Hadithi: Msafara Wa Mamba

Hadithi: Msafara Wa Mamba

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,638
Image may contain: 1 person, text


HADITHI: Msafara wa Mamba
SEHEMU: 01
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500

Siku zote kwenye msafara wa mamba huwa haukosi kenge na mijusi. Msichana Herena bila kutegemea amejikuta akisafiri kwenye msafara wa mamba yeye akiwa kama kenge. Lakini yote ni kutokana na siri nzito ya mama yake ambayo imekuwa majuto kwake, lazima amlaumu mama yake kwa nini hakumueleza ukweli. Ni ukweli gani huo fuatana na mtunzi kwenye mkasa huu wa kusisimua.
****
Ni kweli toka nizaliwe nilikuwa simjui baba yangu lakini hiyo haikunipunguzia kitu chochote kwenye maisha yangu. Mama yangu alinilea maisha mazuri kwa kunipa chochote kinachokihitaji, ikiwemo elimu ambayo ni bora katika ulimwengu wa leo wa sayansi na tekinorojia.
Nilisomeshwa shule za gharama tokea kindagate mpaka elimu ya sekondari. Mama yangu alikuwa na mapenzi ya kweli kwangu kwa kunilea kama mboni ya jicho lake. Lakini pamoja na kulelewa malezi ya kudekezwa , sikuielewa tabia ya mama yangu kuwa na mabwana tofauti tena wenye pesa.
Kila mwanaume niliyemuona nilitambulishwa kama mjomba, mwanzoni sijui ilikuwa akili ya utoto nilijua kweli wale ni wajomba. Lakini baada ya kukua na kupata akili pamoja na mama kuniona bado mtoto nisiyejua chochote. Nilitambua kuwa wale si wajomba bali wanaume wa mama.
Hapo moyo ulinishtuka na kumuona mama yangu kama anajichimbia kaburi kwa mikono yake.Yaani kila kukicha mama yangu alibadili wanaume kama nguo, ni kweli Mungu alimjalia umbile na sura ya mvuto. Lakini matumizi yake aliyatumia vibaya ya kuudharirisha utu wake.
Pamoja na kutofurahia tabia za mama yangu lakini sikuwa na uwezo wa kumwambia asifanye vile. Kwanza ningeanzia wapi pili ningemuelezaje? Angeniuliza nina uhakika gani na yale niyasemayo ningemjibu nini.
Maisha yaliendelea huku na mimi nikiendelea na masomo yangu, wakati huo nilikuwa kidato cha pili. Kutokana na uwezo wangu wa akili nilifanya vizuri mtihani wa kidato cha pili na kufanikiwa kuingia kidato cha tatu.
Siku nilipopata matokeo nilirudi nyumbani nikiwa na furaha tele moyoni ya kuweza kuingia kidato cha tatu. Nilipofika nyumbani sebuleni nilimkuta mama akiongea na mzee mmoja ambaye kama sikukosea macho yangu alikuwa mkurugenzi ya moja ya benki jijini.
Nilipoingia nilikwenda moja kwa moja hadi kwa mama na kumkumbatia huku nikipiga kelele za furaha
"Yoyooo mama nimepitaaa."
"Usiniambieee!" mama alijibu huku akinikumbatika kwa nguvu.
"Kweli mama, tena pamoja na rafiki yangu Fatuma."
"Oooh hongereni sana."
"Asante mama," nilijibu huku machozi ya furaha yakinitoka.
"Sasa mwanangu nitakutayarishia zawadi yoyote uitakayo."
"Ooh, asante mama nashukuru, mama unakumbuka ulisema utaninunulia simu ya laki tano?"
"Kama nilivyo kwambia ahadi zangu zipo palepale."
"Vipi huyu ni binti yako?" aliuliza yule mgeni.
"Ndio...tena wa pekee."
"Mmh! Basi na mimi naongezea zawadi."
"Anko zawadi gani?" niliuliza kwa shauku.
"Kwanza nitakulipia kidato cha tatu mpaka cha nne, kisha nitakutafutia shule ya hadhi ya juu ambayo utasoma kidato cha tano na sita kisha kitakutafutia chuo nje ya nchi."
"Usiniambie Anko," nilijikuta nimemkumbatia Anko kwa furaha bila kujijua.
"Usiwe na wasi jione mtu mwenye bahati, leo hii nitakufungulia akaunti kwenye benki yangu, sawa binti?"
"Mjomba Mungu akuzidishie."
"Asante."
Kama kawaida yangu nilikwenda chumbani kwangu ambako kulikuwa na kila kitu. Kutokana na tabia za mama hakupenda nitumie sebule zaidi ya kuniwekea vitu muhimu chumbani kwangu. Kama tivii na redio kubwa pamoja na kompyuta.
Siku zote nikimaliza kuongea na mama huenda chumbani kwangu na kukutana naye kipindi cha chakula, mara nyingi mama alipenda tule pamoja. Nilikwenda chumbani kwangu na kuendelea na programu zangu za mazoezi ya kompyuta.
Nikiwa chumbani kwangu mama alinifuata kunieleza kuwa mjomba wa benki anataka kuniaga. Nilikwenda hadi sebuleni na kumkuta mjomba akijiandaa kuondoka, aliponiona alinisogelea na kunishika kichwani huku akichezea nywele zangu fupi:
"Herena kesho njoo ofisini ukitoka shule ili upigwe picha na kukufungulia akaunti yako."
"Sawa Anko, lakini kesho siendi shule mpaka shule itakapofunguliwa kwa ajili ya kujiunga na kudato cha tatu."
"Ooh, vizuri basi kesho njoo na mama yako ili nimpe pesa za malipo ya miaka miwili na wewe ufungue akaunti yako kabisa."
"Asante Anko Mungu akuzidishie," sikuamini yote aliyokuwa akiyasema niliona kama ndoto. Mjomba huyu alikuwa tofauti na wote ambao walikuja pale nyumbani wengi walinipa pesa si suala la maendeleo yangu.
****
Siku ya pili mimi na mama tulikwenda hadi pale kwenye ile benki, tulipokelewa kama waheshimiwa fulani. Mkurugenzi mwenyewe ndiye aliyesimamia kufungua akaunti yangu japo kulikuwa na watu wengi. Baada ya kufungua akanti Anko ambaye nilijua ni mpenzi wa mama yangu alimpa mama pesa ambayo sikujua idadi yake.
Tulipotoka pale benki tulikwenda moja kwa moja hadi shule ambapo mama alilipa karo ya shule ya miaka miwili nikishuhudia kwa macho yangu. Baada ya pale tulirudi nyumbani nikiwa na furaha tele na kuwa na uhakika wa maisha yangu kwa kupata elimu mpaka mwisho wa pumzi yangu.
Malengo yangu yalikuwa ni kusoma kwa bidii ili nifike mbali kielimu na kuweza kupata kazi ambayo ingenifanya nisiwe mwanamke tegemezi. Moyoni nilijiapiza kamwe sitaifanya kazi chafu kama ya mama ya kutouthamini mwili wake na utu wake.
Japo hakuwa na mume lakini alitakiwa atafute bwana mmoja ambaye ndiye atakaye kuwa mume wangu na kujijengea heshima mbele ya jamii. Kwa hali ile niliuapia moyo wangu nitasoma kwa bidii zote na kwa nguvu zangu zote.
Nakumbuka siku moja niliporudi nyuimbani kutoka twesheni, sebuleni nilimkuta mama na mwanaume mwingine. Sio siri kwa mara ya kwanza nilichukizwa na kitendo kile cha kukosa heshima na kushindwa kujiheshimu. Ilikuwa ni wiki tu nimepata ufadhiri wa kusomeshwa mpaka mwisho wa maisha yangu.
Nilijiuliza kama atatokea Anko wa benki na kuikuta hali ile kungekuwa na usalama kweli au hatima yangu itakuwa nini kama sio kukatishwa kwa huduma muhimu ambazo ndizo ufunguo wa maisha yangu. Kuliko kutegemea kitega uchumi cha mwili.
Kwa kweli nilikasikilika sana na kujikuta nikisimama mbele ya mama na yule mgeni kama jini la kutumwa na kuuliza:
"Mama huyu nani?"
"Aaah huyu Anko Mody," alijibu huku akinilazimisha nikubaliane na upuuzi wake.
"Anafanya nini hapa?"
"Herena ni maswali gani, unafikili bila kuwa karibu na watu hawa maisha yetu yatakuwa magumu."
"Mama Mungu akupe mara ngapi, huyu bwana atakusaidia nini?"
"Herena hebu toka mbele yangu umefikia hatua ya kunikosea adabu mbele ya wageni au kwa vile nakupenda sana?"
"Noooo mama nasema hivi naomba mgeni aondoke sitaki kumuona," niligeuka mkali kama pilipili.
"Herenaaaa! Hebu ondoka mbele yangu sitaki kukuona nitakubadilikia sasa hivi," mama alinitisha, pamoja na vitisho vya mama sikuwa tayari kuendelea kuuona uchafu ule. Nilijua yule atakuwa wa mfano. Niligeuka na kuelekea jikoni ili nije nimuonyeshe mama mimi ni nani?

