four eyes
JF-Expert Member
- Jan 11, 2017
- 905
- 1,408
Katika zama hizi zisizoeleweka ueledi na umahiri vimekuwa vitu adimu sana vilivyo hatarini kutoweka,utangazaji na uandishi Habari WA zama hizi mpya umekuwa WA kikanjanja kwa kiwango cha kusikitisha.
Kumbukumbu za watangazaji kama Charles Hilary,Ahmed jongo,nyaisanga,debora mwenda na vichwa vingine vya Aina hiyo vinakufanya wakati mwingine uhisi hakuna umahiri Tena zaidi ya umarekani mwingi na kuigana kwa watangazaj WA siku hizi
Hata hivyo hakijapotea kila kitu,bado wapo mafundi kama huyu hemed kivuyo ambae kila nikimsikiliza akiripoti binafsi naburudika sana.
Ni mtangazaji mbunifu,mwenye misemo na visa anavyovitumia kusindikiza ripoti zake akichanganya na sauti yenye mbwembwe za Aina yake.
Nimpe tu heko na kuwasihi vijana wapya katika fani hii waangalie nn cha kujifunza kwa watangazaji kama huyu ili kuwa na taaluma inayoacha alama.
Kumbukumbu za watangazaji kama Charles Hilary,Ahmed jongo,nyaisanga,debora mwenda na vichwa vingine vya Aina hiyo vinakufanya wakati mwingine uhisi hakuna umahiri Tena zaidi ya umarekani mwingi na kuigana kwa watangazaj WA siku hizi
Hata hivyo hakijapotea kila kitu,bado wapo mafundi kama huyu hemed kivuyo ambae kila nikimsikiliza akiripoti binafsi naburudika sana.
Ni mtangazaji mbunifu,mwenye misemo na visa anavyovitumia kusindikiza ripoti zake akichanganya na sauti yenye mbwembwe za Aina yake.
Nimpe tu heko na kuwasihi vijana wapya katika fani hii waangalie nn cha kujifunza kwa watangazaji kama huyu ili kuwa na taaluma inayoacha alama.