Hongera Twalib kwa hili

Jacobus

JF-Expert Member
Mar 29, 2011
4,681
1,698
Wewe ni mtu wa pili kuweka wazi kuwa nchi hii si wote mashabiki wa timu za Inglandi.

Pana katabia ka baadhi ya watu hapa nchini kutaka kuwalazimisha watu wengine wawe kama wao katika unazi katika soka.

Mtu wa mwanzo kunifurahisha in Rais wa Zanzibar alipokuwa na mahojiano na mwandishi Farook Karim ambaye alitaka kumlazimisha mheshimiwa ajipambanue kwenye Usimba na Uyanga. Jibu alilopewa nadhini mpaka leo hawezi lisahau.

Leo katika mwandishi mwenzie Twalib aitwae Tunu kajaribu kumlazimisha Twalib atamke timu anayoipenda EPL, Twalib akabaki akisisitiza kuwa kwa Ulaya yeye anashabikia Real Madrid akimsisitizia kuwa huko yeye ni mtazamaji tu.

Mid nashabikia FC Barcelona.
 
Back
Top Bottom