Nini kitaendelea? Endelea kufuatilia. Soma Chombezo jipya tamu la TOROJO BAMIA ( Winga teleza) linaanza katika group la Whatsapp jiunge sasa.
 
HADITHI: Msafara wa Mamba
SEHEMU: 02
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
"Mama Mungu akupe mara ngapi, huyu bwana atakusaidia nini?"
"Herena hebu toka mbele yangu umefikia hatua ya kunikosea adabu mbele ya wageni au kwa vile nakupenda sana?"
"Noooo mama nasema hivi naomba mgeni aondoke sitaki kumuona," niligeuka mkali kama pilipili.
"Herenaaaa! Hebu ondoka mbele yangu sitaki kukuona nitakubadilikia sasa hivi," mama alinitisha, pamoja na vitisho vya mama sikuwa tayari kuendelea kuuona uchafu ule. Nilijua yule atakuwa wa mfano. Niligeuka na kuelekea jikoni ili nije nimuonyeshe mama mimi ni nani?
SASA ENDELEA…

Nilikwenda hadi jikoni na kutafuta kisu lakini nilipata kisu kidogo, nilipekua pekua lakini sikufanikiwa kupata kisu kikubwa. Nilipoangalia pembeni nilikutana na sufulia aliyokuwa imejaa maji machafu ya vyombo tulivyolia usiku.
Kwa bahati mbaya siku ile mfanyakazi alikuwa anaumwa na vyombo vilinisubiri mimi. Nilibeba lile sufulia la shombo ya vyakula tulivyokula jana yake usiku. Nilitoka nalo hadi sebuleni na kumkuta mama akiendelea kuongea na mgeni wake bila wasiwasi wowote.
Bila kuwashitua nilikwenda hadi pale na kumwagia mgeni shombo la uvundo wa samaki na mchanganyiko wa vyakula. Alijaribu kuyakwepa lakini alichelewa shati lote lilijaa ukoko, nilifoka kwa sauti:
"Nasema toka la sivyo yatakukuta makubwa," nilisema yale huku nikielekea jikoni kutafuta chochote cha kumpigia na zaidi ningemuitia kelele za wizi.
Nilikwenda hadi jikoni huku nikilia kwa uchungu na kupitia kisu cha mkate na kutoka nacho. Mama aliponiona alipiga kelele akimwambia yule mgeni akimbie. Baada ya mgeni kukimbia nilikitupa kisu chini na kuanza kulia.
Mama alinibembeleza huku akiniomba msamaha:
"Basi mwanangu nimekosa."
"Mama haya ni maisha gani?"
"Basi mwanangu, lakini hawa ndio wanaoendesha maisha yetu ya kila siku."
"Hapana...hapana si kweli, hivi mama mngekuwa na mjomba sijui ba’ mdogo mmoja kama yule wa benki ungekuwa amepungukiwa nini?"
"Ni kweli, lakini yule ni mume wa mtu wakati wowote anaweza kukata mawasiliano tutaishi vipi. Kama unavyojua mama yako sina mume sina kazi lakini mwanangu unaishi maisha mazuri pengine kuliko watoto wengi wenye wazazi wawili."
"Yote unayosema sikatai, lakini ulitakiwa kuwa na mwanaume mmoja ambaye atakuwa kama mumeo. Sio kila mwanaume wako mama kwa mtindo huu kuna kupona kweli?"
"Mwanangu hiyo ni mipango ya Mungu."
"Mipango ya Mungu pamoja na kujilinda."
"Basi nimekusikia mwanangu nitafanya hivyo."
Kuanzia siku ile pale nyumbani mwanaume mmoja aliyeruhusiwa alikuwa Anko wa benki tu.Wote niliowakuta niliwatoa kama siwajui, huku nikiwaeleza baba amerudi. Waliponihoji alikuwa wapi niliwajibu hiyo siyo juu yao.
Lakini toka niliwapiga marufuku wale wanaume, mama naye akawa tena si wa kushinda nyumbani kama zamani. Kila niliporudi nilikuwa simkuti, ilifikia hatua ya kupita hata siku mbili bila kuonana. Kuna kipindi Anko wa benki alipokuja nymbani hakumkuta na simu alipompigia ilikuwa haipatikani.
Kweli mzowea punda farasi kupanda hawezi, ilionyesha mama yangu jinsi gani alivyopenda kuwa na wanaume wengi na kuamua kuwafuata baada ya kuwapiga marufuku kuwaona pale nyumbani zaidi ya Anko wa benki.
Siku moja nilipokwenda kumtembelea Anko wa benki, siku ile sikumkuta kwenye hali yake niliyoizoea. Alionekana kama mgonjwa kitu kilichonifanya nihoji kulikoni.
"Anko vipi unaumwa?"
"Herena mama yako ana matatizo gani?"
"Kwa nini Anko?"
"Yaani nimeisha mfumania na wanaume tofauti zaidi ya watano na kumsamehe, lakini sasa imetosha mimi na yeye tumeisha vunja mkataba," kauli ile iliushtua moyo wangu na kujikuta nikipiga ukelele wa mshtuko.
"Toba! Mbona mkosi huu," nilisema yale huku nikishika mikono kifuani kwa mshtuko.
"Lakini Herena pamoja na kuvunja ukataba na mama yako, bado nitaendelea kukuhudumia kama nilivyo kuahidi. Nimesikia juhudi zako za kumkanya mama yako, hiyo imenipelekea kutositisha huduma zangu kwako. Nitakufanyia kama nilivyokuahidi ila mimi na mama yako inatosha. Herena mimi mtu mkubwa siwezi kuchangia wanuka jasho."
"Ooh! Mungu mkubwa, asante Anko," nilimshukuru nusra nimalambe miguu.
Niliporudi nyumbani nilimkuta mama yupo kwenye hali ya kawaida kama hakuna kitu kilichotokea. Ilionyesha kiasi gani mama yangu jinsi moyo wake ulivyo na sugu, hakubabaika na kitu wala kuonyesha mabadiliko yoyote.
Baada ya shughuli za kutwa nzima na chakula cha usiku, nilikaa na mama na kumuuliza juu ya Anko wa benki.
"Mama vipi Anko wa benki?"
"Kuhusu nini?"
"Eti mmekorofishana?"
"Tatizo nini? Huli...huvai....husomi?"
"Hapana mama."
"Alinikuta na amenicha, kuondoka kwake sipungukiwi na kitu amenikuta nifurahia maisha na nitaendelea kuyafurahia maisha."
Mmh maneno ya mama yalinifanya niwee mpole kwa kuwa hakuonyesha kubabaika na tukio lililotokea japo kwa upande wangu liliutikisa moyo wangu. Nilimuaga mama na kwenda kulala huku nikilaani kiburi cha shetani cha kumpotosha mama yangu.
******
Siku zilikatika na mama aliendelea na tabia zake za kuuza mwili wake bila kuangalia madhara yake siku za usoni. Anko wa benki na yeye aliendelea kuhudumia bila kinyongo huku akinipa pesa za matumizi ambazo kwa upande wa mama zilikuwa zimekata eti kwa sababu ya kuwatimua wanaume zake.
Mama akaanza kuumwa kidogo kidogo, kila tulipokwenda hospitali tulitibu na kupata nafuu. Kuna kipindi hushikika na kulala kitandani na kushindwa kutoka nje. Maradhi yale mama yangu yalimfanya ayumbe kidogo.
Lakini mama alikuwa na pesa kidogo benki ilimsaidia kutupunguzia ukali wa maisha. Pesa nyingi alizitumia kwa waganga wa kienyeji kwa kusema amerogwa. Pesa benki zilipoisha, ilibidi na mimi nizichukue nilizoingiziwa na Anko wa benki.
Kwa kweli pesa zilikuwa nyingi kidogo, ambazo zilitusaidia kupunguza makali ya maisha ikiwa pamoja na kumsaidia kulipia malipo ya waganga pamoja na dawa alizoagizwa kununua. Alipopata unafuu kidogo alitoka kama kawaida yake.
Lakini kila alipokuwa akitoka alirudi asubuhi akiwa hoi na kunisababishia nisiende shule ili kumuhudumia. Kutokana na hali ya mama kumzidia kila akienda kulala nje, nilimshauri ajipumzishe ili kuangalia hali yake. Nilishukuru Mungu mama yangu alinisikiliza na kuamua kutulia nyumbani.
Mabwana walipomfuata niliwafukuza kama wizi, japo mama aliniomba niwaache waingie ndani. Kusikuwa tayari kukubali uchafu ule kutokana na wao kusababisha mama na mjomba wa benki kuachana. Kila nilipomkumbuka mjomba wa benki roho iliniuma sana.
Lakini ningefanya nini kwa vile ni mtoto mdogo kila nitakacho mweleza atakiona cha kitoto. Kwa kweli pamoja ya ugumu wa maisha sikuwa tayari kukubali kuwaona wanaume wa mama ndani kwetu. Mama alinikubalia kwa shingo upande, nami sikulegeza uzi wa kuhakikisha hali ya mama yangu inaimalika.
Namshukuru Mungu kipindi kile nilikuwa likizo muda mwingi nilikuwa karibu ya mama. Faraja nyingine niliyoipata ni kutokana na kukuta akiba yangu Anko wa benki ameniongezea. Nilikuwa sina budi kumfuata kazini kwake kumshukuru.
Aliponiona alifurahi sana kwa kwenda kumtembelea, aliniuliza hali ya mama.
"Herena vipi mama yako yupo?"
"Yupo, lakini alikuwa akiumwa"
"Oooh mpe pole, anaendeleaje?"
"Sasa hajambo kidogo."
"Na tabia zake?" Mmmh lilikuwa swali gumu, lakini nilijilazimisha kujibu.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Msafara wa Mamba
SEHEMU: 03
