Hoja za Zitto ni za msingi sana, tatizo harakati zake zimekuja kwa kuchelewa

Babu wa Kambo

JF-Expert Member
May 2, 2016
559
808
Kila mfuatiliaji mzuri wa Siasa za hapa Tanzania ataafikiana na mimi kwamba siku kadhaa hizi Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, amekuwa moto mkali sana hasa baada ya kuanza zile vuta nikuvute Bungeni Naibu Spika alipozuia mjadala wa Wanafunzi wa UDOM ambapo ilipelekea Wabunge kadhaa wa upinzani kufungiwa vikao vya Bunge akiwemo na Zitto mwenyewe

Nasema amekuwa moto kwa sababu Siasa anazozifanya sasa ni tofauti kabisa na aina ya Siasa zake tulizozoea kuziona, yeye huwa ni mtu wa mapambano ya hoja huku akikanyaga kwa tahadhari kubwa, lakini kwa sasa hata anavyoongea tu utagundua kabisa kuna kitu, unaona kabisa ni mtu aliyeamua "lolote na liwe", hakuna tahadhari tena, ni mtu aliyedhamiria. Hizi siyo Siasa za Zitto, japo kidogo alizijaribu akiwa na Chadema lakini si kwa kiwango hiki

Ukimtazama unagundua sasa ni mtu aliyeamua rasmi kupambana na "Mfumo" kandamizi, Mfumo wa Kidikteta chini ya chama kimoja, lakini je wengine tunajiuliza, Mfumo huo ndiyo kauona leo? Kila neno analotoa juu ya Mfumo unaliona ni la ukweli mtupu, lakini je huu ni wakati wake? Jibu ni hapana

Ukweli ni kwamba harakati zake hizi ziko nje ya wakati, it's too late. Utawala huu wa mabavu mnaoulalamikia leo mliuruhusu wenyewe

Unapotaka kupambana na Mfumo ni ngumu sana kuanza papo kwa papo na ukaushinda, wenzake waliliona hili, lakini yeye aliutumia vibaya muda wake akawageuka, haya ndiyo Matunda yake. Kipindi wanafanya yale mapambano ya kuundoa Mfumo-Dola uliojengwa na CCM kipindi yuko CHADEMA ule ndio ulikuwa muda muafaka na si sasa, kipindi kile Mfumo ulikuwa umedhoofu chini ya uongozi dhaifu wa JK ndicho kilikuwa kipindi cha kuuangusha lakini si sasa ambapo mtu mmoja mwenye nguvu amakuja kutengeneza wa kwake na unaomuogopa mno, ni ngumu kuuangusha kirahisi. Ili kuuangusha inabidi kuudhoofisha kwanza, hii haitakuwa kazi rahisi kama anavyodhani Zitto

Anayokula sasa ni "matunda ya usaliti", alidhani anaikomoa CHADEMA na viongozi wake, lakini sasa ndipo anajua kumbe aliisaliti nafsi yake na Taifa lake, ile ndiyo ilikuwa saa ya ukombozi, kwa sasa atapoteza muda na Rasilimali za chama chake bure. Najua anatamani sana apate support ya vyama vingine, kwa bahati mbaya hivyo vyama vingine ndivyo alivyovisaliti kwa mara nyingine kwa kuanzisha Siasa zisizofaa kipindi cha uchaguzi matokeo yake akaipa nguvu zaidi CCM na wateule wake, hakuutambua muda muafaka wa kuunganisha nguvu

Mwisho niseme, sisemi haya kumkatisha tamaa Zitto na Chama chake lakini wengine sisi hupenda kusema ukweli, harakati za Zitto, dhamira ya dhati ya Zitto, vimekuja kwa kuchelewa. Amemaua kupambana kwa sababu yanayomfika sasa ni yale aliyozoea kuyasikia kwa wenzake, ameonja uchungu wake, kusakwa na Polisi kusiko na utaratibu hakukuwahi kumwandama kama ilivyo sasa, ya kufukuzwa Bungeni kusiko na utaratibu yalikuwa ni mambo ya akina LEMA. Hakutaka kuwa mpinzani halisi katika wakati uliofaa

