Hawa STARTIMES wanapata wapi jeuri ya kukaidi agizo la Serikali?

Hawa STARTIMES wanapata wapi jeuri ya kukaidi agizo la Serikali?

Mu7

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2013
Posts
1,635
Reaction score
1,951
Serikali iliagiza channels zote za ndani kuoneshwa bure kwenye ving'amuzi lakini cha ajabu Startimes wamenikatia channels zote wananiachia St. Guide na Safari Channel tu. Ikoje hii??
 
Unatumia startimes gani ya Antenna hizo channels za local ni bure
 
labda kwako ndo wamekata, mimi nina startimes na local channels ni bure usiwasingizie

na saiv niko naangalia ITV hapa na sijalipia
 
kweli nimeamini hali ya uchumi ni tete sana kwa mtu mmoja mmoja!

yaani wachangiaji woote waliochangia kwenye hili bandiko hakuna hata mmoja alielipia king'amuzi

yaani kila mtu anaangalia chanel za bule, kweli tutajenga taifa hili?

ebu lipieni jaman acheni ubahili
 
Back
Top Bottom