Uliza Nkujibu
JF-Expert Member
- Sep 14, 2016
- 806
- 636
Inaboa aisee inaboa sana, ina maana hakuna hata mfanyakazi mmoja wa TBS anaekunywa bia? Hii harufu ya kutu ninayoisikia nikinywa bia ni mimi tu au na wengine mnaisikia?
Watengenezaji wa bia za Castle mnakera, kutu sio nzuri kwa afya ya mwanadamu sasa mnavotulisha siwaelewi mna mpango gani! Mtu unafunguliwa chupa na mhudumu, ukitia mdomoni harufu ya kutu inasikika, sasa kama sio uchafu ni nini?
Kama kutumia chupa kumewashinda tumieni hata packages za plastics, tunaumizana namna hii sio ubinadamu huu.
Nyie mnahitaji hela sisi wateja tunahitaji stimu, tunawapa hela halali mnatupa bia chafu, manake ni nini?
Hebu liangalieni hili kabla sijalifikisha katika vyombo husika.
Watengenezaji wa bia za Castle mnakera, kutu sio nzuri kwa afya ya mwanadamu sasa mnavotulisha siwaelewi mna mpango gani! Mtu unafunguliwa chupa na mhudumu, ukitia mdomoni harufu ya kutu inasikika, sasa kama sio uchafu ni nini?
Kama kutumia chupa kumewashinda tumieni hata packages za plastics, tunaumizana namna hii sio ubinadamu huu.
Nyie mnahitaji hela sisi wateja tunahitaji stimu, tunawapa hela halali mnatupa bia chafu, manake ni nini?
Hebu liangalieni hili kabla sijalifikisha katika vyombo husika.