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Namshukuru Mungu kipindi kile nilikuwa likizo muda mwingi nilikuwa karibu ya mama. Faraja nyingine niliyoipata ni kutokana na kukuta akiba yangu Anko wa benki ameniongezea. Nilikuwa sina budi kumfuata kazini kwake kumshukuru.
Aliponiona alifurahi sana kwa kwenda kumtembelea, aliniuliza hali ya mama.
"Herena vipi mama yako yupo?"
"Yupo, lakini alikuwa akiumwa"
"Oooh mpe pole, anaendeleaje?"
"Sasa hajambo kidogo."
"Na tabia zake?" Mmmh lilikuwa swali gumu, lakini nilijilazimisha kujibu:
SASA ENDELEA…
"Kidogo ametulia."
"Una uhakika gani?"
"Siku hizi muda wote yupo nyumbani."
"Labda sababu ya ugongwa."
"Hapana sasa amebadilika," nilimtetea mama ili Anko alirudishe moyo kwa mama.
"Unajua nini Herena?"
"Hata Anko?"
"Yaani mama yako amenichanganya sana, nilikuwa nina mipango mizuri sana kwenu, hasa wewe."
Kauli ile iliuumiza moyo wangu na kujikuta nikimlaumu mama kwa tamaa zake za muda mfupi, nilijikuta nikijibu kwa sauti ya unyonge.
"Ndiyo hivyo tena sina jinsi, akili za mtu haziazimwi."
"Lakini Herena kuna kitu nimekuandalia kizuri sana."
"Kipi hicho Anko?" nilijikuta nikiuliza kwa shauku kujua nini ameniandalia.
"Taratibu Herena, utakijua siku si nyingi."
"Sawa Anko nakisubiri kwa hamu kubwa."
Niliagana na Anko wa benki na kunipa pesa za matumizi laki mbili. Yaani sikuamini ukarimu wa Anko, nilitamani kama angekuwa baba yangu mzazi. Nilijikuta nikitembea barabara nzima huku nikilia na kutamani kumjua baba yangu.
Nilifika nyumbani macho yamenivimba kwa kulia njia nzima, hata dereva wa teksi alinishangaa na kutaka kujua kulikoni. Lakini nilimdanganya mama yangu ni mgonjwa na nilikuwa natoka kwa baba.
Nilipoingia ndani mama alishtuka kuniona nikiwa kwenye hali ile, alinikimbia na kunihoji kutaka kujua kulikoni?. Nilijikuta nikijitupa chini na kuendeleza kilio, kilicho mchanganya mama.
"Herena mwanangu umekuwaje?" sikumjibu niliendelea kulia huku nikigaagaa chini.
"Vipi umeibiwa?"
"Heri ningeibiwa."
"Sasa umekubwa na maswahibu gani?"
"Mama baba yangu ni nani?" nilimuuliza bila sauti ya kilio ilikuwa sauti kavu inayohitaji jibu sahihi.
"Herena nini?" mama aliniuliza kama hakunisikia vizuri.
"Mama namtaka baba yangu."
"We mwana yameanza lini?"
"Leo."
"Kwani tatizo nini?"
"Tatizo ni kwamba namtaka baba yangu, kila mmoja ana baba na mama heri baba yangu ningejua amekufa ningejua moja"
"Herena mbona mwanangu unanipa kazi nzito."
"Mama kunieleza baba yangu ni fulani hiyo ni kazi nzito?"
"Mmh! Mwanangu sijui nianzie wapi?"
"Mamaa uanzie wapi kivipi au sio mtoto wako uliniokota?"
"Mwanangu wapi unakoelekea huku?"
"Kuna ugumu gani kunieleza baba yako fulani, kama huwezi ni wazi mimi si mwanao."
"Herena naomba suala la baba yako uliache kama lilivyo."
"Hapana mama kuna umuhimu kumtafuta baba na mama yangu wa kweli."
"Herena mwangu kwa haki ya Mungu mimi ni mama yako mzazi."
Mama alijiapiza miungu yote.
"Kama wewe ni mama yangu baba yangu ni nani?"
Mama kabla ya kujibu aliinama kwa muda, mara nilimuona akidondokwa na machozi. Japo sikupenda kumuona mama yangu hata siku moja akitokwa na machozi kwa ajili yangu. Lakini kwa suala lililokuwa mbele yangu sikuwa na huruma kwa mama zaidi ya kuelezwa ukweli.
Nilimuacha mama alie na akimaliza anieleze ukweli juu ya mzazi wangu wa kiume yupo wapi. Mama alitulia kwa muda huku akiendelea kububujikwa na machozi. Baada ya kulia kwa muda alinyamaza na kuvuta kamasi nyepesi.
Kisha aliniangalia kwa jicho lililokuwa jekundu na kuanza kuvimba, sio siri nilimuonea huruma mama yangu hasa kutokana na hali aliyokuwa nayo. Baada ya kuniangalia aliniita jina langu
"Herena."
"Abee mama."
"Mwanangu kwa nini leo umeniuliza neno hili?"
"Mama hivi kuulizia juu ya baba yangu kuna ubaya? Roho uniuma kila niwaonapo wenzangu na baba zao. Vilevile naamini kama baba yangu angekuwepo aibu hii isingetokea."
"Herena mwanangu kwa ukweli wa moyo wangu baba yako simjui."
Kauli ya mama ilikuwa ya kuchekesha lakini kwangu ni kama kuupasua moyo bila ganzi
"Eti nini?" nilimuuliza nikiwa nimemsimamia mbele kama jini la kutumwa.
"Ni kweli kabisa mwanangu baba yako simjui."
"Mama yangu mbona unanichekesha, baba yangu humjui mimba yangu ilijitunga?"
"Herena mwanangu japo sikutaka ulijue hili ambalo linaweza kuupokonya moyo wako furaha ya kila siku. Ndio maana nilikubali niadhirike mwanangu, lakini nihakikishe unaishi maisha yenye furaha na kutopungukiwa na kitu," mama alimeza mate kisha aliendelea.
"Herena mwanangu maisha niliyoishi mama yako sikupenda hata siku moja mwanangu uyajue, lakini sina jinsi zaidi ya kukueleza ukweli. Herena mimi mama yako nimefikia kufanya kazi hii baada ya kuikimbia elimu na kuyakimbilia maisha.
“Ukweli mama yako nimeacha shule nikiwa darasa la sita, baada ya kudanganywa na mwanaume mmoja aliyenitoroshea mjini. Mwanzo nilijua mama yako nimepata, kutokana na kuishi maisha mazuri tofauti na ya kijijini. Mwanangu kumbe bwana yangu alikuwa ni jambazi.
Siku moja nikiwa ndani nimekaa kwenye tivii, niliona picha ya jambazi lililouawa. Picha iliposogezwa karibu, mwanangu nilichanganyikiwa. Kibaya zaidi pale sikuwa nawajua ndugu zake, sikutaka kujitokeza.
“ Bwana yangu alizikwa na jiji, nami eneo lile sikuweza tena kukaa kwa kuhofia macho ya watu. Vilevile nilijua lazima wana usalama watataka kujua siri zaidi ya mume wangu. Nilihama usiku usiku na kuhamia sehemu ya mbali ambako nilikuwa sijulikani.
“Huku niliyaanza maisha nikiwa peke yangu, japo ilikuwa peke yangu sikuona tatizo lolote kutokana na hawara yangu kuniachia pesa nyingi. Kwa kweli sikupungukiwa na kitu na kujiona nitaishi maisha yoyote niyatakayo .
Niliyaishi maisha ya kuitanua na kwenda kumbi zote za starehe wakati nikiwa na baba yako huyo."
"Ina maana ndiye baba yangu?" nilimuuliza mama
"Hapana kwa vile nilishea naye mwili ni baba yako."
"Nimekuelewa, endelea."
"Basi mwanangu kama ujuavyo mali bila daftali huisha bila habari na bandu bandu humaliza gogo. Pesa ziliisha taratibu bila kujua kuja kushtukia pesa zimekwisha na mimi ndio hivyo sikuwa na mradi hapo ndipo mama yako nilipoingia kwenye kazi ya kutumia mradi wa mwili wangu.
“Aliyenifundisha ni shoga yangu ambaye tulikuwa majirani mwanangu japo kazi ilikuwa ya kunidhalilisha lakini ilikuwa inalipa na kunipunguzia ukali wa maisha. Kutokana na kutembea na wanaume wengi nilijikuta nashika ujauzito na aliyenipa sikumtambua.
“Hiyo ndiyo iliyokuwa mimba yako, kwa kweli mpaka leo baba yako simjui mimba yako niliipata kwenye ukahaba. Mimba yako kidogo initoe roho baada ya kujaribu kuitoa bila mafanikio. Ukweli Mungu hakupenda nikuue bila sababu, baada ya kushindikana nilikubali kuilea na kufanikiwa kujifungua salama.
Kutokana matatizo niliyokumbana nayo niliamua kukitoa kizazi."
Kufika hapo mama aliinama na kububunikwa na machozi kisha alijifuta na kuendelea kunipa simulizi nzito. Roho iliniuma sana kwa kujua mimba yangu imepatikana kwenye biashara ya mwili hivyo kushindwa kumjua baba yangu.
"Basi mwanangu, baada ya kujijua sina kizazi nilihamishia mapenzi yangu yote kwako. Nilihamishia nguvu zangu zote kwako kuhakikisha unapata maisha mazuri elimu bora ili usijeishi maisha niliyoishi mama yako."
Mama alitulia kama anawaza kitu kisha aliendelea kunipa simulizi ambazo kwa upande wangu zilikuwa sawa na kuupasua moyo wangu bila ganzi. Sijui maumivu yake yako vipi ukiyapimia, nilishindwa kulia kutokana na kumuonea huruma mama yangu kwa simulizi yake ambayo hakupenda niijue.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Msafara wa Mamba
SEHEMU: 04
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500

