The Guitarist
JF-Expert Member
- Jul 18, 2015
- 3,428
- 4,774
UDHAIFU WAKO NDIYO MAFANIKIO YAKO.
Miaka mingi kabla ya kuwa maarufu katika ulimwengu huu kwa kutumia uwezo wake wa kuburudisha na kuchekesha umati wa watu kama muhusika mkuu katika mfululizo wa filamu mbalimbali za vichekesho huku akijiita Mr Bean. Filamu hizi ndizo zilizomfanya akawa maarufu duniani huku akitajwa kama mwigizaji maarufu zaidi nchini Uingereza.
Bwana Rowan Atkinson alikuwa bado ni kijana mdogo tu kule mitaa ya Newcastle nchini Uingereza mwishoni mwa miaka ya 1950s mpaka mwanzoni mwa 1960s. Kutokana na ucheshi wake watu waliokuwa wakiishi mtaa mmoja na huyu mwamba walijikuta wakipata burudani kutoka kwa kijana huyo na wengi walimtabiria makubwa mbeleni
Alizaliwa January 06 mwaka 1955 katika familia ya kiwango cha kati yaani kama ni fedha basi walikuwa na zakuwatosha kubadilisha mboga tu na sio kuishi kifahari. Huyu jamaa ni msomi wa shahada ya uzamili katika chuo kikuu cha Oxford akibobea katika maswala ya uinjinia wa umeme.
Pamoja na hayo yote Rowan Atkinson almaarufu Mr Bean alikuwa na matamanio ya kuwa muigizaji nguli duniani hivyo kipindi alipokuwa chuo alijiingiza katika vikundi vya uigizaji na akafanikiwa kushiriki matamasha madogo madogo kama yale ya Edinburg Festivals Tringes
Hiyo ikawa kama hamasa ya yeye kutamani kuigiza katika kiwango cha juu zaidi na hapo ndipo matatizo yalipoanzia kwani kila alipojaribu kutafuta nafasi ya kujiunga na vipindi vya runinga alikataliwa sababu kuu ikiwa ni tatizo lake la KIGUGUMIZI japokua alijitahidi kutafuta nafasi zaidi na zaidi aliambulia jibu moja tu HUFAI.
Hapo ndipo akatambua kuwa jambo analopenda hawezi kulifanikisha kwasababu ya udhaifu alio nao. Siku moja akiwa katika mawazo mazito likamjia wazo kwamba kulingana na tatizo lake basi kuna uhusika anaoweza kuutumia ambao hautahitaji yeye kuongea zaidi ya kutenda alijikuta akipata furaha na nguvu ya ajabu. Akarejea tena kuomba nafasi na kuwasilisha wazo lake huku akisema “Nimegundua kwamba ninapoigiza kwa vitendo bila kuzungumza tatizo langu hutoweka”
Safari hii WALIMPUUZA kwa kumuambia hana sura yenye mvuto wala mwili uliojengeka kuvutia watazamaji. Hakika jibu hili lilihitimisha ndoto zake za kupata nafasi ya kuigiza. Hapo akajisemea mwenyewe huwenda sio kila ndoto ni lazima zitimie labda zingine tunaota ili kujifurahisha tu.
Siku zikasogea jamaa akawaza na kuwazua ndipo alipogundua kuwa mtaji wa maskini ni nguvu alizonazo na kama usipofanya wewe hakuna atakaye kufanyia. Na mwisho akaja na wazo la kuanzisha kipindi chake mwenyewe akishirikiana na marafiki zake hapo ndipo akaja na kipindi cha Mr Bean kama muujiza awamu ya kwanza ikawa na mafanikio makubwa hali iliyopelekea kutengenezwa kwa mfululizo wa filamu za Mr Bean na baadae Johnny English kwa mafanikio makubwa akatunukiwa tuzo mbalimbali akavuna na utajiri unaokadiriwa kuwa $130 milioni Huku akimiliki nyumba na magari ya kifahari.
Mwaka 2001 akiwa katika ziara ya mapumziko nchini Kenya ndani ya ndege anayomiliki alikuwa pamoja na familia yake mke wake Sunetra Santry aliyemuoa miaka ya 1980s pamoja na watoto wao Ben na Lily rubani alipoteza fahamu ikamlazimu Mr Bean kukamata uhusika wa kuiendesha bila kuwa na uzoefu wala ujuzi wowote mpaka pale rubani aliporudiwa na fahamu kisha kutua salama katika uwanja Wa ndege wa Wilson Jijini Nairobi. Alipoulizwa aliwezaje kuendesha ndege akajibu alipata maelekezo kupitia sala alizokua akisali katika wakati huo wa hatari.
FUNDISHO
Mafanikio hayahitaji uwe na sura nzuri Pamoja na umbo linalovutia bali yanahitaji kujitoa kwa moyo na kufanya kazi kwa bidii bila kuchoka. Kwakua hakuna binadamu aliyekamilika tujifunze kutumia udhaifu tulionao kama chachu ya kusonga mbele zaidi na zaidi mafanikio yapo kwa wale wanaoamini.
