Hatimaye mabadiliko kuikumba manispaa ya Temeke

Hatimaye mabadiliko kuikumba manispaa ya Temeke

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
137,364
Reaction score
271,791
Iko wazi sasa kwamba ule utawala wa milele wa ccm kwenye baraza la madiwani ndani ya manispaa hii umefika tamati , kwa mfano ccm ina dalili zote za kushindwa kwenye kata ya chang'ombe ambapo mgombea wa UKAWA Benjamini Ndalichako anang'ara mno mbele ya Noel Kipangule wa CCM ambaye wananchi wamemchoka yeye na chama chake , kwenye kata ya keko ndugu Mohamed Fundi wa UKAWA amemwacha mbali mno Mtawa wa CCM.Ikumbukwe kwamba kwenye kata hii CCM ilipata kiti kimoja tu kati ya vitano kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
 
Wakazi wa kurasini ni mashahidi kwamba hakuna tena nafasi kwa wilfred kimati kurudi maana amekabwa koo na Ndugu Matiti Togocho wa UKAWA ambaye pia ni mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa kurasini mivinjeni , kwenye kata hii pia ccm iliangukia pua kwa kuambulia kijiji kimoja kati ya vitano , kata ya miburani mchuano ni mkali kati ya mgombea wa UKAWA tajiri anayemiliki ghorofa pekee keko machungwa ernest moshi dhidi ya jirani yake ambaye ni diwani anayemaliza muda wake ndugu Juma mkenga ambaye amepoteza uaminifu kwa wananchi baada ya kutelekeza maendeleo keko machungwa alipozaliwa na kukulia , kazi ni ngumu mno !
 
Kazi zisizo na tija za mabinti huko uarabuni na ile kashfa ya kudanganya umri kwa miss Tanzania ni kama zimemwondoa kwenye mbio za ubunge ndugu mtevu , hivyo kuacha nafasi ya wazi kwa mgombea wa UKAWA .
 
Iko wazi sasa kwamba ule utawala wa milele wa ccm kwenye baraza la madiwani ndani ya manispaa hii umefika tamati , kwa mfano ccm ina dalili zote za kushindwa kwenye kata ya chang'ombe ambapo mgombea wa UKAWA Benjamini Ndalichako anang'ara mno mbele ya Noel Kipangule wa CCM ambaye wananchi wamemchoka yeye na chama chake , kwenye kata ya keko ndugu Mohamed Fundi wa UKAWA amemwacha mbali mno Mtawa wa CCM.Ikumbukwe kwamba kwenye kata hii CCM ilipata kiti kimoja tu kati ya vitano kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
Nilitoka Posta wiki iliyopita nikakatiza Keko Mwanga nikaona pia rangi ya namna hivyo. Hebu nijuze
 
Back
Top Bottom