Hili la kufukuza walimu wakuu wakifelisha, napingana nalo 100%

Mlalamikaji daily

JF-Expert Member
May 19, 2014
736
1,613
Mheshimiwa Rais nikupongeze kwa kasi yako unayoendelea nayo.Naandika hili nikiwa na uhakika kuwa utalipata.

Ni kweli wakuu wa shule wamepewa jukumu la kuongoza shule na wanatakiwa kuwajibika kwa nafasi zao kama wakuu.

Mheshimiwa Rais, kauli yako kuwa shule ikiwa na division zero(0)
nyingi basi walimu wakuu wawajibike, napingana nayo kwa sababu zifuatazo:

1.Walimu wakuu sio wasababishi wa watoto kufeli.Hebu fikiri mheshimiwa raisi shule ina walimu watatu,haina vitabu,haina madawati,je hao watoto watafaulu vipi?

2.Hali ya walimu.

Je walimu wametengenezewa mazingira gani ya kusababisha wafundishe kwa ufanisi? Mishahara midogo,watu wana madai,hakuna nyumba n.k Je wanafunzi watafaulu vipi?

Katika matokeo ya kidato cha nne tumejionea shule 50 bora zote ni za binafsi.Ina maana tatizo lililosababisha shule za serikali kufanya vibaya ni wakuu wa shule?

3. Mheshimiwa suala hilo pia litasababisha udanganyifu katika mitihani maana wakuu wa shule watafanya mbinu zao wanazojua ili wafaulishe wakuridhishe wewe ilihali katika uhalisia wanafuzi hawakufaulu.

Asante kwa kusoma waraka wangu.

Mwananchi.
 
Kuna wale goldenboy wao hulipwa 36 Milion kama mara 90 hvi ya kima cha chini cha mwalimu kwam wezi hawa hutokea nhc, tra, ewura, sumatra, tanesco and alike.
Kuna wale silverboy hawa hulipwa hadi 20mill kama mara 40 hivi ya kima cha chini cha mwalimu kwa mwezi hawa hutokea psisib, mawaziri na alike
Kuna wale ironboy hawa ndo wale wanaolipwa mpaka 10 mill.kwa mwezi hawa hutokea ubunge ujaji hvi and alike.
Halafu kuna wale wa nni hawa hulipwa chini ya million kwa mwezi.
Tuwe wakwel hvi unatarajia kuvuna nn mahali usipopanda?
Kama kwel mnaona elimu ina umuhimu oneni kwa vitendo. Inawezekana vipi mtu unaemtegemea akuzalishie watu useful umdharau mpaka mwisho na kmpeza juu leo utegemee akuletee matokeo chanya?
Tumedharau mchinja mpya likely wazimu utaturudia.
Ni vizuri kufanya tadhimini kuntu kuliko kuliko kubaki na porojo za watu wasiojielewa!!
 
kwa maana nyingine badala ya kuwatishia walimu serikali ingetatua kero zao kwanza ikianzia kwenye mishahara kwanza hivi huyu aliyepanga walimu walipwe mishahara hii wanayolipwa Leo...alifikiria nini kwanza
 
Mheshimiwa Rais nikupongeze kwa kasi yako unayoendelea nayo.Naandika hili nikiwa na uhakika kuwa utalipata.

Ni kweli wakuu wa shule wamepewa jukumu la kuongoza shule na wanatakiwa kuwajibika kwa nafasi zao kama wakuu.

Mheshimiwa Rais, kauli yako kuwa shule ikiwa na division zero(0)
nyingi basi walimu wakuu wawajibike, napingana nayo kwa sababu zifuatazo:

1.Walimu wakuu sio wasababishi wa watoto kufeli.Hebu fikiri mheshimiwa raisi shule ina walimu watatu,haina vitabu,haina madawati,je hao watoto watafaulu vipi?

2.Hali ya walimu.

Je walimu wametengenezewa mazingira gani ya kusababisha wafundishe kwa ufanisi? Mishahara midogo,watu wana madai,hakuna nyumba n.k Je wanafunzi watafaulu vipi?

Katika matokeo ya kidato cha nne tumejionea shule 50 bora zote ni za binafsi.Ina maana tatizo lililosababisha shule za serikali kufanya vibaya ni wakuu wa shule?

3. Mheshimiwa suala hilo pia litasababisha udanganyifu katika mitihani maana wakuu wa shule watafanya mbinu zao wanazojua ili wafaulishe wakuridhishe wewe ilihali katika uhalisia wanafuzi hawakufaulu.

Asante kwa kusoma waraka wangu.

Mwananchi.
Hapa kazi tu. Huu ni muda wa kutumbua majipu hata ambayo hayajaiva ili tuonekane tunafanya kazi
 
Back
Top Bottom