Hivi Watanzania nani atatukomboa?

Hivi Watanzania nani atatukomboa?

7 5 mm

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2014
Posts
352
Reaction score
200
Ni jambo linalotia hasira sana kusikia udharimu unaofanyika ndani ya hii nchi.

Watanzania tumefanywa watoto wadogo wanaomlilia mama yao halafu anawanyamazisha kwa pipi wakat yeye amejikusanyia vitu kibao vyenye thaman.

Inasikitisha kuona mfanya kazi analipwa mshahara chini ya laki3 kwa mwez wakat wabunge wanachukua zaidi ya laki3 kwasiku, inasikitisha kuona mwalimu halipwi mshahara wake kwa wakat huku akikandamizwa na kodi kubwa wakat mawaziri hawakatwi kodi pamoja na kulipwa mamilion ya pesa.

Inasikitisha kumgandamiza mfanyabiashara mdogo kwa kumtoza kodi kubwa wakat makampuni mbalimbali yanasamehewa kodi.

Inasikitisha kuona raslimali znaibiwa na hawa tunaowaita viongoz wetu wakat mtanzania anaishi maisha ya chini na kimaskini.

Huu ni wakat wa kuisaka haki kwa kuingia msituni, tutakuwa waoga mpaka lini?

Hebu tuige wenzetu kama V.I Lenini na Joseph Stallin waliyoyafanya huko Urusi woga wetu ndio umaskin wetu, tutakuwa watu wenye kulia miaka yote lakin hakuna atakaye tukomboa tusipotoa jasho na damu.
 
toka kwenye keyboard anza wewe kuingia msituni uone muziki wake,,we unajificha nyuma ya keyboard halafu unaongea pumba hapa
 
Tanzania ina kila kitu isipokuwa watanzania wenyewe ndio hawapo
 
wanasiasa wote ni walewale

Changes start with you, huwezi kusema wanasiasa wote ni walewale wakati ambapo wengine hujawapa fursa ya kuongoza nchi. Wenzetu nchi jirani hawana msemo huo, wanafanya mabadiliko kila uchaguzi ujapo.
 
Bado shaka na hvi vyama vyote vya siasa maaana shame kikisimama imara tayari mdudu wa furugu anaingia daaah!! Tanzania chungu cha majungu na fitina kweli nani alale njaa ili amuokoe mwenzake?? Jibu ni hakuna tutabaki hapa hapa !!!
 
Ndio. Mkituchagua 2015 tutamlipa kima cha chini 600,000. Halafu wabunge posho sh 2,000,000/.
 
Turufu ya mabadiliko unayo mwenyewe, hebu washawishi familia yako wapige kura ya mabadiliko 2015.

Shemeji umenifrahisha. Wengi hawapigi kura, baadae utaskia wameiba wakati ya kwake haikuwepo
 
Shemeji umenifrahisha. Wengi hawapigi kura, baadae utaskia wameiba wakati ya kwake haikuwepo

Mh. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka ndiyo atakayeweza kutuokoa Watanzania. Uongozi wake ni wa utukufu zaidi. Yupo poa sn ni msomi, mchapakazi, mpenda maendeleo, mzalendo n.k
 
Mh. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka ndiyo atakayeweza kutuokoa Watanzania. Uongozi wake ni wa utukufu zaidi. Yupo poa sn ni msomi, mchapakazi, mpenda maendeleo, mzalendo n.k

Yule wa mama Kigamboni? C yule huwa anapenda kusema “au sio?” Yule wa Muleba yule etii?

Kama ndo hyo sitampigia 😱😱😱
 
Mh. Prof. Anna Kajumulo Tibaijuka ndiyo atakayeweza kutuokoa Watanzania. Uongozi wake ni wa utukufu zaidi. Yupo poa sn ni msomi, mchapakazi, mpenda maendeleo, mzalendo n.k

Tibaijuka yupi, huyo aliyepo wizara ya ardhi au? Tibaijuka pamoja na kuwa ni waziri wa ardhi anajenga nyumba kule makongo kwenye road reserve na kufanya barabara ya lami isijengwe na watu wa makongo kuhangaika kwa barabara mbovu
 
Back
Top Bottom