Hofu ya Watawala: Polisi Wamezuia Mkutano wa Mbunge Ilemela

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Polisi (kinyume na sheria inayosimamia mikutano ya hadhara), wamezuia mkutano wangu wa hadhara uliokuwa umepangwa na kuandaliwa kufanyika leo Wilaya ya Ilemela.

Hakuna sababu yoyote ya maana zaidi ya mwendelezo wa utawala unaokiuka sheria na kuvunja misingi ya demokrasia na hatimaye ustawi wa jamii.

...
Sababu nyingine ni hofu. Hii ni dalili ya kuwa utawala huu umejawa na hofu sana. Hofu kuanzia kwenye ukweli kuwa hawakushinda uchaguzi. The guilty are afraid.

Wana hofu na namna wanavyoendesha serikali. Hawajiamini. Wanajua kupitia mikutano hii wananchi wataambiwa ukweli kuhusu kukwama kwa bajeti hewa ya serikali, utawala wao unavyosababisha hali ngumu ya maisha kwa wananchi kwa mikakati mibovu ya kutekeleza sera za uchumi, utawala wao unavyokiuka haki za binadamu kwa kupuuza Katiba na Sheria za nchi.

Wana hofu kuwa kwenye mikutano hii wataumbuliwa namna ambavyo wanaipeleka nchi katika hali mbaya kwa kauli na matamko yanayotishia mstakabali wa nchi na umoja wa kitaifa.

Ukweli ni kwamba sababu zote alizotumia OCD huyo wa Ilemela si za msingi na sheria hampi kabisa mamlaka ya kuzuia mkutano wa hadhara bali amefanya hivyo kwa maelekezo aliyopewa baada ya kuuliza afanye nini!

Taarifa nilizonazo ni kwamba Mbunge wa Jimbo la Ilemela hana mkutano wowote leo jimboni kwake achilia mahali hapo palipotajwa. Lakini hata kama angekuwa nao ofisi yangu ilikuwa imeshabadili eneo la mkutano na kupeleka taarifa kwa DED na OCD kuwa tutatumia Uwanja wa Sabasaba.

OCD alipoamua kujibu hiyo barua (siku tatu baadae hali inayoonesha kuwa alikuwa anatafuta maelekezo kwanza), akajibu barua moja tu ya awali iliyokuwa inazungumzia Uwanja wa Stendi Pasiansi ambao tuliamua kuucha kwa sababu siku hizi umekuwa mdogo kutokana na ujenzi wa barabara unaoendelea barabara ya kwenda Airport.

Ofisi yangu ilipowasiliana naye kumweleza kuwa mbona kajibu barua moja tu ya zamani na kwamba pia hana mamlaka ya kuzuia mkutano bali ku-regulate kwa kufanya majadiliano kuhusu muda au mahali, akawa mkali akisema kuwa mkutano ukifanyika yeye atatumia PLAN B kuhakikisha haufanyiki.

Hiyo plan B anayoijua yeye, haikuweza kutumika kufanikisha mkutano?

Kwa hiyo, hofu haiko tu kwa mkubwa wao. Imeshuka hadi kwa baadhi ya wabunge wao. Hawajiamini. Wanajua hwakubaliki kwa wananchi. Wanadhani kuzuia sisi kukutana na wananchi kutawapatia ahueni wao.

Jitihada za ofisi ya Mbunge kuwasiliana na mamlaka zingine kuhakikisha mkutano huu uliopangwa kufanyika leo hadi sasa hazijafanikiwa kwa bahati mbaya maamuzi yanapaswa kufanywa na makada wa CCM walioko serikalini hapo mkoani.

Kwamba polisi wamefikia hatua hawana uwezo wa kusimamia sheria, weledi wa kazi yao kwa jambo ambalo liko ndani ya uwezo wao kisheria, hadi wapate maelekezo ya wanasiasa ni jambo la hatari sana katika kusimamia misingi ya haki nchini.
 

