Hivi kamati kuu ya CHADEMA ipo au haipo?

Hivi kamati kuu ya CHADEMA ipo au haipo?

wakimataifa.

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2015
Posts
1,625
Reaction score
558
Tukiwa wanachama watiifu wa CHADEMA tunauliza kamati kuu ya CHADEMA ipo au haipo naona kimya hawajadili baada ya uchaguzi ni cha kufanya kama chama.

Tunasikia tu kila mmoja ni kutamka matamko ya Magufuli anatekeleza ilani ya CHADEMA.

Hata msemaji wa chama hatumfahamu.
 
Umeuliza na kujieleza kitoto sana Mkuu. Kama CHADEMA ina mwanachama kilaza kama wewe, kuna shida kubwa kwenye hicho chama. Bure kabisa
 
Ungekuwa Mwana Chadema ungejua kwamba baada ya uchaguzi Mkuu iliitishwa Kamati Kuu kujadili matokeo yaliyokuwa yanatangazwa.

Halafu kila siku Makene amekuwa akitoa taarifa mbalimbali kuanzia matokeo,kifo cha Alfonce Mawazo na Kaimu Katibu Mkuu mara nyingi anatoa taarifa wewe huwa unajifungia wapi mpaka usimjue msemaji wa Chama?
 
Umeuliza na kujieleza kitoto sana Mkuu. Kama CHADEMA ina mwanachama kilaza kama wewe, kuna shida kubwa kwenye hicho chama. Bure kabisa

Mkuu achana na huyo si mwana Chadema bali ni wa chama kile ambacho sifa kubwa ya kuwa mwanachama ni kujitoa ufahamu.
 
Mkuu achana na huyo si mwana Chadema bali ni wa chama kile ambacho sifa kubwa ya kuwa mwanachama ni kujitoa ufahamu.

chadema ukihoji unaonekana si mwanachama hilo ndio tatizo tunakipenda chama lakini hakitupendi
 
CHADEMA wapo likizo ya mwaka, Moshi wakiwa huko tamko juu ya uelekeo wa chama kwa mwaka 2016 litatolewa ikiwemo mikakati ya kurudia tena hoja ya KUPIGA VITA UFISADI AMBAYO ILIFIFIA KIPINDI CHA KAMPENI 2015
 
CHADEMA wapo likizo ya mwaka, Moshi wakiwa huko tamko juu ya uelekeo wa chama kwa mwaka 2016 litatolewa ikiwemo mikakati ya kurudia tena hoja ya KUPIGA VITA UFISADI AMBAYO ILIFIFIA KIPINDI CHA KAMPENI 2015

Mbona kashifa ya JPM kuuuza nyumba za serikali na ripoti ya PPRA ilisemwa sana majukwaani na Mameneja kampeni wewe ni Msomali?
 
Mbona kashifa ya JPM kuuuza nyumba za serikali na ripoti ya PPRA ilisemwa sana majukwaani na Mameneja kampeni wewe ni Msomali?

ww ile sio kashfa, kashfa waliouziwa watumishi wa serikali na hela iliingizwa serikalini.
fikiri kabla ya kusema akina mbowe wakipiga filimbi ww unacheza na hujui wimbo wenyewe
 
Sema chadema nayo imekuwa kimya sana. Nini kinaendelea, salum mwalimu anaonekana kupwaya kwenye nafasi yake
 
ww ile sio kashfa, kashfa waliouziwa watumishi wa serikali na hela iliingizwa serikalini.
fikiri kabla ya kusema akina mbowe wakipiga filimbi ww unacheza na hujui wimbo wenyewe

Msikilize CAG alisema nini? Alisema "Hakuna ufisadi mbaya kama ule wa kuuza nyumba za serikali"
Ishu si kuingiza hela serikalini. Vipi mdogo wake aliyeuziwa nyumba wakati si mtumishi wa serikali. Vipi leo serikali inaingia gharama kubwa kuwapangishia Nyumba Mawaziri na maofisa wengine wa serikali kama mahakimu,majaji kwa gharama kubwa wakati nyumba zilikuwepo. Mfano huku Mwanza kuna akimu anakaa kwenye nyumba pango la mwezi ni milioni 1.5 wakati nyumba hiyo hiyo ya serikali iliuzwa kwa Tsh. milioni 10
 
Back
Top Bottom