Hongereni FFU Arusha,huu ni mwanzo mzuri.

Tikerra

JF-Expert Member
Sep 3, 2008
1,702
146
Tunaifahamu FFU,ndiyo na hata police tunawafahamu.FFU wanapashwa kutuliza fujo na police kulinda mali za wananchi,kutunza amani iliyopo na kuhakikisha kwamba kila mtu anaishi kufuatana na maadili tuliyojiwekea katika jamii kama yapo.Hata hivyo nionayo yakifanywa na vyombo hivi ni kinyume kabisa na matarajio yangu.Vyombo hivi vimekuwa vikitetea na kulinda zaidi maslahi ya 'status quo' kuliko ya wananchi.Yale majukumu yao ya msingi wameyaacha kabisa.Tumeshuhudi police wakishiriki katika kunyang'anya haki za msingi kabisa za wananchi wakishirikiana na mahakama.Na pia tumeshuhudia mara nyingi police wakishiriki katika kunyang'anya mali za wanachi, wao wenyewe moja kwa moja au kwa kushirikiana na majambazi.Haya yako wazi.Police wengi wametajirika kwa kupewa fedha na mitandao ya majambazi ili wafumbie macho uovu wao.Mtandao wa Traffic police na ma-boss wao kukusanya pesa barabarani unaeleweka.Sio siri tena kwamba unaweza kuishia jela kwa kubambikizwa kesi kwa kosa ambalo hata hukutenda.Sasa katika mazoea haya,sio rahisi kukubali hili la Arusha,FFU kuwapiga viongozi wa CCM Mkoa na Wilaya,mm,haliingii akilini.Viongozi hawa walikuwa wanafanya vitendo ambavyo ni kinyume cha maadili ya jamii yetu.Sasa kama hawa ndio viongozi wanaopashwa kutuletea maisha bora,nadhani tumeingizwa mkenge.Nasema hili ni dogo, lakini ni mwanzo mzuri,wa kuanza kuondokana na mawazo kwamba kuna 'the untouchables',watu ambao wako juu ya sheria.Hongereni FFU Arusha.
 
Tunaifahamu FFU,ndiyo na hata police tunawafahamu.FFU wanapashwa kutuliza fujo na police kulinda mali za wananchi,kutunza amani iliyopo na kuhakikisha kwamba kila mtu anaishi kufuatana na maadili tuliyojiwekea katika jamii kama yapo.Hata hivyo nionayo yakifanywa na vyombo hivi ni kinyume kabisa na matarajio yangu.Vyombo hivi vimekuwa vikitetea na kulinda zaidi maslahi ya 'status quo' kuliko ya wananchi.Yale majukumu yao ya msingi wameyaacha kabisa.Tumeshuhudi police wakishiriki katika kunyang'anya haki za msingi kabisa za wananchi wakishirikiana na mahakama.Na pia tumeshuhudia mara nyingi police wakishiriki katika kunyang'anya mali za wanachi, wao wenyewe moja kwa moja au kwa kushirikiana na majambazi.Haya yako wazi.Police wengi wametajirika kwa kupewa fedha na mitandao ya majambazi ili wafumbie macho uovu wao.Mtandao wa Traffic police na ma-boss wao kukusanya pesa barabarani unaeleweka.Sio siri tena kwamba unaweza kuishia jela kwa kubambikizwa kesi kwa kosa ambalo hata hukutenda.Sasa katika mazoea haya,sio rahisi kukubali hili la Arusha,FFU kuwapiga viongozi wa CCM Mkoa na Wilaya,mm,haliingii akilini.Viongozi hawa walikuwa wanafanya vitendo ambavyo ni kinyume cha maadili ya jamii yetu.Sasa kama hawa ndio viongozi wanaopashwa kutuletea maisha bora,nadhani tumeingizwa mkenge.Nasema hili ni dogo, lakini ni mwanzo mzuri,wa kuanza kuondokana na mawazo kwamba kuna 'the untouchables',watu ambao wako juu ya sheria.Hongereni FFU Arusha.
Mwanzo mzuri kumchania mtu shati, wakati ingekuwa upinzania watu wanapoteza maisha na hata kupata ulemavu wa kudumu. Hii ni habari ya kutunga tu ama walivamiwa na wahuni wakitaka chochote kutoka kwao.

Kumbuka yaliyotokea Znz, huko tarime, mwembechai, n. k hii ni janja ya kufunika yanayotokea Tarime siwafagiilii polisi hata kidogo
 
Unajua, tunaelewa hawa jamaa wana uovu mwingi, lakini ni vizuri kuwapongeza hata kwa hako kadogo.
 
Huu ni ujanja wa CCM baada ya kuona wakaazi wa kata ya Sombetini wako tayari kukifanya kile wasichotarajia wakaamua kuchukua mamluki kutoka kata zote za Arusha mjini na kufanya maandamano haramu.Mikutano ya kampeni ya CCM ilisusiwa na wananchi kwa ujumla,Kata ya Sombetini ni miongoni mwaka Kata kubwa kwa maana ya kuwa na wapiga kura wengi.
CCM wanajua wakipoteza tena Sombetini maana yake uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ubunge utaenda upinzani[TLP].Bwana F Mrema na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Arusha mjini bwana J Kileo walimhonga aliyekuwa diwani wa TLP bwana Mawazo ajiuzulu ili waweze kuirejesha kata ya Sombetini.Kuna kila dalili mgombea udiwani kwa tiketi ya TLP atashinda,wana mkakati wa CCM wameamua kuanzisha fujo pengine kuandaa uwanja mzuri wa kuiba kura.CCM waliweza kumrubuni bwana Mawazo na aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya TLP bwana Lema lakini wameshindwa kuwarubuni wakaazi wote wa kata ya Sombetini na hii ndiyo chanzo cha fujo za CCM.Wapinzani tuko imara kulinda kura zetu kwa gharama yoyote.
 
When will we learn,that was for public consumption.FFU wakuchanie SHATI tu? hawa nao wajua mimi? nilipigwa magumi na mateke kwa eti kuwachomekea barabarani na nilipokwenda polisi walikataa kufungua jalada.
 
Back
Top Bottom