Hukumu zitolewazo kwa vigogo wa serikalini na watu matajiri huwa zinanipa mashaka!

DOMBWELA

JF-Expert Member
Jan 18, 2014
757
842
Ndugu zanguni goja nitolee mfano wa hukumu ya Mh Daniel Yona na mwenzake, eti wamehukumiwa kutumikia kifungo cha nje na kufanya kazi za kijamii mtaani pamoja na tuhuma zote zile nilizokuwa nikizisikia dhidi yao!. Kadhalika na kesi zingine zinazo fanana na hayo makundi niliyotaja hapo juu. Mwenye kumbukumbu anisaidie, nimatajiri gani na vigogo wepi wamekwisha tumikia vifungo vikubwa kama wanavyo tumikia ndugu zangu walio iba kuku, simbilisi, mbuzi n.k. Mmmm naomba wanajamii forum niaminishe kuwa hata matajiri na vigogo serikalini wanaweza kufungwa kama watu wengine kulingana na makosa yao, vinginevyo nitaendelea kuamini kuwa ukiwa na fedha au ukawa na nafasi kubwa serikali huwezi kuguswa na mahakama zetu, na hata ukiguswa una nafasi ya kujadiliana nazo ukapangiwa adhabu unayoona inafaa kwako.
 
Simtetei mwovu yeyote ila nadhani una uchungu flan na hao watu. Kile kitendo tu cha kuhukumiwa kuwa ana makosa, kwa mtu aliyewahi kuwa kiongozi mkubwa hivyo, hilo ni pigo tosha kabisa.
Alishawahi kuitwa Mheshimiwa, sasa amevuliwa uheshimiwa wake wote na ni mhalifu aliyewahi kupatikana na hatia. Hii pekee imemwondolea hadhi zake zote. Kinyamwezi kwetu tunamwita "A jail Bird". Kwenye wsifu wake itamshushia hadhi milele. Kuna sehem kule unyamwezini hawezi pita tena, kuna watu hawezi watembelea tena, yaani we acha tu.
Nadhani Hakimu aliyaangalia hayo yote akampa hiyo adhabu. Wala usimfananishe huyo kibaka wako na Yona. Si vyema
 
Kwa hiyo unakubaliana na mimi ninaye amini kuwa ukiwa na nafasi nzuri, kubwa serikalini au ukawa na fedha ya kutosha adhabu yako itatofautiana na mtu wa kawaida kama mimi hata mkitenda kosa linalo fanana!.
 
Kuna watu wamesema humu kuwa Mhe. JPM jana aliingilia uhuru wa Mahakama. Hivyo basi hatupaswi pia kuhoji maamuzi yaliyotolewa na Mahakama!
 
Kwa hiyo unakubaliana na mimi ninaye amini kuwa ukiwa na nafasi nzuri, kubwa serikalini au ukawa na fedha ya kutosha adhabu yako itatofautiana na mtu wa kawaida kama mimi hata mkitenda kosa linalo fanana!.


Huo ndo ukweli, hata jela ya muuaji wa kawaida ni tofauti na ile ya muuaji wamfulizo
 
Back
Top Bottom