ILIPOISHIA:
Mama alitulia kama anawaza kitu kisha aliendelea kunipa simulizi ambazo kwa upande wangu zilikuwa sawa na kuupasua moyo wangu bila ganzi. Sijui maumivu yake yako vipi ukiyapimia, nilishindwa kulia kutokana na kumuonea huruma mama yangu kwa simulizi yake ambayo hakupenda niijue.
SASA ENDELEA…
Mashavu ya mama yalibeba michirizi ya machozi na macho yake yalikuwa yamevimba na kuwa mekundu kwa kulia kilio cha kwikwi kilichoambatana na simulizi.
"Mwanangu sikupenda hata siku moja uijue historia hii najua lazima itaujeruhi moyo wako na kukufanya upoteze mwelekeo wa maisha yako. Sitajisikia furaha pale nitakaposikia amevunjika moyo wako aliouonyesha katika masomo...
Mwanangu Herena japo sipendi kuongea habari hizi mbele yako, mama yako nilibweteka na uzuri wangu na kujiona nina rasilimali ya kuweza kunisaidia katika maisha yangu. Mwanangu uzuri umeniponza mama yako."
Kufikia hapo mama alianza kulia na kushindwa kuelewa uzuri umemponza kivipi. Nilitulia tuli huku roho ikiniuma na machozi yalishindwa kujizuia yalitoka bila kupenda, nilimuonea huruma mama yangu. Baada ya kufuta machozi na kamasi nyembamba aliendelea kunisimulia.
"Mwanangu uzuri nilionao mama yako nilifuatwa na wanaume kama malkia wa nyuki. Mama yako nilishindwa kuchagua nimkubali yupi kila mmoja alimzidi mwenzie dau. Kwa kweli kila aliyekuja nilimpokea niliweka masirahi mbele.
“Muda mfupi mama yako niliweza kuishi maisha nusu ya peponi, huku nikikutunza kama mboni ya jicho langu. Ajabu nyingine mwanangu nilijikuta nimekumbwa na ugonjwa wa ngono wa kutoridhika na mwanaume mmoja.
“Mwanangu unashangaa kuachana na Anko wako wa benki, mbona hata mshipa wa fahamu haunigongi. Nimeachana waziri mkubwa serikalini nini nilichokikosa na ndiye aliyenijengea nyumba hii na kuninunulia vitu vyote na benki aliniwekea pesa lukuki.
"Tena.." mama alisita kidogo kuendelea kuzungumza na kujifikiria jambo na kuamua kuendelea kunisimulia
"Mwanangu japo maneno mengine hupaswi kuyasikia lakini hakuna jinsi kwa vile sipendi kosa nililolifanya unalirudia. Yaani mwanangu vitu vingine mbona aibu yaani sijui nimerogwa ugonjwa gani wa kupenda ngono kupindukia...
Anko wako wa Serikalini alinifumania na muuza mchicha.. mmh we acha yaani muuza mchicha mwenyewe pesa nilikuwa nampa mimi," Mmmh yaani sijui niseme nini nilimuangalia mama yangu na maneno yake kwa kumshusha na kumpandisha bila kupata jibu. Nilijua hakuna ugonjwa bali ni kujiendekeza na matokeo yake kuwa wazoea.
"Basi mwanangu kama nilivyo kwambia mama yako nilikuwa kama malkia wa nyuki nilipo achana na Muheshimiwa yule nilipata muarabu mmoja ambaye sikukaa naye sana kutokana na tabia zake chafu ambazo hizo hupaswi kuzijua ila elewa tulishindwana tabia.
“ Kwa kweli sikuyumba hata siku moja na maisha yaliendelea kuwa mazuri. Nina imani hata siku moja hukuteteleka katika maisha yako, hata uliponiuliza kuhusu baba yako na kukukanya uliziba mdomo wako.
“ Lakini ajabu tabia yako iliyobadilika ghafla tena yenye msimamo ilinichanganya sana. Pamoja na kukutisha hukuonekana kutetereka na msimamo wako ulikuwa pale pale kuhusu kuwafukuza wanaume zangu. Niliweza kusalimu amri na nyumba yangu kwa kweli imerudisha heshima.
“Niliamua kufanya mambo yangu nje ya hapa, lakini kwa bahati mbaya nimeandamwa na maradhi. Kwa kweli nilishindwa kutulia nyumbani kutokana mradi wangu wa mwili nisingeweza kutulia nyumbani. Kutokana na sehemu kubwa ya mahitaji yangu kupatikana kwa njia ya kuutoa mwili wangu.
“ Sina budi kukushukuru kwa kuweza kunizuia kutoka nje ili kuokoa hali yangu. Kwa kweli nilikuwa siamini hata siku moja kama akili za mtoto zinaweza kumsaidia mtu mzima. Kweli usidharau usicho kijua, ila leo umekuja na mapya ya kutaka kujua kumjua baba yako sina budi kukueleza ukweli.
“Naomba unisamehe mwanangu, hiyo ndiyo kweli ila nakuomba mwanangu habari hizi zisikukatishe tamaa".
Mama alinipigia magoti, kwa kweli roho iliniuma na kumuonea huruma mama yangu. Nilimshika mabegani na kumnyanyua, tulikumbatiana kila mmoja alilia na kumlowesha mwenzake machozi.
Mama alikuwa wa kwanza kunyamaza na kuninyamazisha mimi, nilinyamaza na kumuomba mama japo maji yameisha mwagika abadilike tabia. Mama alikubali kubadilika ili kuilinda afya yake na kumuomba aende kwa Anko wa benki kumuomba msamaha.
Lakini mama alikataa alisema katu hawezi kurudiana na mtu aliyeachana naye. Sikuwa na uwezo wa kumlazimisha, nilimuomba mama tuanzishe mradi ili tuepukane na maisha tegemezi hata kama mjomba atakapositisha huduma zake.
Tuliyaanza maisha mapya ambayo japo hatukuwa juu kiuwezo, lakini mama alibadilika kwa kiasi kikubwa. Kwa kweli hata mimi moyo ulitulia japo sikumjua baba yangu na jinsi mimba yangu ilivyopatikana, sikutaka habari zile zinikatishe tamaa. Niliamua kusoma kwa bidii ili kujikwamua na hali iliyokuwa ikija mbele yetu.
Anko wa benki aliendelea kunihudumia kama mtoto wake, na hali ya mama iliendelea kuimalika siku hadi siku. Ajabu mama alinenepa na kunawili, wakati huo mama alikuwa amefungua palepale nyumbani duka la kuuza vocha na kupigisha simu pamoja na kuuza mawigi na vitu vya kike.
Kidogo ilisaidia kupata pesa ndogo ndogo za matumizi, pesa zote nilizoingiziwa na Anko wa benki niliongezea kwenye duka na kuongezea vipodozi. Lilionekana duka lililoshiba na kuweza kutupatia kipato chenye kutuwezesha kuweka angalau pesa kidogo kwa wiki. Kweli mzowea punda farasi hamuwezi, mama baada ya kupendeza akaanza kubadilika na kurudia tabia yake ya awali ya ukahaba. Kila nilivyo mkanya alikuja juu na kusema yeye anajua zaidi yangu kwa vile ameona jua kabla yangu.
Mama alibadilika kwa kiasi kikubwa na kurudi nyumbani amelewa, tabia zile zilinichanganya kwa kiasi kikubwa na kusababisha hata kuyumba kimasomo. Mama hakutaka kabisa kunisikiliza na mara nyingi alikuwa mkali kwa kutotaka kunisikiliza.
Siku moja nilikwenda ofisini kwa Anko wa benki, kwa kweli hakunipokea kama ilivyo kawaida. Nilishangaa na kumuuliza kulikoni, aliyonieleza yaliniacha mdomo wazi kwa kusema:
Kuwa amekutana na mama yangu kwenye pati akiwa na mkewe yaani mke wa Anko. Mama alikuwa na mwanaume wake, alipomuona alianza kumtukana na kusema pesa zake ndizo zinazo nitia mimi kiburi cha kukosa heshima. Kwa hiyo alimuomba aache mara moja kumihudumia.
Mjomba alisema alipata aibu mbele ya mkewe na kusababisha ugomvi mkubwa na mkewe. Kwa hiyo ameamua kusitisha huduma kwangu mara moja.
Kauli ile ililivuruga tumbo langu na kunifanya nisikie tumbo la kuhara. Nilimbembeleza mjomba, lakini hakuwa tayari kunisaidia na kuniuliza swali:
"Herena."
"Abee Anko," niliitikia huku nikilia.
"Mimi mzazi wako?"
"Hapana."
"Nina imani una baba yako, lakini nimeamua kubeba jukumu la kukulea kutokana na tabia zako na juhudi zako kimasomo. Na nilikuwa sikujui bila mama yako na mama yako ndiye aliyenipiga marufuku sasa mimi nifanyeje?"
"Hapana Anko naomba unisaidie nitakimbilia wapi?" nilipiga magoti mbele yake.
"Herena itakuwa vigumu kama aliweza kunieleza vile mbele ya mke wangu nikirudia si atanifuata nyumbani au hata kusema nimekubaka na kunishushia heshima yangu..Mfuate baba yako."
"Anko, sina baba."
"Mimba mama yako amejibebesha?"
"Nilipatikana kwa njia ya kukutana na wanaume tofauti na kushindwa kumjua baba yangu," ilibidi nijivue nguo mbele ya Anko labda ningepata msamaha, lakini haikusaidia kitu.
"Ooh, pole sana ndio hivyo sina jinsi siyo mimi ni mama yako nina imani huenda amekuandalia maisha mazuri ndio maana amekuambia amewahi kuona jua hivyo muachie. Hata ulipofikia hujui pesa alipata vipi, tena sasa hivi analipa. Amerudi kwenye hali yake ya zamani. Utapata baba mpya au yatari ameisha mpata."
Maneno ya Anko niliona sasa yanaelekea kunisimanga, sikutaka kuongeza neno niligeuka na kuondoka. Sikuwa na haja ya kulia japo moyo uliniuma, nilijikaza mtoto wa kike na kurudi hadi nyumbani.
Nilipoingia ndani nilimkuta mama na mwanaume wa kizungu walikuwa wakinywa pombe kali, aliponiona alinyanyuka ili anikumbatie.
"Wawooo..my Babiiii."
Aliponisogelea ili anikumbatie nilimsukuma na kuanguka chini, sikutaka kumuangalia nilikimbilia chumbani kwangu huku nikilia.

