Si huyu anayebeba MKEWE KWENYE safari zake na pia kuhutubia ili kupata PerDeM as well... Sijawahi kuona hivyo ni Rais KIKWETE huwa anamtumia Mama Salma kuhutubia wananchi wakati wa SHEREHE za CCM KIGOMA
Sasa Kama Uchapakazi ni kutumia MKEWE pia MORE POWER 2 HIM; Enzi za JK NYERERE wake Walikuwa na HESHIMA sio kuburutwa kuchota PESA za KODI za wananchi na NCHI ni MASIKINI
*** SOMA CHINI***
2/13/13 Mke wa Waziri Mwanri afichua siri ya mumewe
www.habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/8220-mke-wa-waziri-mwanri-afichua-siri-ya-mumewe?tmpl=component&print=1&layout=default&page= 1/1
MKE WA WAZIRI MWANRI AFICHUA SIRI YA MUMEWE
KUFUATIA Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Aggrey Mwanri kuwa mkali na kukagua ujenzi wa miradi ya kijamii mkoani Rukwa kwa umakini mkubwa na kubaini mapungufu mengi mkewe Agnes Mwanri amefunguka na kusema ndivyo alivyo hata akiwa nyumbani kwao.
Mama Mwanri anafuatana na mumewe katika ziara ya kikazi ya siku sita mkoani hapa.
Alisema: Msimshangae mkadhani anajipendekeza hapana yeye (Mwanri) ndiyo alivyo hata akiwa nyumbani anafanya vitu vyake kwa umakini wa hali ya juu na hapendi kudanganywa wala kuona watu wakidhulumiwa haki zao.
Mume wangu ndivyo alivyo hata akiwa nyumbani kwanza hapendi uonevu wala udanganyifu wa aina yoyote ile yeye siku zote anasimama katika haki.
Hivyo nimeamua kuwaeleza haya kwa sababu kutokana na kuwa makini katika kazi zake hususani anapokagua ujenzi wa miradi, isieleweke kuwa anajipendekeza la hasha yeye ndivyo alivyo, alisema.
Mwanri amekuwa kivutio kikubwa na kumwagiwa sifa kemkem na wananchi katika maeneo mbalimbali alipotembelea na kukagua ujenzi wa miradi ya kijamii wakidai kwamba hawajawahi kushuhudia kiongozi yeyote wa ngazi za juu akikagua ujenzi wa miradi hiyo kwa umakini wa hali ya Juu.