Hukukosea Kuoa, Umekosea namna ya kufikiri !!

Hukukosea Kuoa, Umekosea namna ya kufikiri !!

Himidini

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2013
Posts
5,534
Reaction score
4,190
^^
Umekosea kuoa?
Hilo ni swali nilomuuliza rafiki yangu kipenzi sana. Alinifuata kwa maongezi ya kawaida. Maongezi yenye upendo,furaha, amani na urafiki. Wepesi wangu wa kumjua rafiki yangu ndio ulizua mengi. Hakuwa na furaha! Ni kana kwamba alijilazimisha kusema! Hata hivyo hakuwa msemaji sana bali, aliishia kutamka tu 'nimekosea kuoa!'
....
Ni vigumu kukataa ukweli uliondani ya usemi wa rafiki yangu. Maana ktk mahusiano hufika mahali kila mwanaume huwaza kuwa 'amekosea kuoa' na hata huthibitisha mawazo yake kupitia majirani ambao huwatathimini uhusiano wao kwa namna ya nje kuliko ndani zaidi. Na ni kweli pia yapo mahusiano yasiyobebeka hata uwe na kichwa chuma, yatakuyeyusha tu mpaka uyaache. Lakini yapo ambayo yanaweza kudhibitiwa yasife mbali kiasi cha kutengana.
...
Rafiki yangu anadai mkewe hashauriki, haambiliki, wakipanga hivi yeye hufanya vile, nyumba inaonekana ina wanaume tu na anadai mkewe hawezi kubadilika kamwe! Ni katika mwaka wa tatu na wana mtoto mmoja. Sasa anasema 'amekosea kuoa' anakumbuka X wake alivyomuasa kuhusu mpenzi wake, ambae sasa ni mkewe! Anasisitiza amekosea kuoa
...
Jawabu langu lilikuwa rahisi, 'Umekosea namna ya kufikiri'. Nadhani hili linawagusa wengi walio katika uchumba au ndoa, wanaodhani wamekosea kuwa na wenzi wao! Lakini ukidadisi vizuri wamekosea namna ya kufikiri. Mahusiano ya aina hii nayaona katika namna ifuatayo
I:
MAHUSIANO YANAHITAJI KIASI FULANI CHA HEKIMA
Unapokuwa na mwenza wa uchumba au ndoa, ni vema kukubali kuwa huna mtu mkamilifu. Anayo madhaifu ya kimwili, kiuamuzi au kiushawishi. Hekima ni namna gani unaondoa kwa uangalifu milango aliyoziba mwenzio katika kupata muafaka.

II:
HATA MPYA ANAYO YASIYOPENDEZA
Kumuacha uliyetoka nae mbali kwa tofauti za mawazo,mitazamo au tabia zinazoweza kujadiliwa na kumpata mpya, haina maana kuwa kule utapata asiye na kasoro. Jambo baya ni kusahau mambo mazuri makusudi kama heshima yake, mchango wake wa kukutunzia watoto, umakini wake katika kuhudumia familia, kukupa mavazi yanayokufanya usifiwe ofisini n.k Mahusiano ni zawadi inayohitaji kupakwa rangi.
..
UMEKOSEA KUFIKIRI
Asili ya maamuzi yote ni matunda ya kufikiri. Ukifikiri vibaya utavuna tunda la uchungu upweke au kujihukumu. Ukifikiri vema na kupembua mambo utapata tunda la kuchukuliana, kuvumiliana na kupalilia mti wa penzi upya.
Kagua namna yako ya kufikiri.
^^
 
Umegusa sehem husika. Hzo ndizo kauli zetu baada ya mambo kuharibika
 
Hamna mwanamke anayependa kuwa juu ya mmewe kama mwanaume anajibehave, tatzo wanaume mnajua san kukurupuka na mtu ukishauriwa kidogo ndo madai ya kusema unapandwa kichwani... Mwanamke anayekuonya na kukuelekeza jema huyo ndo anayekupenda, Kimada au mwanamke ambaye yupo na wew kimaslAhi hawezi kamwe kukuonya zaidi atakusifia hata kwa mabaya unayofanya bora anapata anachotaka., basi hapo mwanaume ndo unaona sasa huyu ndo anayenipenda, Na dunian hamna mtu mkamilifu hAta mmoja, labda uumbe wakwako
 
Back
Top Bottom