Nini kitaendelea?
 
HADITHI: Msafara wa Mamba
SEHEMU: 05
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500
...ILIPOISHIA:
Maneno ya Anko niliona sasa yanaelekea kunisimanga, sikutaka kuongeza neno niligeuka na kuondoka. Sikuwa na haja ya kulia japo moyo uliniuma, nilijikaza mtoto wa kike na kurudi hadi nyumbani.
Nilipoingia ndani nilimkuta mama na mwanaume wa kizungu walikuwa wakinywa pombe kali, aliponiona alinyanyuka ili anikumbatie.
"Wawooo..my Babiiii."
Aliponisogelea ili anikumbatie nilimsukuma na kuanguka chini, sikutaka kumuangalia nilikimbilia chumbani kwangu huku nikilia.
SASA ENDELEA…

Mama alinifuata na kuniuliza nalia nini, nilimweleza upuuzi wake wote alioufanya kwa mjomba.
“Najua amekujaza maneno ya uongo, lakini nataka nikupe habari njema mwanangu.”
“Habari gani?” nilimuuliza mama huku nikimtazama macho yaliyojaa machozi.
“Umemuona yule mgeni?”
“Ndiyo mama.”
“Basi yule ni rafiki yangu wa siku nyingi alikuwa amekwenda kwao Ulaya lakini amerudi na kunitafuta na kuniulizia maendeleo yako. Nilimweleza uchungu wako katika elimu, ameahidi kukusomesha mpaka Ulaya.”
“Mama huyu ndiye mwanaume wako wa mwisho au bado una tamaa za mwili?” japo swali lilionesha kukosa adabu lakini ilikuwa lazima nimuulize.
“Kwa nini unaniuliza hivyo?”
“Anaweza kuwa na nia njema lakini akamtibua kama Anko wa benki.”
“Mwanangu nimechoka kukutia jaka moyo, sasa hivi natulia ili mwanangu nawe upumzike.”
“Mmh! Sawa.”
“Basi njoo umsamilie Anko wako.”
Nilifuta machozi na kutoka hadi sebuleni alipokuwa amekaa Anko mzungu akinywa pombe kali. Alionekana mtu mwenye maono ya mbali kwa jinsi alivyoniuliza na ahadi alizotoa.
“Anko nitashukuru sana.”
“Ni bidii yako tu nikuhakikishia kuyabadili maisha yako ili ije umsaidie mama yako, mama yako kanipa sifa zako hivyo itakuwa kazi nyepesi kukufikisha unapotaka na zaidi.”
“Nitashukuru sana Anko.”
“Jione mwenye bahati katika maisha yako, na kesho tunaanza mipango ya paspoti ili ukimaliza elimu ya sekondari ukasomee chuo Ulaya nchi utakayoichagua na chuo unachokitaka.”
Kwa kweli ilikuwa surprise kubwa kwangu baada ya Anko wa benki kujitoa kunisaidia kwa ajili ya maneno ya mama. Kilichoniumiza moyo ilikuwa tabia ya mama ya kutoridhika na mwanaume mmoja. Niliapa kupambana ili kuibadili tabia yake japo tabia ya mtu ni kama ngozi kuibadili ni kazi kubwa.
Anko mzungu siku ile alilala pale nyumbani huku akiniahidi kumaliza matatizo yaliyokuwa yakitutatiza. Mama alipewa pesa nyingi mbele yangu kwa ajili ya masomo yangu na kumshukuru Mungu kumrudisha mwokozi.
Siku ya pili ilikuwa wiki endi hivyo sikwenda shule, baada ya kufungua kinywa, mama na Anko mzungu walikwenda mjini na kuniacha nyumbani peke yangu nikicheza gemu kwenye laptop ya Anko.
Majira ya mchana Anko mzungu alirudi peke yake nilipomuuliza mama yupo wapi alisema alienda kushughulikia masuala yangu ya paspoti yangu. Baada ya kupumzika alikwenda kwenye friji na kutoa pombe kali na kusogea karibu yangu kwenye kochi na kuanza kunywa.
“ Herena unatumia pombe?”
“Hapana Anko.”
“Hata kidogo.”
“Ndiyo Anko.”
“Jaribu kidogo.”
“Hapana Anko sipendi pombe na nimeapa kutokunywa katika maisha yangu.”
“Mmh! Sawa, basi kachukue juisi kwenye friji ili kila mtu awe na kinywaji.”
Sikutaka kubishana na Anko nilikwenda kwenye friji na kuchukua juisi na kuiweka kwenye glasi na kurudi kuendelea kucheza game.
Nakumbuka kuna kipindi nilikwenda msalani niliporudi niliendelea kucheza game huku nikinywa juisi yangu. Lakini ghafla macho yalianza kupoteza nguvu kama mlevi na Anko alinibeba kunipeleka ndani, baada ya hapo kilichoendelea sikujua.
Nilishtuka usingizini na kujikuta kitandani kwangu, nilijinyanyua kitandani huku kichwa kikiwa kizito, nilipojiangalia nilishtuka kujiona nimeingiliwa kimwili uonesha nimebakwa. Sikuamini hali ile linyanyuka kitandani mwili wote nikihisi maumivu makali.
Nilitoka hadi sebuleni na kuwakuta mama na hawara yake wakiwa wamekumbatiana katika mapenzi mazito. Nilisimama na kuwaangalia kwa muda na kushindwa kuelewa aliyenibaka alikuwa ni yule mzungu au nani.
Nilisimama niliwaangalia huku machozi yakinitoka kwa uchungu, wa kwanza kuniona alikuwa ni hawara ya mama, alinyanyuka na kunifuata nilipokuwa nimesimama na kunivutia kifuani kwake na kuniuliza kwa sauti ya chini.
"Vipi Helena una tatizo gani?"
Sikumjibu nilijitoa mikononi mwake na kurudi nyuma, alipotaka kunisogelea nilimsukuma. Mama alishtuliwa na hali ile na kutaka kujua kwa nini nimekuwa kwenye hali ile. Alinifuata nilipokuwa nimesimama na kutaka kujua kwa nini nipo kwenye hali ile.
"Helana mwanangu mbona kila siku huishi vituko, haya tena una nini?"
"Mama uliyoyataka yamekuwa," nilimjibu mama huku nikilia.
Mama alishtuka na kutaka kunishika, lakini niligeuka na kuelekea chumbani kwangu. Mama alinifuata nyuma hadi chumbani kwangu, nilipofika nilijitupa kitandani na kuanza kulia. Mama alinisogelea ili kujua nina tatizo gani?.
Nilimuelezea mama hali niliyojikuta nayo muda mfupi baada ya kuamka, nilimuonyesha mama hali nilijikutanayo baada ya kuamka, mama hakuamini na kutaka kipi kilichonifanya nilale wakati aliniacha nikijisomea.
Sikumficha nilimweleza jinsi ba mdogo alivyonishawishi kunywa pombe lakini nilikataa na kunywa juisi na baadaye kupoteza kumbukumbu na kujikuta nimelala na nilipozinduka ndipo nilipokuta nimeingiliwa kimwili.
Baada ya maelezo yale na kuona mwenyewe kwa macho yake nilimuona mama akiinama kisha alikuna kichwa na kuniuliza.
"Helena mwanangu unataka kuniambia baada ya kuondoka Anko wako alirudi peke yake?"
"Ndiyo mama, hata mimi nilishangaa lakini sikuwa nalakuhoji."
"Mmh! Sawa, basi leo atanitambua na uzungu wake, pesa zake zisiwe kigezo cha kunibakia mwanangu."
Mama aliyekuwa amekunywa kidogo nilimuona pombe zikimtoka na kujifunga kanga kama anakwenda kucheza mdundiko. Alitoka kama Faru, nami nilimfuata nyuma ili nione mama anataka kufanya nini.
Mama alikwenda hadi alipokuwepo yule mzungu aliyekuwa akiendelea kunywa pombe taratibu. Mama alipofika alimsimamia mbele yule mzungu huku ameshikilia chupa ya pombe kali mkononi.
"Mr Hans amemfanyaje mwanangu?"
"Ooh taratibu, kwani vipi" alijibu yule mzungu huku akinyanyuka kitini kumfuata mama.
"Mr Hans sihitaji kusogelewa ila nataka jibu umemfanyaje mwanangu?" Mama alikuwa mkali na nywele zilimsimama kwa hasira.
Yule mzungu alionesha kutoshtuka na kauli ya mama aliendelea kumsogelea pamoja na kupigwa stop ya kumfuata.
Nilishtushwa na mlio wa chupa kupasuka kwenye kichwa cha mzungu, alikuwa mama aliyempiga chupa iliyompasua vibaya, mzungu alipiga kelele za maumivu.
"Unaniua mama Herena."
"Kufa shetani mkubwa wee," mama kwa hasira alichukua chupa nyingine ya pombe iliyokuwa juu ya meza ili amuyongeze mzungu aliyekuwa ameanguika chini, lakini nilimuwahi ili asimuumize zaidi.
"Mama basi utamuua."
"Wacha afe mshenzi hawezi kunichezea mimi na mwanangu, kwanza kwa kipi hasa?" Mama alikuwa amepandisha hasira.

Nini kitaendelea?
 
Nyie watuzi bana mnachekesha utam utam halafu unakata manaake nn ss mkiaza mjue na kumaliza Nana
 
