Mali/kitu chochote chenye thamani kubwa ambacho kimeporwa na majambazi ili kukitoa mikononi mwa hayo majambazi ni lazima kuyaonyesha majambazi hayo kuwa mali/kitu hicho wanachokishikilia hakitakuwa na thamani kwao kwa kuendelea kukishikilia kwa nguvu; badala yake ndiyo itakayokuwa njia yao ya kuangukia pua haraka sana.
WaTanzania ni muhimu sasa waelewe thamani kubwa aliyonayo Tundu Lissu kwa taifa hili.
Tundu Lissu akitaka kuondoka gerezani kwake ni rahisi sana wakati huu.
Atakubali tu kuwa hatashiriki tena kuwasumbua hao majambazi; au hata kwamba atashiriki kuwashawishi waTanzania wakubali kutawaliwa tu na majambazi.
Akitaka kufanya hivyo, leo hii hii anatoka gerezani
Yupo gerezani kwa sababu hataki kuwaweka waTanzania wenzake katika gereza la kudumu chini ya waovu hawa..