El Artista
Miaka mingi kabla ya kuwa maarufu katika ulimwengu huu kwa kutumia uwezo wake wa kuburudisha na kuchekesha umati wa watu kama muhusika mkuu katika mfululizo wa filamu mbalimbali za vichekesho huku akijiita Mr Bean. Filamu hizi ndizo zilizomfanya akawa maarufu duniani huku akitajwa kama mwigizaji maarufu zaidi nchini Uingereza.
Bwana Rowan Atkinson alikuwa bado ni kijana mdogo tu kule mitaa ya Newcastle nchini Uingereza mwishoni mwa miaka ya 1950s mpaka mwanzoni mwa 1960s. Kutokana na ucheshi wake watu waliokuwa wakiishi mtaa mmoja na huyu mwamba walijikuta wakipata burudani kutoka kwa kijana huyo na wengi walimtabiria makubwa mbeleni
Alizaliwa January 06 mwaka 1955 katika familia ya kiwango cha kati yaani kama ni fedha basi walikuwa na zakuwatosha kubadilisha mboga tu na sio kuishi kifahari. Huyu jamaa ni msomi wa shahada ya uzamili katika chuo kikuu cha Oxford akibobea katika maswala ya uinjinia wa umeme.
Pamoja na hayo yote Rowan Atkinson almaarufu Mr Bean alikuwa na matamanio ya kuwa muigizaji nguli duniani hivyo kipindi alipokuwa chuo alijiingiza katika vikundi vya uigizaji na akafanikiwa kushiriki matamasha madogo madogo kama yale ya Edinburg Festivals Tringes
Hiyo ikawa kama hamasa ya yeye kutamani kuigiza katika kiwango cha juu zaidi na hapo ndipo matatizo yalipoanzia kwani kila alipojaribu kutafuta nafasi ya kujiunga na vipindi vya runinga alikataliwa sababu kuu ikiwa ni tatizo lake la KIGUGUMIZI japokua alijitahidi kutafuta nafasi zaidi na zaidi aliambulia jibu moja tu HUFAI.
Hapo ndipo akatambua kuwa jambo analopenda hawezi kulifanikisha kwasababu ya udhaifu alio nao. Siku moja akiwa katika mawazo mazito likamjia wazo kwamba kulingana na tatizo lake basi kuna uhusika anaoweza kuutumia ambao hautahitaji yeye kuongea zaidi ya kutenda alijikuta akipata furaha na nguvu ya ajabu. Akarejea tena kuomba nafasi na kuwasilisha wazo lake huku akisema “Nimegundua kwamba ninapoigiza kwa vitendo bila kuzungumza tatizo langu hutoweka”
Safari hii WALIMPUUZA kwa kumuambia hana sura yenye mvuto wala mwili uliojengeka kuvutia watazamaji. Hakika jibu hili lilihitimisha ndoto zake za kupata nafasi ya kuigiza. Hapo akajisemea mwenyewe huwenda sio kila ndoto ni lazima zitimie labda zingine tunaota ili kujifurahisha tu.
Siku zikasogea jamaa akawaza na kuwazua ndipo alipogundua kuwa mtaji wa maskini ni nguvu alizonazo na kama usipofanya wewe hakuna atakaye kufanyia. Na mwisho akaja na wazo la kuanzisha kipindi chake mwenyewe akishirikiana na marafiki zake hapo ndipo akaja na kipindi cha Mr Bean kama muujiza awamu ya kwanza ikawa na mafanikio makubwa hali iliyopelekea kutengenezwa kwa mfululizo wa filamu za Mr Bean na baadae Johnny English kwa mafanikio makubwa akatunukiwa tuzo mbalimbali akavuna na utajiri unaokadiriwa kuwa $130 milioni Huku akimiliki nyumba na magari ya kifahari.
Mwaka 2001 akiwa katika ziara ya mapumziko nchini Kenya ndani ya ndege anayomiliki alikuwa pamoja na familia yake mke wake Sunetra Santry aliyemuoa miaka ya 1980s pamoja na watoto wao Ben na Lily rubani alipoteza fahamu ikamlazimu Mr Bean kukamata uhusika wa kuiendesha bila kuwa na uzoefu wala ujuzi wowote mpaka pale rubani aliporudiwa na fahamu kisha kutua salama katika uwanja Wa ndege wa Wilson Jijini Nairobi. Alipoulizwa aliwezaje kuendesha ndege akajibu alipata maelekezo kupitia sala alizokua akisali katika wakati huo wa hatari.
FUNDISHO
Mafanikio hayahitaji uwe na sura nzuri Pamoja na umbo linalovutia bali yanahitaji kujitoa kwa moyo na kufanya kazi kwa bidii bila kuchoka. Kwakua hakuna binadamu aliyekamilika tujifunze kutumia udhaifu tulionao kama chachu ya kusonga mbele zaidi na zaidi mafanikio yapo kwa wale wanaoamini.
El Artista