BekaNurdin
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 2,267
- 2,041
Hata nipigwe bani, Kamwe sitetereki
Ninapopigwa bani, Hata kama si haki
Nitabaki kundini, Jeefu sitoroki
Siku tano kambani, Katu haz'zoeleki
Nimetengwa kundini, Na mods kindaki
Kwani uzito gani, Ya kwangu misiteki?
Wanagawiwa bani, Kana kwamba ni keki
Wawekwa gerezani, Na mamodi kindaki
Watiwa hatiani, Kosa bila hakiki
Mwapata sifa gani, Wengine piga loki?
Mwasutwa nafsini, Bila kutenda haki
Ukali legezeni, Jamvi liwe rafiki
Walio kifungoni, Furaha hailiki
Pia mahakamani, Mello we hukumbuki?
Na wengine kwa nini, Mwawatia maloki?
Mkizidisha bani, Mtazidisha chuki
Siredi za udini, Zinachochea chuki
Mwazipotezeani, Mbona hazifungiki?
Matusi ya nguoni, Na siasa za chuki
Zinaletwa jamvini, Na hazipigwi loki
Mkitaka amani, Mzingatie haki
Mods jipimeni, Kama mwatenda haki
Je anifea bani, Yawapandisha kiki?
Bure nisameheni, sienezagi chuki
Nimetoka kifungoni, Kwa madaha lukuki
N'taheshimu kanuni, Nitahubiri haki
Kuna ugumu gani, Kuzingatia haki?
Ninapopigwa bani, Hata kama si haki
Nitabaki kundini, Jeefu sitoroki
Siku tano kambani, Katu haz'zoeleki
Nimetengwa kundini, Na mods kindaki
Kwani uzito gani, Ya kwangu misiteki?
Wanagawiwa bani, Kana kwamba ni keki
Wawekwa gerezani, Na mamodi kindaki
Watiwa hatiani, Kosa bila hakiki
Mwapata sifa gani, Wengine piga loki?
Mwasutwa nafsini, Bila kutenda haki
Ukali legezeni, Jamvi liwe rafiki
Walio kifungoni, Furaha hailiki
Pia mahakamani, Mello we hukumbuki?
Na wengine kwa nini, Mwawatia maloki?
Mkizidisha bani, Mtazidisha chuki
Siredi za udini, Zinachochea chuki
Mwazipotezeani, Mbona hazifungiki?
Matusi ya nguoni, Na siasa za chuki
Zinaletwa jamvini, Na hazipigwi loki
Mkitaka amani, Mzingatie haki
Mods jipimeni, Kama mwatenda haki
Je anifea bani, Yawapandisha kiki?
Bure nisameheni, sienezagi chuki
Nimetoka kifungoni, Kwa madaha lukuki
N'taheshimu kanuni, Nitahubiri haki
Kuna ugumu gani, Kuzingatia haki?