Kila la kheri Zitto na ACT, lakini mko nje ya wakati, poleni kwa mikikimiki mnayopitia, Mfumo huu hautaanguka bila kuudhoofisha kwanza, mapambano haya yanahitaji mtafute nguvu ya pamoja. Poleni wapinzani kwa ujumla wenu
 
Hayo yalipita faraka hazina nafasi kwa sasa ni kuungana kupinga udikteta kwani nani alikuwa hana madhaifu
 
Utawala wa Magufuli utafikia pabaya sana.
Moto unafuka chini kwa chini. Hayo ya kina Zitto ni moshi tu, moto unakuja.
 
Kila mfuatiliaji mzuri wa Siasa za hapa Tanzania ataafikiana na mimi kwamba siku kadhaa hizi Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, amekuwa moto mkali sana hasa baada ya kuanza zile vuta nikuvute Bungeni Naibu Spika alipozuia mjadala wa Wanafunzi wa UDOM ambapo ilipelekea Wabunge kadhaa wa upinzani kufungiwa vikao vya Bunge akiwemo na Zitto mwenyewe

Nasema amekuwa moto kwa sababu Siasa anazozifanya sasa ni tofauti kabisa na aina ya Siasa zake tulizozoea kuziona, yeye huwa ni mtu wa mapambano ya hoja huku akikanyaga kwa tahadhari kubwa, lakini kwa sasa hata anavyoongea tu utagundua kabisa kuna kitu, unaona kabisa ni mtu aliyeamua "lolote na liwe", hakuna tahadhari tena, ni mtu aliyedhamiria. Hizi siyo Siasa za Zitto, japo kidogo alizijaribu akiwa na Chadema lakini si kwa kiwango hiki

Ukimtazama unagundua sasa ni mtu aliyeamua rasmi kupambana na "Mfumo" kandamizi, Mfumo wa Kidikteta chini ya chama kimoja, lakini je wengine tunajiuliza, Mfumo huo ndiyo kauona leo? Kila neno analotoa juu ya Mfumo unaliona ni la ukweli mtupu, lakini je huu ni wakati wake? Jibu ni hapana

Ukweli ni kwamba harakati zake hizi ziko nje ya wakati, it's too late. Utawala huu wa mabavu mnaoulalamikia leo mliuruhusu wenyewe

Unapotaka kupambana na Mfumo ni ngumu sana kuanza papo kwa papo na ukaushinda, wenzake waliliona hili, lakini yeye aliutumia vibaya muda wake akawageuka, haya ndiyo Matunda yake. Kipindi wanafanya yale mapambano ya kuundoa Mfumo-Dola uliojengwa na CCM kipindi yuko CHADEMA ule ndio ulikuwa muda muafaka na si sasa, kipindi kile Mfumo ulikuwa umedhoofu chini ya uongozi dhaifu wa JK ndicho kilikuwa kipindi cha kuuangusha lakini si sasa ambapo mtu mmoja mwenye nguvu amakuja kutengeneza wa kwake na unaomuogopa mno, ni ngumu kuuangusha kirahisi. Ili kuuangusha inabidi kuudhoofisha kwanza, hii haitakuwa kazi rahisi kama anavyodhani Zitto

Anayokula sasa ni "matunda ya usaliti", alidhani anaikomoa CHADEMA na viongozi wake, lakini sasa ndipo anajua kumbe aliisaliti nafsi yake na Taifa lake, ile ndiyo ilikuwa saa ya ukombozi, kwa sasa atapoteza muda na Rasilimali za chama chake bure. Najua anatamani sana apate support ya vyama vingine, kwa bahati mbaya hivyo vyama vingine ndivyo alivyovisaliti kwa mara nyingine kwa kuanzisha Siasa zisizofaa kipindi cha uchaguzi matokeo yake akaipa nguvu zaidi CCM na wateule wake, hakuutambua muda muafaka wa kuunganisha nguvu

