Comi
JF-Expert Member
- Oct 2, 2011
- 3,328
- 958
Kutokana na matokeo ya uchaguzi wa wiki iliyopita na haya ya marudio leo imejidhihirisha kuwa upinzani unakuwa kwa kasi. Matokeo hayo yawezakuwa ni matunda ya vyama hivyo kuungana(ukawa). Sasa jukumu lililombele ni viongozi waliochaguliwa kuonyesha kwa vitendo ili iwe rahisi katika uchaguzi ujao kupata viti vingi vya udiwani na ubunge.
Niwapongeze upinzani kwa kuendesha kampeni za amani ambazo zimeweza kuwapa elimu wananchi na kuweza kuchagua wale wanaowaamini kuwa wataweza kuwavusha katika miaka mitano. Pia niwapongeze viongozi kwa sababu pamoja na kutokea hujma za wazi,ukiukwaji wa utaratibu wa kupiga kura lakini bado wamekuwa na busara kwa kulinda amani ya nchi.
Hongereni viongozi wa chama tawala mnaopigania kuondoa amani ya nchi kwa ajili ya madaraka na maslahi yenu. ASIYEKUBALI KUSHINDWA SI MSHINDANI. Ni wakati wenu sasa wakujitathimini na kubadilika pale mnapoona mmelikosea taifa kabla ya uchaguzi mkuu mwakani. Mabavu mnayotumia sasa hivi ni msaada ambao mnawapa upinzani bure kwani wananchi watajiuliza hawa ccm wanataka nini kutoka kwetu hata watumie mabavu kiasi hiki.
Kwa matokeo yaliyokwisha toka ni dhahiri upinzani umepanda kwa kasi kubwa kwani ni nadharia ccm haijashinda bali imeshindwa kwani awali ilikuwa inamiliki hayo maeneo na sasa yameponyoka mikono mwake.
Hongereni upinzani kwa matokeo mazuri ila mnatakiwa kuendelea kutoa elimu ya uraia kwa wananchi kadri muwezavyo
Niwapongeze upinzani kwa kuendesha kampeni za amani ambazo zimeweza kuwapa elimu wananchi na kuweza kuchagua wale wanaowaamini kuwa wataweza kuwavusha katika miaka mitano. Pia niwapongeze viongozi kwa sababu pamoja na kutokea hujma za wazi,ukiukwaji wa utaratibu wa kupiga kura lakini bado wamekuwa na busara kwa kulinda amani ya nchi.
Hongereni viongozi wa chama tawala mnaopigania kuondoa amani ya nchi kwa ajili ya madaraka na maslahi yenu. ASIYEKUBALI KUSHINDWA SI MSHINDANI. Ni wakati wenu sasa wakujitathimini na kubadilika pale mnapoona mmelikosea taifa kabla ya uchaguzi mkuu mwakani. Mabavu mnayotumia sasa hivi ni msaada ambao mnawapa upinzani bure kwani wananchi watajiuliza hawa ccm wanataka nini kutoka kwetu hata watumie mabavu kiasi hiki.
Kwa matokeo yaliyokwisha toka ni dhahiri upinzani umepanda kwa kasi kubwa kwani ni nadharia ccm haijashinda bali imeshindwa kwani awali ilikuwa inamiliki hayo maeneo na sasa yameponyoka mikono mwake.
Hongereni upinzani kwa matokeo mazuri ila mnatakiwa kuendelea kutoa elimu ya uraia kwa wananchi kadri muwezavyo