mdada.
Kuna wakati mtu anaweza jikuta kwenye mahusiano yanayomwacha njia panda.
Labda wewe mkaka husomeki kwake, kwa hiyo kaingia mguu mmoja nje ndani?
Kuna vitu hakuelewi na wewe hujaamua kuviweka wazi?
Unaonekana kito.bi, so anakuwa na wasiwasi kujiachia kwako?
Ungemuuliza yuko njia panda kivipi?
Huko kutopokea simu zako ni 'defensive mechanism' inaweza kuwa njia ya kujifariji kwamba hujamwingia moyoni, still anaweza kuchunia simu zako na maisha yakaendelea. Lakini 'ukweli' yaweza kuwa kinyume chake.
miezi mitatu bado michache sana usitake akujibu kwa kukurupuka