Hivi kwanini Star Times mnakua wahuni kiasi hiki?

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,493
54,900
Wiki iloisha nlienda kununua king'amuzi 50,000. Nikaambiwa ntakuta channel 30, cha ajabu nafika home home nakuta channel 15. kuwapigia wakanambia nunua antena. nikanunua antena 20,000 lakini ikawa vilevile. kuwauliza wakasema nimelipia 9000 so nilipie 18000 ili nione zote 30. kuwabana maswali wakanambia "nimechukua king'amuzi cha kukodi yaani wamenikodisha kwa dhamana ya 39000 kwa mwaka so hadi local channels inabidi niwe nalipia" nikashangaa!. so jana sikuona mpira. ntanunua kingine. mia
 
hadi local chanel huwe unazilipia? ..kumbe ndo maana huku chenga tupu,alafu mbona walisema local ni free? pasua kichwa!!
 
Jamaa wahuni sana, bora uwe na dish, mimi mwenyewe ninacho cha kukodi, lakini hakishiki wakaniambia nitumie antena ya nje nikafanikiwa kupata channel 3 tu nilivyowapigia wakaniambia nielekezee kisalawe, nikawaambia kisalawe sipajui, na kwa nini ving'amuzi vyao havina GPS ili niweze kujua kisalawe direction wakakosa jibu, so ninaking'amuzi ila useless najiandaa kufunga Dish nikipata mafao yangu ya uzeeni
 
hadi local chanel huwe unazilipia? ..kumbe ndo maana huku chenga tupu,alafu mbona walisema local ni free? pasua kichwa!!

bila kulipia sioni. walinambia nikimaliza mwaka nikirudishe lakini niwe nmelipia miezi 10 mfululizo. kinacho niuma sioni channel ya watoto wala santnta. wameniwekea za kichinachina. nina hasira ka nini. mia
 
Cheap is expensive

kweli aisee!. mi nikawa naona matangazo tu. kumbe unatakiwa ununue kwa 78000/-. nikawambia basi niwarudishie hiki niwaongeze hela mnipe kizuri hawataki. hapa inabidi nijipange nichukue easy tv tu. sijui hii chuma chakavu ntaiuza wapi. mia
 
Jamaa wahuni sana, bora uwe na dish, mimi mwenyewe ninacho cha kukodi, lakini hakishiki wakaniambia nitumie antena ya nje nikafanikiwa kupata channel 3 tu nilivyowapigia wakaniambia nielekezee kisalawe, nikawaambia kisalawe sipajui, na kwa nini ving'amuzi vyao havina GPS ili niweze kujua kisalawe direction wakakosa jibu,

nami wakanambia nielekeze kisalawe. nikawauliza ving'amuzi vyenu kama vinashika kisalawe kwanini mniuzie huku dar? wakakaa kimya!. mia
 
kweli aisee!. mi nikawa naona matangazo tu. kumbe unatakiwa ununue kwa 78000/-. nikawambia basi niwarudishie hiki niwaongeze hela mnipe kizuri hawataki. hapa inabidi nijipange nichukue easy tv tu. sijui hii chuma chakavu ntaiuza wapi. mia
Easy tv ndo mpango mzima sasa hivi
 
Acha bana, wazee waliopo kwenye system wanaomba wapunguze umri ili waendelee kutupiga, kimsingi hakuna haja ya kuangalia TV kama una modem yako au simu yenye internat.
 
Acha bana, wazee waliopo kwenye system wanaomba wapunguze umri ili waendelee kutupiga, kimsingi hakuna haja ya kuangalia TV kama una modem yako au simu yenye internat.

tupe maujanja. mi naona jamiiforums ndo tv, radio na gazeti rangu. mia
 
hawajajipanga kabisa inabid tcra wajaribu kulifuatilaa tena kwa umakini zaid bila hvyo tv ni mateso tupu mara no service mara no signal wakati tumelipia 18000
 
Hiki cha kukodi ndio balaa, eti nilipie miezi kumi, kwa sisi tunaojua hesabu 6000 mara miezi kumi ni 60000, kwa kuangalia kitu gani kwenye TV za kibongo, sioni sababu ya kuendelea na utaratibu huu,
 
Back
Top Bottom