Hivi yupo wapi msanii Tekno wa kipindi cha nyuma

Xavi Hernandez Alcantara

JF-Expert Member
Oct 19, 2019
278
280
Siku ya kwanza nasikia ngoma inaitwa Duro kutoka kwa Tekno nikasema hii ni hit haiitaji maelezo.

Hakuishia hapo zilifuata ngoma zilizonamba Afrika na zikavuka boda mastaa kibao wa Mamtoni walijirekodi wakicheza.

Hivi yupo wapi Tekno wa kipindi cha nyuma..
Tekno ya Duro, Wash, Diana, Pana, Where, Go, Jogodo, Yawa N.k

Kwa speed ya kipindi kile cha nyuma kidogo Afrika ilianza kumtabiria makubwa kwamba anakuja kuuvunja ufalme wa Davido na StarBoy Wizkid. Japo inaitaji ulale Studio kuwamaliza hao jamaa.

Kwa sasa Naona Tekno Amerudi nyuma kidogo sisikii hit kama zile za mwanzo. hii ngoma yake mpya na Zlatan ina miezi kama miwili na bado ina Views Million 3 youtube.

Wakati Mkwaju kama Pana umejizolea Youtube Viewa milion 115.

Game Ngumu? Au kalizika? Au kuna Jambo linakuja kutoka kwa Tekno?
 
Back
Top Bottom