Mwisho niseme, sisemi haya kumkatisha tamaa Zitto na Chama chake lakini wengine sisi hupenda kusema ukweli, harakati za Zitto, dhamira ya dhati ya Zitto, vimekuja kwa kuchelewa. Amemaua kupambana kwa sababu yanayomfika sasa ni yale aliyozoea kuyasikia kwa wenzake, ameonja uchungu wake, kusakwa na Polisi kusiko na utaratibu hakukuwahi kumwandama kama ilivyo sasa, ya kufukuzwa Bungeni kusiko na utaratibu yalikuwa ni mambo ya akina LEMA. Hakutaka kuwa mpinzani halisi katika wakati uliofaa

Kila la kheri Zitto na ACT, lakini mko nje ya wakati, poleni kwa mikikimiki mnayopitia, Mfumo huu hautaanguka bila kuudhoofisha kwanza, mapambano haya yanahitaji mtafute nguvu ya pamoja. Poleni wapinzani kwa ujumla wenu

(1)Hatumuogopi Magufuli

Hapa inaonyesha nyuma ya Zitto kuna watu wamemtuma

(2)Wakati wa Nyerere Walipanga kumupindua Nyerere Mara nane

Hapa inaonyesha watu walionyuma ya Zitto wanafikilia kufanya mapinduzi

(3)CCM wameshindwa kumudhibiti Magufuli

Hapa inaonyesha Zitto anahudhuria vikao vya CCM kwa mlango wa Nyuma

(4)Bajeti haijapandaila Shilingi ya Tz imeshuka thamani

Wakati wa Kikwete Shilingi ilishuka kutoka Tshs1700 hadi Tshs 2300 lakini mda ule Zitto hakuona sasa leo figure hataji ila anaona

(5)Magufuli si Mwenyekiti wa CCM bado

Hapa inaonekana madai ya Gwajima ni ya Kweli
 
Saivi hakuna hela wala vyeo tena CCM hata kamati wamemnyima pamoja na kuhudhuria hotuba ya Rais ya Uzinduzi wa Bunge,inabidi tu apambane sasa afanye siasa,kibarua cha Lumumba kimeota nyasi hakuna fungu hilo tena.
 
Kila mfuatiliaji mzuri wa Siasa za hapa Tanzania ataafikiana na mimi kwamba siku kadhaa hizi Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, amekuwa moto mkali sana hasa baada ya kuanza zile vuta nikuvute Bungeni Naibu Spika alipozuia mjadala wa Wanafunzi wa UDOM ambapo ilipelekea Wabunge kadhaa wa upinzani kufungiwa vikao vya Bunge akiwemo na Zitto mwenyewe

Nasema amekuwa moto kwa sababu Siasa anazozifanya sasa ni tofauti kabisa na aina ya Siasa zake tulizozoea kuziona, yeye huwa ni mtu wa mapambano ya hoja huku akikanyaga kwa tahadhari kubwa, lakini kwa sasa hata anavyoongea tu utagundua kabisa kuna kitu, unaona kabisa ni mtu aliyeamua "lolote na liwe", hakuna tahadhari tena, ni mtu aliyedhamiria. Hizi siyo Siasa za Zitto, japo kidogo alizijaribu akiwa na Chadema lakini si kwa kiwango hiki

Ukimtazama unagundua sasa ni mtu aliyeamua rasmi kupambana na "Mfumo" kandamizi, Mfumo wa Kidikteta chini ya chama kimoja, lakini je wengine tunajiuliza, Mfumo huo ndiyo kauona leo? Kila neno analotoa juu ya Mfumo unaliona ni la ukweli mtupu, lakini je huu ni wakati wake? Jibu ni hapana

Ukweli ni kwamba harakati zake hizi ziko nje ya wakati, it's too late. Utawala huu wa mabavu mnaoulalamikia leo mliuruhusu wenyewe

