Hotuba za Baba wa Taifa TBC zimeisha?

Hotuba za Baba wa Taifa TBC zimeisha?

Pastor Achachanda

JF-Expert Member
Joined
May 4, 2012
Posts
3,023
Reaction score
1,316
Nimetoka kusikiliza hotuba za mwalimu Nyerere lakini haina tofauti na niliyoisikiliza juzi na jana.Mbona hawabadilishi?
 
Ndugu yangu hii hotuba inayohusu vita vya kagera sasa inakaribia mwezi kama sio zaidi....

Sijui anayehusika na kitengo ameenda matenity leave.

Nashangaa na ushindani wote uliopo zama hizi kwa vyombo vya habari jamaa bado wapo dunia ya analogia.

Wanakera kwa kweli.
 
He kumbe ni mwezi sasa sikujua.Inawezekana kweli mhusika yupo maternity.Ninaposikiliza huwa nadhani mpya kumbe ileile 2!
 
He kumbe ni mwezi sasa sikujua.Inawezekana kweli mhusika yupo maternity.Ninaposikiliza huwa nadhani mpya kumbe ileile 2!

Hawa wana lao jambo huwa wanafanya hivi makuudi hasa wakati huu wa vuguvugu la kisiasa ili watu tuwaogope serikali kwamba wako fiti kumbe hamna lolote, Wamisri wameweza bana.
 
Penye nia pana njia.Watu hawana masihara na haki zao na hatuogopi.Pia hamieni stesheni za wajanja kama RFA,Iboni FM nk
 
Hawana tatizo kwani wao upinzani na vyombo vingine hauwahusu,wanakula kodi za watanzania!
 
Nimetoka kusikiliza hotuba za mwalimu Nyerere lakini haina tofauti na niliyoisikiliza juzi na jana.Mbona hawabadilishi?

Labda ni Amri toka kwa Rais wa NCHI... asivyompenda NYERERE hotuba zake nyingi zina mafundisho ya LEO tunayoyapata; NI BORA Msikilize VITa YVA KAGERA nenda rudi... Rais wetu wa sasa HAKWENDA VITANI alikuwa Kamishna wa Siasa JESHINI...
 
Jamani wana forum wenzangu ni kweli hotuba ya vita imedumu muda mrefu na sasa hivi nimemaliza kusikiliza tena wana boa
 
Hotuba za Mwl. zina maneno makali ya kukemea ubaya, sasa hawa wanaogopa kwa kuwa wameshatopea kwenye ubaya aliokuwa anaonya Nyerere, tena wamepitiliza.

The truth pains but must be told!
 
Ndugu yangu hii hotuba inayohusu vita vya kagera sasa inakaribia mwezi kama sio zaidi....

Sijui anayehusika na kitengo ameenda matenity leave.

Nashangaa na ushindani wote uliopo zama hizi kwa vyombo vya habari jamaa bado wapo dunia ya analogia.

Wanakera kwa kweli.


ushindani umekatwa kabisa na ving'amuzi ndugu
 
Hotuba za mwl sio za mchezo.kwani zinawachoma.hasa kwa kipindi hiki.utafikiri mwl yu hai.alikuwa anatoa UNABII hivyo hiyo ya vita vya kagera angalau angalau.
 
Back
Top Bottom