KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 19,166
- 37,178
Habari za wakati huu huu wandugu na majamaa.....
Siku hizi imekuwa ni jambo la kawaida kukuta mwanamke yupo singo hata katika umri ambao angetazamiwa kuwa ameshaolewa....
Au imekuwa ni kawaida kukuta mwanamke akiwa na mtoto au watoto huku akiwa peke yake....na wengi wao huonekana wanafurahia hali hiyo.....hili jambo wadau wengi wa masuala ya kijamii wamekuwa wakilielezea kuegemea upande wa kuwalaumu wanawake tu kana kwamba ni watu wenye tabia mbaya na hizo mimba walijipa wenyewe.....
Kiukweli hii hali haikujitokeza tu kwa bahati mbaya au kwa kuzuka tu....hii ni hali ambayo kwa namna fulani imeundwa na hali ya wanaume kuyakataa au kuyakimbia majukumu yao.......
Iko wazi kuwa miaka hii au zama hizi wanaume wamepoteza sifa na sababu za wao kuwa viongozi wa familia kwa kuwa na upeo mdogo wa kukabiliana na majukumu ya kifamilia......hata humu kuna kesi kibao za vijana wa kiume wakiomba ushauri kuhusu familia zao katika masuala ambayo mtu hata kwa akili ya kawaida mtu unashindwa kuelewa kuwa kama baba wa familia anashindwa kutatua suala dogo kama hilo je hiyo familia anaiendeshaje....???
Miaka ya nyuma ilikuwa ni jambo la kujivunia kwa mwanamke kuolewa na kuwa na familia yake na lilikuwa ni jambo la kishujaa kwa mwanamume kuweza kumudu kuihudumia familia yake katika mahitaji yao yote ya msingi...
Kwa familia ilikuwa ni fedheha kwa mtoto wao wa kike kutokuolewa...lilikuwa ni tukio la kuwafanya wazazi au wanafamilia waende mbali zaidi hata kwenye mambo ya kishirikina yote ni kutafuta kujua kwanini binti yao haolewi.......
Lakini nyakati hizi kutokana na mienendo mibovu ya wanaume kwenye ndoa imewafanya wanawake wasione umuhimu wa kuwa na mume achilia mbali kuishi na mwanamume......
Kila kukicha vyombo vya habari vinatawaliwa na habari za mwanamume kumfanyia mkewe ukatili usioelezeka......
Kila siku wanawake wanasikia habari mbaya za wakina mama wanaoteseka kwa mateso baada ya kutelekezwa na waume zao.....
Kila uchao kunazuka taarifa za vijana wanaokataa mimba au wanawake wanao pata maradhi baada kuchukua maamuzi ya kutoa mimba baada kusalitiwa na wale waliodhani ni wenzi wao(wanaume)
Katika mazingira kama hayo unategemea kuna mwanamke gani mwenye ujasiri wa kuwa na hamu ya kuingia kwenye ndoa...ikizingatia kuwa wengi wao wanajiweza kiuchumi.......
Hali iliyopo ya wanawake kutaka kuwa sawa na wanaume ni kutokana wanaume kuyakimbia majukumu yao na kuwaachia wanawake.....na huu ni udhaifu mkubwa sana ambao wanaume tunauonyesha....kwa wanawake....
Fikiria kuwa ikiwa mwanamke anamudu gharama za kuitunza familia na kuipatia mahitaji yote ya msingi baada ya kutelekezwa na mumewe ataachaje kujiona sawa na mwanaume ikiwa majukumu yote ya mwanaume kwenye familia anayafanya yeye mwenyewe na kuyamudu....???
Nisiendelee mbali ila ninachowakumbusha wanaume wenzangu turudi kwenye mstari na tusimame kwenye majukumu yetu na kuyatiniza ipasavyo kamwe hutasikia wanawake wakidai usawa....kwa huo usawa utafunikwa na huduma atakazopewa na mumewe.......