SEHEMU: 06
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500
ILIPOISHIA:
"Kufa shetani mkubwa wee," mama kwa hasira alichukua chupa nyingine ya pombe iliyokuwa juu ya meza ili amuyongeze mzungu aliyekuwa ameanguika chini, lakini nilimuwahi ili asimuumize zaidi.
"Mama basi utamuua."
"Wacha afe mshenzi hawezi kunichezea mimi na mwanangu, kwanza kwa kipi hasa?" Mama alikuwa amepandisha hasira.
"Mama tupige simu polisi," nilimshauri.
"Tena kweli na lazima afie gerezani."
Mama alipiga simu polisi baada ya muda polisi walifika na kumchukua yule mzungu na kumfungulia kosa la kubaka.
SASA ENDELEA…
******
Baada ya kuvunja mahusiano na mzungu, mama aliamua kuachana na wanaume na kuendelea na biashara zetu. Pamoja na kutokuwa na mtu wa kutufadhiri hali ya kimaisha haikuwa mbaya, vilevile nilimshukuru Mungu mama yangu kutulia na kuachana na wanaume.
Maisha yalikuwa mazuri tuliweza kufurahia maisha bila kuwa tegemezi, nami niliendelea kusoma bila tatizo lolote, mama aliyatamani yale maisha tungeishi tokea awali. Kwa kweli mama yangu alipendeza na kurudisha heshima iliyopotea.
Mwaka mmoja baadaye mama alianza kusumbuliwa na maradhi yasiyoeleweka, Mara leo kichwa kesho miguu kukosa hamu ya kula, ile hali nilimshauri mama twende hospitali. Lakini mama alikataa kwa kusema.
"Herena mwanangu wanadamu siwema, lazima wameniroga kutokana na maisha yetu kuonesha maendeleo."
"Sawa mama, lakini twende hospitali kwanza."
"Hapana twende kwa mganga, nina mganga wangu mmoja lazima atanieleza ukweli."
Basi sikuwa na jinsi nilikubaliana na mama kwenda kwa mtaalamu wa miti shamba. Tulipokwenda mama alipewa dawa nyingi za kunywa na kuoga, japo hali ya mama ilikuwa na unafuu kidogo lakini haikumuwezesha kufanya kazi zaidi ya kushinda ndani.
Matibabu ya mama yalikula pesa nyingi, tulijikuta tukiyumba kiuwezo na kufikia hatua ya duka kufilisika na mimi pesa zote benki kukatika. Utafikili labda ulisubiri pesa zituishie ndipo ugonjwa wa mama uzidi.
Nilichanganyikiwa mtoto wa kike hali ya mama ilikuwa mbaya na pesa zilikuwa zimetuishia. Nilijiuliza niende wapi kuomba msaada, wazo lilikuja niende kwa mjomba wa benki nikamuelezee hali halisi ili anisaidie.
Siku ya pili nilikwenda hadi benki kwa mjomba, aliponiona alinikarisha kwa heshima zote, kitu kilichonipa moyo wa kusaidiwa.
"Herena za siku mbona umepotea sana?"
Ajabu badala ya kumjibu nilianza kububujikwa na machozi kitu kilichomshtua mjomba na kuhoji.
"Herena vipi mbona unanidondoshea machozi?"
Sikumjibu upesi niliendelea kuinama nikiendelea kudondosha machozi, Anko aliponiona simjibu na kuendelea kudondosha machozi alinyanyuka kwenye kiti chake na kuzunguka kunifuata nilipokuwa nimekaa.
"Herena kuna nini tena mbona unanitisha?" Aliniuliza huku akinikanda mabegani.
"Hali ya mama ni mbaya sana."
"Ooh pole sana, anasumbuliwa na nini?" Aliondoa mkono mabegani na kuzichezea nywele zangu chache.
"Hata sijui kila siku hali yake inazidi kubadilika."
"Mm’hu kumbe ndilo hilo, vipi hospitali mmekwenda?"
"Hataki anang’ang’ania kwa waganga wa kienyeji."
"Sasa alikuwa unahitaji nini kwangu?"
"Msaada Anko."
"Msaada upi huo?"
"Wa pesa."
"Mmh, Herena najua unaelewa ugumu wa maisha kwa sasa," alizungumza huku akizunguka meza na kurudi kwenye kiti chake.
"Ndiyo" nilijibu kwa kifupi.
"Unataka kuniambia nitamsaidia kivipi ikiwa hata familia yangu ina matatizo nayo inanitegemea mimi?"
"Anko kiasi chochote kila sio lazima kiwe kikubwa."
"Herenaaa, dunia hii ya leo pesa haitoki bure nina imani we mkubwa sasa una miaka mingapi?"
"Anko miaka yangu ya nini?"
"Herena hebu nijibu sihitaji swali."
" 19."
"Mmh, umekuwa mtu mzima una uwezo wa kumsaidia mama yako."
"Kumsaidia kivipi na kazi sina."
"Upo tayari kumsaidia mama yako?"
"Sijakuelewa kivipi?" Nilishindwa kumwelewa Anko.
"Ukipata kazi nyepesi yenye malipo makubwa."
"Nipo tayari kama nikiipata," alijibu bila kujua kazi hiyo.
"Ok, njoo leo saa mbili usiku pale ABC Hotel."
"Aah, Anko kama kazi ya hotel nitapata muda gani wa kusoma?"
"Herena mbona unakuwa si muelewa, nani amekwambia kazi ya hotelini."
"Sawa Anko nitakuja."
Nilinyanyuka ili niondoke nilipogeuka ili niondoke Anko aliniita.
"Herena."
"Abee Anko," niliitika huku nikigeuka kumwangalia.
Bila kusema kitu aliinama na kuvuta droo na kutoa pesa.
"Herena hizi zitakusaidia kwa matumizi ya leo na nauli, usikose sawa?"
"Sawa Anko Mungu akuzidishie," nilimshukuru Anko huku nikizipokea pesa ambazo sikuzihesabu.
"Atuzidishie sote."
Baada ya kuzipokea niligeuka na kuondoka huku moyoni nikimshukuru Anko kwa kuonesha utu japo maneno ya mama kuonekana kumchefua. Nilijikuta nikiionea wivu familia yake kwa kuwa na mzazi wenye ubinaadamu.
Nilipofika nje ya ofisi nilizihesabu zile pesa nilizopewa, sikuamini macho yangu pale nilipokuta laki mbili taslimu. Nilibadili wazo la kupanda daladala na kukodi bajaj, kwanza nilipitia sokoni na kununua mahitaji muhimu ambayo nyumbani hayakuwepo pamoja na dawa za mama zilizokuwa zimekwisha. Mahitahi yangu yote nilitumia elfu sitini.
Nilirudi nyumbani na kumweleza mama jinsi Anko alivyonisaidia na jinsi alivyodhamilia kunisaidia zaidi kwa ajili ya kazi ya muda mfupi na kupata pesa kidogo za kuweza kumsaidia. Nilimuona mama yangu akilia na kujuta kuachana na Anko na maneno machafu aliyomtolea.
"Herena mwanangu nikipata nguvu kidogo nitakwenda kumuomba msamaha."
"Ndicho kilichobaki, kwa jinsi ninavyomjua lazima atakusamehe."
Baada ya shughuli za siku nzima, nilifanya kazi zangu harakaharaka ili kuwahi miadi na Anko ABC saa mbili usiku. Majira ya saa moja baada ya kumuogesha mama na kumpatia chakula cha usiku nilimuaga mama ili nimuwahi Anko asije kukasirika.
Nilikodi bodaboda hadi ABC Hotel njia nzima nilikuwa najifikilia ni kazi gani hiyo mpaka tukutane hotelini. Lakini wazo lingine liliniambia huenda ni kunikutanisha na wakubwa wenzake ambao watanipa kazi kama mtoto wake, nilifuata maelekezo kama alivyonielezea.
Nilipokelewa na muhudumu na kunielekeza sehemu ya kumsubiri Anko. Aliniuliza natumia kinywaji gani, nilimjibu soda japo nilikuwa na hamu ya bia ya baridi.
Nikiwa pembeni ya ukumbi nikinywa soda yangu taratibu, nilishtushwa na mkono alionigusa begani nilipogeuka nilikutana na Anko.
Nini kitaendelea?
 