Unapotaka kupambana na Mfumo ni ngumu sana kuanza papo kwa papo na ukaushinda, wenzake waliliona hili, lakini yeye aliutumia vibaya muda wake akawageuka, haya ndiyo Matunda yake. Kipindi wanafanya yale mapambano ya kuundoa Mfumo-Dola uliojengwa na CCM kipindi yuko CHADEMA ule ndio ulikuwa muda muafaka na si sasa, kipindi kile Mfumo ulikuwa umedhoofu chini ya uongozi dhaifu wa JK ndicho kilikuwa kipindi cha kuuangusha lakini si sasa ambapo mtu mmoja mwenye nguvu amakuja kutengeneza wa kwake na unaomuogopa mno, ni ngumu kuuangusha kirahisi. Ili kuuangusha inabidi kuudhoofisha kwanza, hii haitakuwa kazi rahisi kama anavyodhani Zitto

Anayokula sasa ni "matunda ya usaliti", alidhani anaikomoa CHADEMA na viongozi wake, lakini sasa ndipo anajua kumbe aliisaliti nafsi yake na Taifa lake, ile ndiyo ilikuwa saa ya ukombozi, kwa sasa atapoteza muda na Rasilimali za chama chake bure. Najua anatamani sana apate support ya vyama vingine, kwa bahati mbaya hivyo vyama vingine ndivyo alivyovisaliti kwa mara nyingine kwa kuanzisha Siasa zisizofaa kipindi cha uchaguzi matokeo yake akaipa nguvu zaidi CCM na wateule wake, hakuutambua muda muafaka wa kuunganisha nguvu

Mwisho niseme, sisemi haya kumkatisha tamaa Zitto na Chama chake lakini wengine sisi hupenda kusema ukweli, harakati za Zitto, dhamira ya dhati ya Zitto, vimekuja kwa kuchelewa. Amemaua kupambana kwa sababu yanayomfika sasa ni yale aliyozoea kuyasikia kwa wenzake, ameonja uchungu wake, kusakwa na Polisi kusiko na utaratibu hakukuwahi kumwandama kama ilivyo sasa, ya kufukuzwa Bungeni kusiko na utaratibu yalikuwa ni mambo ya akina LEMA. Hakutaka kuwa mpinzani halisi katika wakati uliofaa

Kila la kheri Zitto na ACT, lakini mko nje ya wakati, poleni kwa mikikimiki mnayopitia, Mfumo huu hautaanguka bila kuudhoofisha kwanza, mapambano haya yanahitaji mtafute nguvu ya pamoja. Poleni wapinzani kwa ujumla wenu
Dah umetema madini utafikiri umetumwa uongee kuwakilisha mawazo ya watu wengi...Kipindi kile wenzake wanaandama yeye hata siku moja hakuwahi kuandamana wala kuwekwa ndani,wala kupigwa...simuamini zitto lakini pia simdharau..ni mwanasiasa mwenye aikli mno na fundi wa kujenga hoja.Katika hili la kupambana na system namuunga mkono.Kwenye siasa hakuna adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu.Kanyaga twende tutajua mbele ya safari baada ya kufanikiwa ...
 
ni kweli na wazi kuwa zito alichezea wakati wake! sasa hali siyo ile iliyokuwepo enzi zile!..Zito hana tofauti sana na muheshimiwa mukulu ...akipewa nchi hii..itakuwa mbovu kuliko ilivyo sasa!
 
Kila mfuatiliaji mzuri wa Siasa za hapa Tanzania ataafikiana na mimi kwamba siku kadhaa hizi Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, amekuwa moto mkali sana hasa baada ya kuanza zile vuta nikuvute Bungeni Naibu Spika alipozuia mjadala wa Wanafunzi wa UDOM ambapo ilipelekea Wabunge kadhaa wa upinzani kufungiwa vikao vya Bunge akiwemo na Zitto mwenyewe

Nasema amekuwa moto kwa sababu Siasa anazozifanya sasa ni tofauti kabisa na aina ya Siasa zake tulizozoea kuziona, yeye huwa ni mtu wa mapambano ya hoja huku akikanyaga kwa tahadhari kubwa, lakini kwa sasa hata anavyoongea tu utagundua kabisa kuna kitu, unaona kabisa ni mtu aliyeamua "lolote na liwe", hakuna tahadhari tena, ni mtu aliyedhamiria. Hizi siyo Siasa za Zitto, japo kidogo alizijaribu akiwa na Chadema lakini si kwa kiwango hiki

