Hata angekuwepo,CHADEMA ingeshindwa pale Kalenga!

Hata angekuwepo,CHADEMA ingeshindwa pale Kalenga!

kensh

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2012
Posts
527
Reaction score
113
Hatimaye ile tamthilia yenye mbwembwe,vituko,uhuni na kila aina ya kihoja imeisha pale kalenga.Jumapili ya 16/3/2014 imehitimisha tamthilia hiyo,imetuacha na ama majibu machache kuliuko maswali,ama haijatupatia jibu lolote kwa maswali yetu.

Najiuliza,nani kaibuka mshindi? Na nani kapoteza? Kwanini?

Wapo ambao wakisoma swali la mwanzo,haraka wangebeza na kuona mleta hoja hajitambui au hajui lolote na ni mpiga kelele wa kawaida tu,na wangemtaja haraka alieshinda kuwa ni Mgimwa,yule mtoto wa marehemu William Mgimwa.
Na,wpo wale ambao wangesema mshindi ni Grace,yule mgombea wa Chadema,sababu wanazo.

Siwafahamu sana waliokuwa wakigombea,ila nawezasema jambo kuhusu nilivowafahamu kipindi kile cha kampeni,nilimuona Mgimwa,nilimsikiliza na kupima uwezo wake wa kujieleza na kupambanua mambo.Nilimsikiliza Grace pia,nilimfuatilia alivyojenga hoja,alivyofafanua mambo na kuwasilisha mbele ya jamii.Nilishawishika sana na namna Grace alivyojieleza,alionesha uwezo na uthibitisho wa alichokisema,alijenga hoja na kutoa ufafanuzi mbalimbali wa jambo ili wananchi welewe alichojaribu kuwaeleza,alithibitisha uwezo binafsi.Tofauti na Mgimwa,ambaye alionekana kukariri tu yale aliyoyasema,hakuwa na uwezo zaidi wa kuongezea hoja na kuzipambanua zaidi ya vile alivyokaririshwa,alisema kwa vituo vingi,akiashiria kujaribu kukumbuka sana yale aliyokaririshwa.

Hata iweje,Mgimwa ndie mbunge wa Kalenga kwa tiketi ya CCM,hayo ndiyo maajabu yaliyotokea Kalenga!

Kwanini Grace alipoteza?

Wapo walionichekesha walipokuwa wakijibu swali la namna hii,waliziziba akili zao zisitafakari wala kuona mambo kihalisi.Walimkimbilia mtu wao,walimtaja na kujenga hoja kuwa bila huyo Chadema haiwezi,si lolote wala chochote,wakapaaza sauti,wakamtaja kwa majina yake mtu huyo kuwa ni Zitto Zuberi Kabwe.Wakasema mzimu wa huyo,unaitesa Chadema.Nikajiuliza 'ANA MZIMU?'

Nikajikumbusha machache ya juu juu tu,kuwa je,kule Arumeru alishiriki huyo mwenye mzimu? Je,kule jimboni kwake,kuna madiwani wangapi wa Chadema waliopatikana kwa mwaka 2010 wakati wa uchaguzi mkuu? Na kigoma kwa ujumla ina madiwani wangapi wa Chadema waliopatikana 20101? Kata zilizonyakuliwa na CCM au NCCR kule Kigoma wakati wa uchaguzi mkuu,nani alikuwa na Mzimu kipindi hicho? Wanaojenga hoja kuwa kushindwa kwa Chadema kule Kalenga ni matokeo ya kutimuliwa kwa ZZK,ni watu hoi kifikra au wana mahaba ya kupindukia kwa ZZK kiasi kwamba kila jambo linaloenda kombo kule Chadema,wao husema sababu ni kutokuwepo kwa ZZK,hawajui kuwa ZZK ameikuta Chadema ikiwa na mafanikio yake na hata matatizo yake pia,na hakukua na mwenye mzimu! Kuna uwezekano kuwa wanaomtukuza ZZK wanafanya kusudi kumpotosha au wanatafuta fursa moyoni mwa ZZK,bila shaka wataipata huko ATC.

Nani adui wa Chadema Kalenga?

Bilashaka swali hili limejibiwa,tena labda kabla sijajiuliza.Wengi wamesema,mimi narudia au kuongezea tu.Adui wa chadema ni DAFTARI LA WAPIGA KURA na si mzimu wa ZZK! Kwanza hana Mzimu,na kama anao,basi anautumia kwa mengine, yake binafsi.

Daftari la wapiga kura ni kikwazo kikubwa kwa upinzani nchi hii.Ukitizama sana muamko wa siasa katika nchi hii,utaona jinsi vijana walivyo na hamasa ya kushiriki katika uchaguzi,wanataka kuleta mabadiliko HARAKA! Tatizo ni hilo DAFTARI. Daftari halijafanyiwa marekebisho yoyote ya maana,nakumbuka mimi nimeandikwa katika daftari 2004,kule kwetu Mbozi.Leo ninaishi Mwanza,je,nitashiriki vipi uchaguzi hapa Mwanza? Nirudi nyumbani pindi za uchaguzi ili tu nikapige kura? Nauli? Pia,je tangu 2004,ni vijana wangapi leo hii 2014 ambao wana sifa zote za kuwemo katika daftari na hawamo na wanashiriki sana katika kuhamasisha wakati wa kampeni za chaguzi mbalimbali? Wengi wa wapiga kura ni vijana na hawamo katika daftari la wapiga kura,na hao ndio hasa wanaotaka mabadiliko,ndio wanaotaka vyama mbadala,ndio wanaotaka chadema,cuf au nccr.

Endapo daftari la wapiga kura likiboreshwa leo,hakika nitavitia moyo vyama vyoote vya upinzani vishiriki katika chaguzi mbalimbali.Vinginevyo,vyama hivyo vya upinzani vitazidi kulialia tu kuwa vimechezewa rafu hii au ile bila kupata ufumbuzi.Vitalilia jeshi la polisi,vitalaumu green guard,vitalaumu kauli ya mwenyekiti wetu ile ya kuacha unyonge na wala havitapata ufumbuzi.

Vyama vya upinzani na wapenda demokrasia,waje pamoja,washirikiane na watanzania wengine,kwa pamoja tudai marekebisho ya DAFTARI LA WAPIGA KURA lifanyiwe marekebisho yoote muhimu ikiwa ni pamoja na kuandikwa kwa wengine woote wenye sifa za kuwemo katika daftari. IT CAN BE DONE! Vinginevyo,tutaendelea kutegemea mizimu ya akina Lisu,Mbatia,Mtikila na wakati mwingine hata mzimu wangu.

Chalinze hapatakuwa na jipya zaidi ya muendelezo wa kile kilichotokea Kalenga,ila daftari likiboreshwa kesho kabla ya uchaguzi,hakika Chalinze itashangaza wengi,itaenda upinzani.
 
Haihitaji mtu akili ya darasa la saba kutambua uwezo wako mdogo! By only single variable ume jump into conclusion! Ptuuuuu! Akili za BAVICHA hizo
 
bila zito chadema inayumba.. huyu mama grace angegombea kupitia chama chake cha jahazi asilia angeshinda, chadema imemuingiza chaka
 
Kama unajua Mtapewa cha mbavu CHALINZE Mwambie Mbowe asisimamishe mgombea kule.

ZITTO HATA HAUSIKI NA KICHAPO CHENU KULE.

HAPO MNAPOTEZA WOTE,CDM INAPOTEA NA ZITTO ANAPOTEA

MNGESHINDA KALENGA MMEMTUKANA SANA HUMU!

NA BADO,MTAENDELEA KUPEWA KCHAPO
 
Hilo Daftari la wapiga kura linaandikisha wanachama wa CDM peke yake? Wengi ambao hujiandikisha na kupiga kura ni wale wasiokuwa na vyama!
 
Kulegalega kwa Chadema ni kwa sababu ya viongozi wake kung'ang'ania kuwepo madarakani kwa nguvu bila kuitisha uchaguzi ulio huru, na pia viongozi hao kuziba masikio kwenye vilio vya sehemu ya wanachadema wanaohitaji uwajibikaji wa wazi na haki, kupunguza udikteta, kuondoa double standards na kushikisha makundi yote ya Tz katika chama. Hilo ndo linapigiwa kelele kwa sana, wala siyo hilo la ZZK unalolisema wewe.

Kuboresha daftari la wapiga kura ni sawa, lakini haitasaidia kitu kama CDM na uongozi wake hautajirekebisha, au kama hazitafanyika juhudi za kushawishi makundi kama ya kina mama, wazee (ambao mnawasema hawana mwamko hivyo wao kujiona kama wanatengwa na CDM), Waislam na makabila yote ya Tanzania.
 
Mtu yeyote mwenye uelewa atatambua Chadema haikuwa na uhakika wa kushinda Kalenga! Jimbo la Kalenga kama yalivyo mengi mkoa wa Iringa bado ni stronghold za CCM. Naipongeza Chadema kwa kuwa Ilikwenda kutimiza wajibu wa kuendeleza kuinua mwamko miongoni mwa wananchi wa kupigania mabadiliko. Na kwa hili imefanikiwa kiasi kikubwa sana!
Mawazo mengine kama hayo ya KENSH hayana mashiko......BIG UP CDM!
 
Ulichosema ndo ukweli mwenyewe, huyo kibaraka hakuwahi kushirika uchaguzi mdogo popote tofauti na zile kata tatu wakati wenzake wako Arumeru. Alikimbia kule baada ya kuogopa siri kuvuja Lema angemtoa meno, tukirudi kwenye point ni kuwa baada ya uchaguzi wa Kalenga pressure yetu ya kudai daftari la kudumu itaanza upya! Tatizo kuna mkanganyiko, tutaumia viparata au vitambulisho vya taifa uchaguzi ujao?

Lakini kwenye mikutano yetu yote inayoendelea vijijini tunanawaeleza watu hasa vijana umuhimu wa kujiandikisha. Vijana wako tayari kwa mabadiriko na kama Ccm wanadanganywa na uchaguzi mdogo wasubiri kipigo cha mwakani vijana watakapokuwa wamejiandikisha.
 
Hivi ni kwa nini cdm wanvuajihakikishia kuwa watu wote ambao hawajaandikishwa ndo wapiga kura wao? Wana uhakika Gani? Hivi wangekuwa makin Si wangejipanga na kuchukua kura za hats hao waliokwishaandikishwa tayari!kubalini kushindwa bhana
 
mwambien slaa akagombeee chalinze muone hiyo aibu kama kweli chadema ni chama/?:nod:
 
Back
Top Bottom