Mwananchi360
Member
- Jan 26, 2016
- 42
- 35
Hakuna taifa lililowahi kufikia maendeleo ya kweli kwa kuwa na viongozi chawa. Taifa lolote linalotegemea kujipendekeza badala ya utendaji linajenga utawala dhaifu, usio na uwajibikaji na hatimaye linadidimia katika dibwi la ufisadi na uzembe wa kiuongozi.
Katika mfumo huu mamlaka inahamia kwa mtu mmoja (Rais). Yeye ndiye anayepaswa kutoa kauli juu ya kila jambo, kusuluhisha kila tatizo na kusimamia kila sekta, wakati wale waliokabidhiwa dhamana ya kuongoza wanakaa pembeni wakisubiri amri. Matokeo yake sifa na lawama zote zinamwelekea Rais huku viongozi wa ngazi nyingine wakibaki wasindikizaji wa maamuzi.
Uchawa si tu unadumaza fikra za uongozi, bali pia ni adui wa maendeleo ya taifa. Ili tufikie maendeleo ya kweli tabaka hili la kujikomba lazima litokomezwe.
Taifa lenye viongozi waoga na wasio na uthubutu wa kusema ukweli au kufanya maamuzi yenye tija haliwezi kupiga hatua za kimaendeleo. Hatuhitaji viongozi wa "ndiyo mzee", “mama anaupiga mwingi” tunahitaji viongozi wenye uwezo wa kufikiri, kutoa suluhisho na kusimamia maendeleo ya wananchi kwa haki na uwajibikaji.
Ni wakati wa kusema hapana UCHAWA. Taifa linahitaji viongozi NA si wasindikizaji.
Katika mfumo huu mamlaka inahamia kwa mtu mmoja (Rais). Yeye ndiye anayepaswa kutoa kauli juu ya kila jambo, kusuluhisha kila tatizo na kusimamia kila sekta, wakati wale waliokabidhiwa dhamana ya kuongoza wanakaa pembeni wakisubiri amri. Matokeo yake sifa na lawama zote zinamwelekea Rais huku viongozi wa ngazi nyingine wakibaki wasindikizaji wa maamuzi.
Uchawa si tu unadumaza fikra za uongozi, bali pia ni adui wa maendeleo ya taifa. Ili tufikie maendeleo ya kweli tabaka hili la kujikomba lazima litokomezwe.
Ubaya wa UCHAWA
1. Kupoteza haki za wananchi
Viongozi chawa hawafanyi kazi kwa ajili ya wananchi,l bali kwa ajili ya kujipendekeza kwa Rais. Hii inasababisha huduma mbovu kwa wananchi kwani mawazo ya maendeleo yanapimwa kwa kiasi gani yanampendeza mkuu wa nchi badala ya kuleta manufaa kwa jamii. Matokeo yake ni wananchi kuendelea kutaabika huku viongozi wakisubiri neema itoke juu.2. Kukuza rushwa na ufisadi
Uchawa unazalisha mazingira ya rushwa. Viongozi wanapotanguliza maslahi binafsi badala ya maendeleo ya taifa, wanakuwa tayari kupitisha maamuzi yenye maslahi binafsi ili kuendelea kushikilia nafasi zao. Ufisadi unakua kwa kasi kwa sababu hakuna anayethubutu kupinga maamuzi yenye sura ya udanganyifu.3. Kukosekana kwa uwajibikaji
Moja ya athari kubwa za uchawa ni kufifisha uwajibikaji wa viongozi. Badala ya kutoa mawazo mbadala au kupendekeza suluhisho la matatizo ya wananchi, viongozi wanahofia kusema ukweli kwa kuhofia kupoteza nafasi zao. Serikali inayoundwa na viongozi wa namna hii inakuwa dhaifu na isiyo na uthubutu wa kuchukua hatua sahihi kwa manufaa ya nchi.4. Kusababisha migawanyiko ya kisiasa
Uchawa hauwaathiri tu wananchi bali pia huleta migogoro ndani ya serikali. Pale ambapo uongozi unategemea kujipendekeza badala ya ufanisi ,migongano ya madaraka huibuka. Waziri anaweza kupoteza nafasi ya kuonana na Rais kwa sababu kuna mtu mwingine mwenye nafasi ya karibu na Mkuu wa nchi. Hali hii husababisha mivutano ya ndani ya serikali na kushusha ari ya kufanya kazi kwa pamoja kwa maendeleo ya nchi.5. Kudhoofisha demokrasia
Katika mazingira ya uchawa viongozi wanapoteza uhuru wa mawazo na maamuzi. Wanashindwa kusimamia haki za wananchi kwa kuhofia kupingana na matakwa ya Mkuu wa nchi. Matokeo yake ni kuzorota kwa demokrasia, kupotea kwa uhuru wa mawazo na kudhoofika kwa haki za binadamu. Taifa linalokosa uhuru wa maoni linaelekea kwenye utawala wa kiimla.6. Kukosa ufanisi katika utawala
Serikali inayojengwa juu ya msingi wa uchawa haiwezi kuwa na ufanisi. Viongozi hawawezi kutoa maamuzi bora kwa kuwa wanajali zaidi kulinda nafasi zao badala ya kutimiza majukumu yao ipasavyo. Miradi ya maendeleo inacheleweshwa, rasilimali za taifa zinapotea na hatimaye nchi inashindwa kupiga hatua za kimaendeleo kwa kasi inayotakiwa.7. Kuharibu heshima na uadilifu wa viongozi
Viongozi chawa wanapoteza heshima na imani ya wananchi. Wanapoonekana wakitetea kila kitu hata kile kisicho na mantiki, wananchi wanatambua kuwa hawawezi kutumainiwa kusimamia maendeleo yao kwa haki na uwazi. Hili linapunguza imani ya wananchi kwa serikali na kuifanya ionekane kama chombo cha manufaa binafsi badala ya kuwa mtetezi wa maendeleo ya jamii.Hitimisho
Uchawa ni sumu kwa maendeleo ya taifa. Ili Tanzania ifikie maendeleo ya kweli lazima mfumo wa kujipendekeza ukome. Viongozi wanapaswa kufanya kazi kwa mujibu wa majukumu yao na si kwa hofu ya kupoteza nafasi zao.Taifa lenye viongozi waoga na wasio na uthubutu wa kusema ukweli au kufanya maamuzi yenye tija haliwezi kupiga hatua za kimaendeleo. Hatuhitaji viongozi wa "ndiyo mzee", “mama anaupiga mwingi” tunahitaji viongozi wenye uwezo wa kufikiri, kutoa suluhisho na kusimamia maendeleo ya wananchi kwa haki na uwajibikaji.
Ni wakati wa kusema hapana UCHAWA. Taifa linahitaji viongozi NA si wasindikizaji.