Nawasilisha......
Siku hizi imekuwa ni jambo la kawaida kukuta mwanamke yupo singo hata katika umri ambao angetazamiwa kuwa ameshaolewa....
Au imekuwa ni kawaida kukuta mwanamke akiwa na mtoto au watoto huku akiwa peke yake....na wengi wao huonekana wanafurahia hali hiyo.....hili jambo wadau wengi wa masuala ya kijamii wamekuwa wakilielezea kuegemea upande wa kuwalaumu wanawake tu kana kwamba ni watu wenye tabia mbaya na hizo mimba walijipa wenyewe.....
Kiukweli hii hali haikujitokeza tu kwa bahati mbaya au kwa kuzuka tu....hii ni hali ambayo kwa namna fulani imeundwa na hali ya wanaume kuyakataa au kuyakimbia majukumu yao.......
Iko wazi kuwa miaka hii au zama hizi wanaume wamepoteza sifa na sababu za wao kuwa viongozi wa familia kwa kuwa na upeo mdogo wa kukabiliana na majukumu ya kifamilia......hata humu kuna kesi kibao za vijana wa kiume wakiomba ushauri kuhusu familia zao katika masuala ambayo mtu hata kwa akili ya kawaida mtu unashindwa kuelewa kuwa kama baba wa familia anashindwa kutatua suala dogo kama hilo je hiyo familia anaiendeshaje....???
Miaka ya nyuma ilikuwa ni jambo la kujivunia kwa mwanamke kuolewa na kuwa na familia yake na lilikuwa ni jambo la kishujaa kwa mwanamume kuweza kumudu kuihudumia familia yake katika mahitaji yao yote ya msingi...
Kwa familia ilikuwa ni fedheha kwa mtoto wao wa kike kutokuolewa...lilikuwa ni tukio la kuwafanya wazazi au wanafamilia waende mbali zaidi hata kwenye mambo ya kishirikina yote ni kutafuta kujua kwanini binti yao haolewi.......
Lakini nyakati hizi kutokana na mienendo mibovu ya wanaume kwenye ndoa imewafanya wanawake wasione umuhimu wa kuwa na mume achilia mbali kuishi na mwanamume......
Kila kukicha vyombo vya habari vinatawaliwa na habari za mwanamume kumfanyia mkewe ukatili usioelezeka......
Kila siku wanawake wanasikia habari mbaya za wakina mama wanaoteseka kwa mateso baada ya kutelekezwa na waume zao.....
Kila uchao kunazuka taarifa za vijana wanaokataa mimba au wanawake wanao pata maradhi baada kuchukua maamuzi ya kutoa mimba baada kusalitiwa na wale waliodhani ni wenzi wao(wanaume)
Katika mazingira kama hayo unategemea kuna mwanamke gani mwenye ujasiri wa kuwa na hamu ya kuingia kwenye ndoa...ikizingatia kuwa wengi wao wanajiweza kiuchumi.......
Hali iliyopo ya wanawake kutaka kuwa sawa na wanaume ni kutokana wanaume kuyakimbia majukumu yao na kuwaachia wanawake.....na huu ni udhaifu mkubwa sana ambao wanaume tunauonyesha....kwa wanawake....
Fikiria kuwa ikiwa mwanamke anamudu gharama za kuitunza familia na kuipatia mahitaji yote ya msingi baada ya kutelekezwa na mumewe ataachaje kujiona sawa na mwanaume ikiwa majukumu yote ya mwanaume kwenye familia anayafanya yeye mwenyewe na kuyamudu....???
Nisiendelee mbali ila ninachowakumbusha wanaume wenzangu turudi kwenye mstari na tusimame kwenye majukumu yetu na kuyatiniza ipasavyo kamwe hutasikia wanawake wakidai usawa....kwa huo usawa utafunikwa na huduma atakazopewa na mumewe.......
Nawasilisha......