Halotel ni kiboko kwa internet speed


Hahaha. Khaaaa eti download download. 😄😄😄😄
 
mkuu vocha huku zipo za kumwaga, kweli ina kasi sana
 
Kwa hiyo ni lazima uwe na simu ya 4G ndipo upate spidi nzuri ya tigo au hata kwenye 3G?
 
Kwa hiyo ni lazima uwe na simu ya 4G ndipo upate spidi nzuri ya tigo au hata kwenye 3G?

Nchi hii ukitaka kupata speed nzuri unatakiwa usiwe na mtandao unaoupenda, kuwa na line zote 6 then kila baada ya kipindi fulani test mtandao upi unakupa speed nzuri.

Eneo ambalo tigo hawana watu wengi unapata speed nzuri tu kwa 3g ambayo inaweza fanana hata na wa 4g
 

Utakuwa hujamuelewa jamaa anamaanisha nini.
 

Inawezekana mkuu. Ngoja tusubiri mtandao upate wateja wa kutosha tuone kama watazidiwa ama la. Ila mimi sidhani kama watakuja kuzidiwa kwa sababu hawa jamaa wamefunga 3g minara yao yote. Tofautisha na VODA AU TIGO ambao sehemu kubwa hata hiyo 3g hawana.
 

Sasa sababu halotel wana 3g vijijini na eneo langu tigo wana speed kuliko halotel then niache kutumia tigo nitumie halotel?
 

still poor!
 
Moro-Dar full 3G njia nzima, ya uhakika. Hapa naona tofauti kati ya hawa Halotel na wengine. Miongoni mwa vitu ambavyo vilikuwa vinanishangaza ni kukosekana kwa intaneti ya uhakika katika barabara kuu. Yaani kwa mitandao mingine ukishauacha mji ni shida, hata mjini kwenyewe inachagua maeneo.
Halotel wamenishawishi nitafuta dual sim smartphone na power bank nzuri tu, nikiwa njiani ni raha tu.
Hawa jamaa wako vizuri. Suala la kuchagua maeneo kama lipo basi ni kwa kiasi kidgo sana, binafsi sijawahi kukumbana nalo. Hapa 800MB za kasi kubwa zimeisha ila natazama video YouTube vizuri tu ingawa ubora wa picha umepungua kidogo.
 
Yes wana speed ila hawajafika hapa kwa tiGO, kwenye hii picha hapa chini ni speed ninayopata kwenye dashboard na chini yake ni torrent downloder Bitcomet.


Badae ikapanda mpaka 12.85 Mbps


Hebu toka hilo eneo nenda shemu tofauti, je spidi itabaki hivyo? Yaani hata huo mji uliopo ukienda mtaa mwingine unaweza ukakuta kitu tofauti. Kama kwa halotel kuna kuchagua maeneo basi ni kwa kiasi kidogo sana au hakuna, hiyo ndo tofauti.
Kwa halotel spidi ya mtaani kwako iko sawa na spidi ya mtaa mwingine.
 

4G ya tigo inapatikana kila mahal dsm kwa sasa? nilikua sijanunua line yao mda wanaanza maana uswahilini kwetu ilikua bado haijafika coverage yake!
 
4G ya tigo inapatikana kila mahal dsm kwa sasa? nilikua sijanunua line yao mda wanaanza maana uswahilini kwetu ilikua bado haijafika coverage yake!

nahisi itakua mji mzima maana...maeneo ya kinondoni posta..kko...mabibo ..kigogo...ubungo..mcty...manzese...tandale....mkwajuni..studio...kivukoni....stesheni...mnazi.mmoja.... inakamata vizuri tu..sijajua maeneo mengine ila wako vizuri sana.
 

Hawajafunga 3G minara yao yote.

Kwenye district ambayo ninaisimamia mimi tokea tunaanza kuingia mikataba na wenye maeneo hadi kumaliza ujenzi wa towers, siyo minara yote tuliyofunga 3G japo minara mingi ni ya 3G.
 
hapa kwangu nikiwa bush ni E hadi niwe mjini ndo nipate hyo 3G, kwa hiyo badoooooo ila wajikongoja
 
hapa kwangu nikiwa bush ni E hadi niwe mjini ndo nipate hyo 3G, kwa hiyo badoooooo ila wajikongoja

Muda si mrefu utawekewa 3G.

Kuna kijiji kilikuwa ndani sana tumeweka tower hapakuwa na Airtel, Voda wala tiGo. Baada ya kuiwasha tower na wahusika kuwapelekea lines mnara ulijaa subscribers ndani ya siku tatu hadi makao makuu wakashangaa. Siku hizi tukienda kule wanatushangilia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…