Ukimtazama unagundua sasa ni mtu aliyeamua rasmi kupambana na "Mfumo" kandamizi, Mfumo wa Kidikteta chini ya chama kimoja, lakini je wengine tunajiuliza, Mfumo huo ndiyo kauona leo? Kila neno analotoa juu ya Mfumo unaliona ni la ukweli mtupu, lakini je huu ni wakati wake? Jibu ni hapana

Ukweli ni kwamba harakati zake hizi ziko nje ya wakati, it's too late. Utawala huu wa mabavu mnaoulalamikia leo mliuruhusu wenyewe

Unapotaka kupambana na Mfumo ni ngumu sana kuanza papo kwa papo na ukaushinda, wenzake waliliona hili, lakini yeye aliutumia vibaya muda wake akawageuka, haya ndiyo Matunda yake. Kipindi wanafanya yale mapambano ya kuundoa Mfumo-Dola uliojengwa na CCM kipindi yuko CHADEMA ule ndio ulikuwa muda muafaka na si sasa, kipindi kile Mfumo ulikuwa umedhoofu chini ya uongozi dhaifu wa JK ndicho kilikuwa kipindi cha kuuangusha lakini si sasa ambapo mtu mmoja mwenye nguvu amakuja kutengeneza wa kwake na unaomuogopa mno, ni ngumu kuuangusha kirahisi. Ili kuuangusha inabidi kuudhoofisha kwanza, hii haitakuwa kazi rahisi kama anavyodhani Zitto

Anayokula sasa ni "matunda ya usaliti", alidhani anaikomoa CHADEMA na viongozi wake, lakini sasa ndipo anajua kumbe aliisaliti nafsi yake na Taifa lake, ile ndiyo ilikuwa saa ya ukombozi, kwa sasa atapoteza muda na Rasilimali za chama chake bure. Najua anatamani sana apate support ya vyama vingine, kwa bahati mbaya hivyo vyama vingine ndivyo alivyovisaliti kwa mara nyingine kwa kuanzisha Siasa zisizofaa kipindi cha uchaguzi matokeo yake akaipa nguvu zaidi CCM na wateule wake, hakuutambua muda muafaka wa kuunganisha nguvu

Mwisho niseme, sisemi haya kumkatisha tamaa Zitto na Chama chake lakini wengine sisi hupenda kusema ukweli, harakati za Zitto, dhamira ya dhati ya Zitto, vimekuja kwa kuchelewa. Amemaua kupambana kwa sababu yanayomfika sasa ni yale aliyozoea kuyasikia kwa wenzake, ameonja uchungu wake, kusakwa na Polisi kusiko na utaratibu hakukuwahi kumwandama kama ilivyo sasa, ya kufukuzwa Bungeni kusiko na utaratibu yalikuwa ni mambo ya akina LEMA. Hakutaka kuwa mpinzani halisi katika wakati uliofaa

Kila la kheri Zitto na ACT, lakini mko nje ya wakati, poleni kwa mikikimiki mnayopitia, Mfumo huu hautaanguka bila kuudhoofisha kwanza, mapambano haya yanahitaji mtafute nguvu ya pamoja. Poleni wapinzani kwa ujumla wenu
Isingekuwa rahisi kwa kipindi alipokuwa CDM kuweza kuyafanya haya anayoyafanya sasa.
Ukiangalia mtazamo na msimamo wa kisiasa wa CDM na ACT kuna tofauti kubwa.
Lkn pia isingekuwa rahisi kwake kupata support kubwa ndani ya CDM kama ambayo anaipata sasa ndani ya ACT kwa kuzingatia mazingira alokuwa nayo ndani ya CDM.
 