Attachments

  • Chadema1.jpg
    Chadema1.jpg
    37.2 KB · Views: 151
  • Chadema2.jpg
    Chadema2.jpg
    6.1 KB · Views: 50
  • Chadema3.jpg
    Chadema3.jpg
    30 KB · Views: 46
  • Chadema4.jpg
    Chadema4.jpg
    6.3 KB · Views: 41
  • Chadema6.jpg
    Chadema6.jpg
    21.1 KB · Views: 46
Hii haingii akilini. Mpaka leo inteligensia inaonyesha kuna watu watafanya vurugu kwenye mikutano ya wapinzani tu lakini hawakamatwi? Polisi wakiendelea hivi watashangaa vurugu zitakuwa zitatokea kwenye mikutano ya CCM pamoja na kwamba "intelijensia" yao haionyeshi hivyo. Tusifikie huko.
 
Hii haingii akilini. Mpaka leo inteligensia inaonyesha kuna watu watafanya vurugu kwenye mikutano ya wapinzani tu lakini hawakamatwi? Polisi wakiendelea hivi watashangaa vurugu zitakuwa zitatokea kwenye mikutano ya CCM pamoja na kwamba "intelijensia" yao haionyeshi hivyo. Tusifikie huko.
Acha kukurupuka, mkutano uliozuiwa ni wa mbunge wa CCM jumbo la Ilemela.
 
Cdm nao mmeona hii nayo Hoja!!
Mnapaswa kuelewa Sasahivi hakuna cha ccm cdm wala nani
ni Tanzania kwanza.
Mkutano ukiwa na mashaka uwe wa ccm au cdm
lazima polisi wauzuie
 
Acha kukurupuka, mkutano uliozuiwa ni wa mbunge wa CCM jumbo la Ilemela.

Kwa hiyo barua ya huyu mbunge wa CCM ataichukulia kwa mbunge wa viti maalum chadema sio? Nakusamehe bure kwa sababu chama chenu kimejaa mabashite msiojua hata kusoma. Hata huyo aliyeandika barua naye fafafa tu, barua kapokea 2017 ye analeta 2014.
chadema1-jpg.490005
 
Upinzani mnasikitisha sana. Huyo aliyetaka kuongea na wananchi yaani hakuna hata jambo moja la kimaendeleo kwao, bali ni kutaka kudakia ya CCM na kuongea kuipinga. Yaani viongozi wa upinzani bado kabisa, bora hata polisi wamezuia kwa sababu wamewaokoa msijiaibishe kwa kuongelea uliyoyaandika. Mna kazi kubwa sana ya kujipanga, nimesoma nikifikiri ningekuta mazuri kumbe blah blah blah. Muache tamaa, kunyanyasana, n.k.
 
Upinzani mnasikitisha sana. Huyo aliyetaka kuongea na wananchi yaani hakuna hata jambo moja la kimaendeleo kwao, bali ni kutaka kudakia ya CCM na kuongea kuipinga. Yaani viongozi wa upinzani bado kabisa, bora hata polisi wamezuia kwa sababu wamewaokoa msijiaibishe kwa kuongelea uliyoyaandika. Mna kazi kubwa sana ya kujipanga, nimesoma nikifikiri ningekuta mazuri kumbe blah blah blah. Muache tamaa, kunyanyasana, n.k.
Kugawa milioni 20 hovyo hovyo ndio kuleta maendeleo kwa watu?
 
Upinzani mnasikitisha sana. Huyo aliyetaka kuongea na wananchi yaani hakuna hata jambo moja la kimaendeleo kwao, bali ni kutaka kudakia ya CCM na kuongea kuipinga. Yaani viongozi wa upinzani bado kabisa, bora hata polisi wamezuia kwa sababu wamewaokoa msijiaibishe kwa kuongelea uliyoyaandika. Mna kazi kubwa sana ya kujipanga, nimesoma nikifikiri ningekuta mazuri kumbe blah blah blah. Muache tamaa, kunyanyasana, n.k.
Unajua kazi za opposition party? Unajua wajibu wako kama RAIA wa Tanzania? Unajua haki zako kikatiba? Unajua mipaka ya kisheria kwenye vyama vya siasa na sheria iliyounda jeshi LA polisi? Unajua sheria uliyoanzisha vyama vya siasa? Ukipata majibu nishilikishe
 
Hao maOCD ni zero kabisa. Siku zote inteligensia inaripoti mikutano ya upinzani tu na Huo wa Mabulla hautodhuriwa na magaidi

Sent from my TECNO P5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom