Harakati za Kupigania Uhuru Tanga

Harakati za Kupigania Uhuru Tanga

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,454
Reaction score
32,980
Mwinyi Mangara tafadhali soma historia hiyo hapo chini kutoka kitabu cha Abdul Sykes inayoendana na picha hiyo uliyotuwekea:

''Kamati hiyo ilikuwa na wajumbe wafuatao: Abdallah Rashid Sembe, Mohamed Kajembe, Victor Mkello, Dhili Mgunya, Ali Mohamed, Abdallah Mohamed na Mohamed Sadik.

Peter Mhando alijitolea nyumba yake kuwa ofisi ya kwanza ya tawi la TANU mjini Tanga.

Mara tu baada ya mkutano huu wazee wa Tanga wakiongozwa na Makoko Rashid, mwanachama wa zamani wa TAA walianza kufanya kampeni kwa ajili ya TANU.

Chama kilipata msukumo mwingine na kuongezeka nguvu wakati Sadik Ali Patwa Muasia tajiri alipoingia TANU.

Patwa alikuwa Muislam wa madhehebu ya Shia.

Patwa alikuwa amehamia Tanganyika kutoka Zanzibar mwaka 1918 baada ya kumalizika kwa Vita Kuu ya Kwanza.

Pale Tanga Patwa alianzisha kiwanda cha soda na akatajirika.

Wakati huo wa zama za ukoloni wakati Waasia wenzake walikuwa wakiwabagua Waafrika, Patwa alikuwa akikaa na Waafrika wa rika lake akinywa nao kahawa.

Halikadhalika watoto wake wakawa wanacheza kandanda na vijana wenzao wa Kiafrika katika vilabu vya Tanga.

Hili lilikuwa jambo geni na lisilokuwa la kawaida kutoka kwa familia ya Kiasia wakati wa ukoloni.''

Patwa alisaidia harakati za kudai uhuru kwa hali na mali, na akaifanyia kampeni TANU miongoni mwa jamii yake mwenyewe ya Kiasia.

Wakati wa harakati Nyerere alikuwa akifanyiana maskhara na Patwa akimwambia, ‘’Mzee Patwa baada ya kupata uhuru nadhani tukuteuwa uwe balozi wetu India.’’

Lakini Patwa hakuiona Tanganyika huru, alifariki kabla ya uhuru kupatikana.

1755449876366.jpeg
1755449921439.jpeg
1755449965819.jpeg

1755449994074.jpeg

1755450028089.jpeg
1755450060014.jpeg

Picha:
1.Sadik Patwa na Julius Nyerere
2.Mwalimu Kihere
3.Peter Abdallah Mhando
4.Mamboleo Rashid Makoko
5.Hamisi Heri
6.Sheikh Abdallah Rashid Sembe
 
Mwinyi Mangara tafadhali soma historia hiyo hapo chini kutoka kitabu cha Abdul Sykes inayoendana na picha hiyo uliyotuwekea:

''Kamati hiyo ilikuwa na wajumbe wafuatao: Abdallah Rashid Sembe, Mohamed Kajembe, Victor Mkello, Dhili Mgunya, Ali Mohamed, Abdallah Mohamed na Mohamed Sadik.

Peter Mhando alijitolea nyumba yake kuwa ofisi ya kwanza ya tawi la TANU mjini Tanga.

Mara tu baada ya mkutano huu wazee wa Tanga wakiongozwa na Makoko Rashid, mwanachama wa zamani wa TAA walianza kufanya kampeni kwa ajili ya TANU.

Chama kilipata msukumo mwingine na kuongezeka nguvu wakati Sadik Ali Patwa Muasia tajiri alipoingia TANU.

Patwa alikuwa Muislam wa madhehebu ya Shia.

Patwa alikuwa amehamia Tanganyika kutoka Zanzibar mwaka 1918 baada ya kumalizika kwa Vita Kuu ya Kwanza.

Pale Tanga Patwa alianzisha kiwanda cha soda na akatajirika.

Wakati huo wa zama za ukoloni wakati Waasia wenzake walikuwa wakiwabagua Waafrika, Patwa alikuwa akikaa na Waafrika wa rika lake akinywa nao kahawa.

Halikadhalika watoto wake wakawa wanacheza kandanda na vijana wenzao wa Kiafrika katika vilabu vya Tanga.

Hili lilikuwa jambo geni na lisilokuwa la kawaida kutoka kwa familia ya Kiasia wakati wa ukoloni.''

Patwa alisaidia harakati za kudai uhuru kwa hali na mali, na akaifanyia kampeni TANU miongoni mwa jamii yake mwenyewe ya Kiasia.

Wakati wa harakati Nyerere alikuwa akifanyiana maskhara na Patwa akimwambia, ‘’Mzee Patwa baada ya kupata uhuru nadhani tukuteuwa uwe balozi wetu India.’’

Lakini Patwa hakuiona Tanganyika huru, alifariki kabla ya uhuru kupatikana.
Hizi hadithi zimepitwa na muda. Kwa sasa waandikie vijana ukombozi wa fikra kwa wakati huu.
 
Hizi hadithi zimepitwa na muda. Kwa sasa waandikie vijana ukombozi wa fikra kwa wakati huu.
Kadhi...
Sina ujuzi wa somo la ukombozi wa fikra.

Tafadhali waombe wenye ujuzi wa ilm hiyo watuandikie.

Kupitwa na muda ndiyo historia yenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom