Hatimaye wananchi wafunguka

Hatimaye wananchi wafunguka

Robethn

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2015
Posts
2,103
Reaction score
354
WANAICHI WAKATAA KUBURUZWA.

Kwa namna isiyoitarajiwa leo tujikumbushe ule mstari wa biblia unaosema “Enyi Wagalatia ni nani aliyewaroga? Wanainchi tulio wengi tunawafananisha Wagalatia na UKAWA kwa kweli. Maana Wagalatia walihasi imani yao kwa kutenda na kuyageukia yale ambayo walikuwa wanayakemea mwanzoni na kuyafanya kuwa ndio mtindo wa maisha yao. Hii haina tofauti sana na kilichotokea UKAWA kwani walilaani sana kuhusu ufisadi na walikuwa wanasubiria kwa hamu kuwa CCM wamteue mzee Lowassa tu ambaye viongozi wote wa UKAWA walimshutumu na kumtangaza kuwa mzee ni fisadi LAKINI BADO kawa mgombea wao nafasi ya uraisi.

Lakini leo hii bila aibu wanamnadii tena hadharani na kumtetea haswaaaa kwa kila kitu anachokifanya. Mmmhhh kweli UKAWA mmehasi imani yenu ya kuwachukia mafisadi na hakika tunashindwa kuelewa ni nani aliyewaroga kiasi hicho. Inakuwaje uchafu wa mtu ukasafishika kirahisi hvyo; au ule ubaya wake mliokuwa mnausema ukageuka kuwa wema ghafla?

Nadhani Tanzania inahitaji viongozi wenye msimamo pia kuongozwa na vyama vyenye misimamo. Zaidi ya yote inahitaji viongozi na chama ambacho kitaweza kuchukua maamuzi magumu kwa maslahi ya wananchi. Wengi walidhani kuwa Mh.Kikwete atamteue babu kwa sababu ya urafiki wao; lakini tunampongeza Mh.Kikwete kwa kutambua kuwa maslahi ya nchi ni ya muhimu zaidi kuliko mahusiano ya kirafiki. Eti leo kwenye mitandao ya kijamii bila hata haya mnapost picha yenye maneno eti shujaa amezaliwa leo……leo mnamuita shujaa wakati siku za nyuma mlimtangaza kama fisadi aliyekubuhu. Hakika mnahitaji kujichunguza ni wapi mlipokosea ili mpate kuirudia imani yenu.

Watanzania tunapaswa kuwa makini sana na wanasiasa wa namna hii,wasiojitambua na kuthamini maendeleo yetu, tusikubali kuburuzwa kwa manufaa ya kikundi kidogo:
October 25 tuudhihirishie ulimwengu kuwa tupo makini katika kipigania utaifa wetu na si vinginevyo.
 
Tunataka mabadiliko Lowasa anaweza,hata Maghufuli alisema watanzania wanataka mabadiliko
 
Acha kuboa wewe kibaraka wa ccm,nenda kapost kwenye twitter ya ccm na katoe habari katika gazeti la uhuru
 
Magufuli na hadithi ya Bwana Sanja."Msiiue CCM"
 
ebu nisaidie mleta mada hwaa wanywa viroba kawazalisha nani?kodi ya viroba anankusanywa na tra ama?je anaekunywa na anasubiri kodi ya viroo ikusanywe na tra nan mlevi?
 
Ukiona mtu anamkashifu mkeo ukifanya kosa la kumwacha usishangae kesho kukuta kamuoa!
 
Nakushukuru kwa kuwa unajua na biblia. Paulo hapo awali aliitwa sauli cjui km unafahamu habari hii! Alikuwa mtaabishaji mkubwa wa kanisa lkn baada ya kukutana na Kristo akawa ndo mkombozi wa kanisa. Lkn kwa waliomjua km Sauli haikuwa rahisi kumuamini walisema maneno km yako! Piga magoti mwombe Mungu akuoneshe kiongozi bora usihangaike sn na UKAWA!
 
Nakushukuru kwa kuwa unajua na biblia. Paulo hapo awali aliitwa sauli cjui km unafahamu habari hii! Alikuwa mtaabishaji mkubwa wa kanisa lkn baada ya kukutana na Kristo akawa ndo mkombozi wa kanisa. Lkn kwa waliomjua km Sauli haikuwa rahisi kumuamini walisema maneno km yako! Piga magoti mwombe Mungu akuoneshe kiongozi bora usihangaike sn na UKAWA!


MKuu, mkumbushe na ile habari ya SAFINA YA NUHU, nani waliingia humo na nini kiliwakuta wakaidi. Hayo tu.
 
Jamani tumechoshwa Na maisha haya magumu wao wanagawana mahela ya escrow Na familia zao sisi wanatupa T'Shirt Na vilemba
 
Maji yamefika shingoni.
Mwanakwale wa maji ahishi kutapatapa.

Magamba wameshikwa pabaya.
 
Back
Top Bottom