lini zitto amefanya siasa za kuiga? mlitaka muandamane naye kwenda kunywa chai ikulu? Mbona maandamano mnayoyafanya mmechagua baadhi ya miji?. Kwa mtazamo wangu ni muda sahihi tu,maana zile siasa za kubebana mzobamzoba kutoana kwenye vikao hazijawahi kubadl chochote hata kwenye sheria zetu . Acheni kujidhania ni bora kuliko wengine. Kama unaona maandamano ni bora we endelea nayo
 
Zitto Kabwe, Mwanasiasa makini kama alivyo, mwenye upeo kama alivyo, mjenga hoja kama alivyo. Wengi walitamani aendelee kuwepo CHADEMA lakini baadae ilishindikana. CHADEMA hawakuwahi kumuamini. Chanzo cha ugomvi wao ni kwamba Zitto alikuwa anawauza. Waliamini kuwa alikuwa na urafiki wa karibu na Rais aliyepita. Inawezekana ndio maana Zitto hakuwahi kutoa post nyingi mfululizo za kumchapa Rais aliyepita moja kwa moja kama anavyofanya katika utawala huu. Alideal zaidi na skendo za Bunge ambazo hazikuwa na athari kubwa kwa Rais moja kwa moja zaidi ya zile ambazo zilikuwa zinamtaka Rais afanye mabadiliko. Hata alipoondoka CHADEMA wenye Chama kile Waliamini kuwa Zitto angekuwa mpinzani wa wapinzani. Ilianza kuonekana alipobaki bungeni wakati wenzake walipotoka nje siku Rais wa sasa alipokuwa akifungua bunge. Na Rais huyu alimsifia kuwa alikuwa mpinzani wa kweli. Hata hivyo dakika moja baada Rais wa sasa kutoa mguu wake bungeni na kuanza kazi ya Urais ni wazi kwamba amejitofautisha sana na Rais aliyepita kimisimamo na kifikra. Kabla safari haijafika mbali, Zitto amekuwa mpinzani hasa wa moja kwa moja dhidi ya Rais wa sasa. Anapost mara nyingi zaidi. Na kama ilivyo kawaida yake, Anapost mantiki sana. Hata kihisia anaonekana kuwa mpinzani halisi na ameonja machungu ya utawala huu. Kafungiwa vikao vya bunge. Kasakwa na polisi usiku na mchana. Dakika za mwisho za utawala uliopita mambo haya yasingemtokea Zitto. Mantiki ya kijinga ya makala hii ni kuwaza tu kama Rais wa sasa angeingia madarakani baada ya kuondoka tu kwa Rais Ben Mkapa huenda Zitto angekuwa bado CHADEMA. Mapambano anayopitia sasa Zitto ndio ambayo CHADEMA wamepitia utawala uliopita na watapitia utawala huu. Wasingeishi kwa hofu ya kutoaminiana, kuonana wasaliti kwa system, mpaka wakafukuzana mahakamani. Adui yao angekuwa mmoja. Lakini katika utawala uliopita Zitto na CHADEMA waligeuzana maadui badala ya kumtazama adui. It's too late. Unavyodhani, Zitto wa leo Ukawa wakitoka nje ya bunge yeye atabakia ndani?.....Edo Kumwembe.
 
Zitto hajawahi kuwa msaliti, Zitto alikuwa na ugomvi na Mbowe kuutaka uenyekiti wa chama kitu ambacho ni MUHALI kwa mbowe kuachia
 
ni kweli na wazi kuwa zito alichezea wakati wake! sasa hali siyo ile iliyokuwepo enzi zile!..Zito hana tofauti sana na muheshimiwa mukulu ...akipewa nchi hii..itakuwa mbovu kuliko ilivyo sasa!
Tatizo lililopo ni kuwa serikali ya sasa haina cheo cha MSALITI anayeajiriwa kutoka chama au vyama vya upinzani ili atoe siri za upinzani kwa serikali halafu alipwe mapesa mengi. Sasa wale wapinzani waliokuwa na ajira hizo baada ya kuzikosa katika awamu hii wanafanya jitihada zote kumpinga Magufuli ili labda awaajiri ndio waache kimshutumu. Je Mh. Magufuli atatoa hiyo ajira kupitia TISS?
 
Back
Top Bottom