SEHEMU: 07
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500
ILIPOISHIA:
Nilipokelewa na muhudumu na kunielekeza sehemu ya kumsubiri Anko. Aliniuliza natumia kinywaji gani, nilimjibu soda japo nilikuwa na hamu ya bia ya baridi.
Nikiwa pembeni ya ukumbi nikinywa soda yangu taratibu, nilishtushwa na mkono alionigusa begani nilipogeuka nilikutana na Anko.
"Aaah kumbe Anko, karibu."
"Asante, Helena umenifurahisha sana kwa kwenda na wakati nina imani hata hiyo kazi utaifanya vizuri na kupata malipo manono."
"Nitashukuru Anko maana hali ni mbaya sana."
Anko alivuta kiti na kukaa karibu yangu, huku akinichanulia tabasamu aliniuliza.
"Vipi mama yako anaendeleaje?"
"Aaah kidogo hajambo japo bado."
"Nina imani mambo yatakuwa mazuri baada ya leo."
"Hata mimi ndilo ninalo liomba kila siku."
Anko aliagiza pombe kali na kuanza kunywa taratibu na mimi nilikunywa soda yangu taratibu huku nikiwa na shauku kujua ni kazi gani hiyo nyepesi yenye malipo manono.
"Herena mbona unakunywa soda? hujawahi kunywa pombe?"
"Mara moja moja sana."
"Ooh, usiniogope kunywa hii au unataka bia?"
"Kilimanjaro ya baridi."
Nililetewa kilimanjaro ya baridi na kunywa taratibu huku nikisubiri kuelekezwa hiyo kazi. Nilijikuta nakata bia ya tatu bila kusikia lolote, mara ililetwa nyama choma ambayo tuliishambulia wote.
Muda wote sikuwa na wasiwasi wowote kutokana nilivyokuwa na Anko. Nilijikuta nikichanganya vinywaji vikali na baridi, mwisho kilichoendelea sikujua. Niliposhtuka nilijikuta kitandani nimelala na pembeni yangu kulikuwa na mwanaume amelala.
Nilipojichunguza vizuri nilijikuta sina nguo yoyote zaidi ya shuka niliyojifunika. Nilijikuta nikipandwa na gadhabu na kujiuliza ina maana kazi nyepesi aliyonitafutia Anko ni ukahaba. Nilipeleka mkono sehemu za siri na kujikuta nimeingiliwa.
Roho iliniuma sikuamini kama kweli Anko ndiye aliyenipeleka kwenye kazi ile au aliniacha na mtu kunichukua kama msamalia mwema na kunigeuza kitoweo. Mtu aliyekuwa amelala pembeni yangu ambaye alionekana eneo la kifua lililokuwa limesheheni manyoya, alikuwa bado kwenye usingizi mzito tena akikoloma.
Nilijikuta napata wazo na kuchukua kitu chocho kilichokuwemo mule ndani nimpige nacho kwa kitendo cha kuniingilia bila idhini yangu.
Nilijinyanyua kitandani huku nikiwa na hasira kwa kitendo nilichotendewa na mtu ambaye alikuwa kwenye usingizi mzito.
Nilisimama na kuivuta ile shuka ili nifuate nguo zangu, sikuamini kukuta yule mwanaume aliyekuwa uchi wa mnyama ni Anko. Nilijikuta nguvu zikiniisha na kuhisi kizunguzungu na kuanguka chini kilichoendelea sikujua. Nilipozinduka nilijikuta nikiwa nimelazwa kitandani nikiwa na nguo zangu. Niliposhtuka nilimuona daktari akiwa amesimama pembeni yangu.
Nilijiuliza pale nimefikaje na kwa nini nipo kitandani ikionesha ni mgonjwa. Anko alikuwa amesimama pembeni akifuta jasho kwenye paji la uso, nilitulia tuli nikiwaangalia wote waliokuwemo mule chumbani.
Taratibu kumbukumbu zilinirudia na kujikuta nikianza kulia na kutaka kunyanyuka kitandani huku nikisema kwa uchungu
"Ankoooo.. kwanini Anko?"
Kabla ya kunijibu nilimuona akimpa ishara yule daktari atoke nje ya chumba naye alifanya hivyo. Chumbani tulibakia wawili tu, nilinyanyuka na kutaka kusimama lakini alinishika kifuani na kunirudisha kitandani.
"Herena hebu tulia."
"Hapana Anko kwa nini umenifanya hivi au kwa ajili ya umasikini wangu?"
"Hapana Herena nina malengo mazuri sana kwako."
"Anko..Anko..ya.a.ani huwezi kunisaidia hadi unitumie, ni unyama gani huu?" nilijikuta nikilia kwa uchungu na kukumbuka maisha ya tabu ya mama yangu ndiyo yaliyopelekea niwe kwenye hali ile."
"Usifikilie hivyo mimi siwezi kukutumia ila nataka uwe mke wangu mdogo."
"Anko ni uchafu gani huo yaani utembee na mama yangu halafu utembee na mimi? Hata siku moja."
"Sikiliza Herena usiwe mjinga mimi sina uhusiano wowote na wewe lakini nimekuwa nikikusaidia kwa kiasi kikubwa. Nina imani nikikuoa kabisa matatizo ya mama yako tutayatatua kwa kiasi kikubwa. Kama kutokea imeisha tokea, hivi mimi ni kiumbe gani nitakaye fanya kazi isiyo na malipo."
"Anko Mungu angekulipia."
"Herena unanichekesha, ni nani aliyekweenda kwa Mungu akarudi akasema amelipwa malipo kwa matendo yake mema. Siku malipo ya duniani ubakia duniani na ndio maana tunafanya kazi na kupata mshahara na hatusubuiri malipo ya kwa Mungu si tungekufa njaa.
“Sikiliza mipango yangu kwako ni ya muda mrefu toka mama yako alipokata mahusiano na mimi. Herena kilichotokea nina imani hutakijutia ila jione kiumbe mwenye bahati, hebu fikilia leo nakupa laki tano siku ya mwanzo wa mahusiano yetu nina imani huu ni ukurasa mpya wa ukombozi wa maisha yenu..Kamata hizi."
Alinipa burungutu la pesa na kunikabidhi mkononi, nilisita kuzipokea lakini alining'ang'ani
za. Nilijua yameisha tokea na hali ya mama ni mbaya na pa kukimbilia sina niliamua kuzipokea.
Baada ya kuzipokea nilifuta machozi kwa kwenda bafuni kunawa uso, niliporudi nilimkuta Anko akinisubiri na kuniambia.
