Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
Nchini India watu wengi wameathilika na program ambazo zinatoa mikopo ya pesa kwa kuweza kudhalilishwa kutokana na mikopo waliokopa.
Takribani zaidi ya wahindi 60 wamejiua baada ya kunyanyaswa na kutishiwa kwa namna moja au nyingine baada ya kuomba mikopo. Ni app ambazo zinapatikana Kwenye soko la play store inatoa mikopo kwa watu kwa namna moja au nyingine.
Ukifanikiwa kupata mkopo unapewa hapo hapo mkopo yani hakuna kusubiria siku mbili au moja ila shida yake inaanza unasumbuliwa Kwenye kurudisha maana mkopo wao ni zaidi ya "kausha Damu😃!".
Kwani ukifanikiwa kuinstall app Kwenye simu Yako basi inachukua picha zako kwa namna tofauti tofauti na kuanza kuzisambaza mtandaoni wakati mwingine wanakuweka mpaka kwenye kurasa za ngono nk.
Picha zako zinasambazwa mitandaoni jambo linalopelekea wahindi wengi kupatwa na msongo wa mawazo na kufikia hatua ya kujiua kwani unaweza pigiwa simu kwa siku zaidi ya 100 kutaka urudishe pesa.
Wakati mwingine wanawapigia ndugu, jamaa na marafiki zako na kuwasumbua, watu wengi walioathilikq ni wahindi, waafrika , watu wa Asia nk.
Mjihadhari na program za mikopo kwani Zingine zinachukua taarifa zako na kuzisambaza mtandaoni