Hivi kwanini tunakufa?

Hivi kwanini tunakufa?

Mcqueenen

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2019
Posts
7,260
Reaction score
12,611
Dah wakuu, sasa hivi hapa nilikuwa natembea tembea, mara ghafla nyumba jirani nasikia watu wazima wanalia kama watoto.

Haina hata haja ya kuuliza unajua tu nini kimetokea, Hivi kwanini tunakufa?
Yani unazaliwa ili ufe?

Mungu kwanini asingeweka hata alternative jamani? Mimi wazazi wote wapo ila huwa nawaza sana zamu yangu kuwalilia!

Kama sio mimi kuwalilia wao basi wao watanililia mimi, ila kulia haikwepeki.
Nini maana yake? Kwanini lakini?Aaaarghhhhhh Aaaaaaaaarggggh
This is not fair aise!
 
Una akili sana!! Kifo kipo tu kama ukumbusho kifo kipo mda wowote ule ila Kuna stage inafika nasi tunakuwa tunangojea kufa yaani miaka mingi ukifika kama utajaaliwa kuanzia 100 utakuwa umechoka ....so lipi la kujifunza? Ni kwamba hapa duniani ni sehemu tu tunaishi japokuwa tuna utofauti wa elimu, dini, utaifa, kipato ,akili na maendeleo but final njia yetu ni moja kwamba despite ya vitu vyote ivyo sisi sote tuko sawa na njia ni moja ...

Nini tufanye haijalishi itakuwaje ila lazima tuishi kwa upendo, tupunguze majigambo, kiburi ,ujuaji , dharau na kujifanya tuko juu...unaweza kuvimba hapa uko safi kesho tu umeparalyze huwezi hata kunyanya kidole cha mkono ni nusu ya maiti kabisa hapo ujanja kwisha.....Tutafute pesa na maishi bila kumkwaza mtu tutumie njia za halali tuache dhuluma ,utapeli , uwizi yote yanaweza kupelekea mwisho mbaya..


La mwisho hatujui Lin tunakufa ila tuombe mwisho mwema kwa uwezo MUNGU.
 
ila Kuna watu wapo stoo na mmezika mabox mkijua Ni wao.
Unseen realm pigo kwetu wadhambi
 
Tunakufa Ili tuwapishe wengine wapate kuishi, hebu waza kizazi Cha Nuhu kingekuwepo, kizazi cha Ibrahim, kizazi cha sodma na gomora, kizazi Cha Musa, kizazi Cha kina Samson, na Delilah wewe ungekuwepo?
 
Tunapokula samaki au nyama ya ng'ombe pia huwa najiuliza Ina maana ningekuwa kuku ningeshachonjwa
Dah inasikitisha, Kwasababu ukiondoa ile ego ya ubinadamu (kutokana na kuwa sisi tuna ubongo mkubwa)....Kimsingi Hatuna tofauti na hao wanyama😐
 
Back
Top Bottom