Tunaifahamu FFU,ndiyo na hata police tunawafahamu.FFU wanapashwa kutuliza fujo na police kulinda mali za wananchi,kutunza amani iliyopo na kuhakikisha kwamba kila mtu anaishi kufuatana na maadili tuliyojiwekea katika jamii kama yapo.Hata hivyo nionayo yakifanywa na vyombo hivi ni kinyume kabisa na matarajio yangu.Vyombo hivi vimekuwa vikitetea na kulinda zaidi maslahi ya 'status quo' kuliko ya wananchi.Yale majukumu yao ya msingi wameyaacha kabisa.Tumeshuhudi police wakishiriki katika kunyang'anya haki za msingi kabisa za wananchi wakishirikiana na mahakama.Na pia tumeshuhudia mara nyingi police wakishiriki katika kunyang'anya mali za wanachi, wao wenyewe moja kwa moja au kwa kushirikiana na majambazi.Haya yako wazi.Police wengi wametajirika kwa kupewa fedha na mitandao ya majambazi ili wafumbie macho uovu wao.Mtandao wa Traffic police na ma-boss wao kukusanya pesa barabarani unaeleweka.Sio siri tena kwamba unaweza kuishia jela kwa kubambikizwa kesi kwa kosa ambalo hata hukutenda.Sasa katika mazoea haya,sio rahisi kukubali hili la Arusha,FFU kuwapiga viongozi wa CCM Mkoa na Wilaya,mm,haliingii akilini.Viongozi hawa walikuwa wanafanya vitendo ambavyo ni kinyume cha maadili ya jamii yetu.Sasa kama hawa ndio viongozi wanaopashwa kutuletea maisha bora,nadhani tumeingizwa mkenge.Nasema hili ni dogo, lakini ni mwanzo mzuri,wa kuanza kuondokana na mawazo kwamba kuna 'the untouchables',watu ambao wako juu ya sheria.Hongereni FFU Arusha.