"Herena nina imani jioni tutakutana hapa hapa, nina mpango wa kumpeleka hospitali mama yako kwa ghalama yoyote."
Nilijikuta nikijilamu kwa kumchukia Anko ambaye hakunipunguza kitu chochote hata nikiendelea naye bado nitabakia Herena yule yule. Vilevile tatizo la ukata na matibabu ya mama yatapata ufumbuzi. Nilimkubalia Anko kukutana naye jioni, tuliagana na kunipa elfu 50 za nauli ya kuja jioni. Jumla ya pesa alizonipa siku ile zilikuwa laki nane, yaani asubuhi ya jana laki mbili na nusu na usiku laki tano na nusu.
Nilirudi nyumbani na kumkuta mama akiwa amelala, sikutaka kumwamsha kwa vile nilikuwa nimeisha kula, nuilikwenda bafuni kuoga na kupanda kitandani. Asubuhi nilikutana na mama ambaye alitaka kujua hatma ya safari yangu.
Nilimdanganya mama kuwa mambo si mabaya ila nimetakiwa kurudi jioni ya siku ile. Nilimficha mama kuwa nimepata pesa, nilijua lazima atakuwa na wasiwasi na kutaka kujua pesa zote zile kwa kazi gani, nilizificha ndani kwa ajili ya kututatulia matatizo yetu.
***
Kuanzia siku ile nikawa nyumba ndogo ya Anko nikiwa nimemrithi mama yangu mzazi. Lakini ilikuwa siri kubwa ambayo mama hakuijua, na matibabu ya mama yalikuwa mazuri yaliyorudisha hali ya mama upya.
Kwa kweli maisha yalikuwa mazuri na Anko kukubali kutusaidia kwa kisingizio ananiona kama mwanaye wa kuzaa. Sikuwa na sababu ya kuacha kunihudumia kiumbe nisiye na hatia, mmh kumbe tulikuwa tunamla mama kisogo.
Shule niliendelea kama kawaida, sikuwa tena yule Herena msichana mbishi mwenye msimamo mkali kwa walimu wapenda ngono. Siku za nyuma nilikuwa nipo tayari kuadhibiwa na walimu niliowakataa kimapenzi. Lakini baada ya kujua faida ya mwili wangu wa kunisaidia kwenye matatizo, sikuwa tena mbishi, mwalimu alipotaka kuniadhibu bila kosa nilimuuliza tatizo nini, jibu aliniambia kwani sijui, basi nilimwambia anione kwa wakati wake.
Herena nilijikuta nikipoteza mwelekeo kwa kuwa mama huruma kwa kugawa mapenzi ovyo bila kuhofia hatari iliyopo mbele yangu.
********
Siku zilivyozidi kwenda nilijikuta hata hamu ya masomo inapotea na muda mwingi nilifikilia mapenzi hasa penzi la Anko. Nlijikuta nikiacha shule kwa sababu ya ugomvi wa kila siku na wanafunzi wenzangu juu ya kuchangia mabwana yaani walimu.
Kingine ni ile hali ya kuutoa mwili wangu bure kwa walimu na pindi nikataapo huambulia adhabu kali. Ajabu ilikuwa tofauti na awali nilipomueleza Anko juu ya uamuzi wangu wa kuacha shule, aliupokea kwa mikono miwili. Hakuonyesha kunijutia kwa uamuzi wangu mgumu, alinieleza kitu ambacho kwa kweli siku ile nilikufurahia sana kumbe...Anko alinieleza kuwa.
"Herena kusoma kote ni kwa ajili ya kupata pesa kama una mtu mwenye pesa kusoma kuna maana gani? Unakosa nini Helena muda si mrefu nitakamilisha jumba lako la kifahari pamoja na usafiri wa nguvu.
“ Wewe sasa hivi hutakiwi kuumiza akili yako bali kuituliza na kula raha ya maisha, au hujui wanaume tumeumbwa kuwatafutia wanawake. Herena maisha mazuri yanakusogelea kwani hujui kusoma?"
"Najua." nilimjibu huku nikimtazama usoni, wakati huo nilikuwa nimemlalia mapajani tukiwa juu ya kitanda ndani ya nyumba ya wageni.
"Kingereza unaongea kwa ufasaha sasa tatizo nini?"
"Hakuna mpenzi."
"Hapo ndipo ninapokupendea, unajua mama yako angekuwa kama wewe sasa hivi ningekuwa nimemjengea ghorofa lakini kwa vile ameichezea bahati nafasi hiyo ni yako. Kula raha mtoto wa kike umri bado unaruhusu."
Yalikuwa maneno yaliyonivimbisha kichwa na kujiona mimi ndiye mimi, ni mwanamke niliye bahatika kuliko wanawake wote. Baada ya kuacha shule kwa kweli sikuwa Herena yule uliyenizoea, muda mwingi niliutumia kujipodoa na kuvaa nguo za gharama.
Pamoja na kufanya upuuzi ule sikumuacha mbali mama yangu nilimpa kipa umbele katika kumshughulikia matibabu yake. Kwa kweli pesa haishindwi na kitu. Mama alijenga afya yake kwa mara nyingine, kwa kweli mama alinishukuru kwa kuyaokoa maisha yake.
Uamuzi wa kuacha shule nilipomweleza mama kwanza alikuja juu, lakini nilimueleza sababu za muhimu moja walimu kunitaka kwa nguvu kimapenzi na Anko kuamua nipumzike huku akinitafutia shule nyingine. Nilitengeneza uongo ambao mama aliukubali.
Kuanzia hapo hakuna aliyeulizia maisha yangu zaidi ya kila kukicha kuongeza huduma nyumbani. Siku moja mama aliniambia kitu ambacho kilinishtua.
"Mwanangu Herena siwezi kukuzuia kwenye matamanio ya mwili ni wazi kuna mtu ana mahusiano na wewe. Ninacho ogopa ni Anko wako kujua huenda akapunguza au kukata kabisa huduma zake.
“Hivyo basi sipendi tumuudhi kwa mara nyingine samahani ilizidi hugeuka kero. Pia mwanangu kama kweli huyo mwenzako anakupenda basi usikubali akugeuze gunia la mazoezi. Mlete hapa atambulike kisha muwe mke na mume naogopa mwanangu anaweza kukupa ujauzito na kukukimbia.
“Nitajisikia vibaya siku moja ukija kuishi maisha kama yangu, haya sio maisha ni maisha yasiothaminika katika jamii yetu. Pia mwanangu sipendi siku moja uingie kwenye msafara wa Mamba wakati wewe ni mjusi hata ukenge hujafikia."
"Una maana gani mama?"
"Mwanangu ugonjwa wa ukimwi ni mbaya ukikupata yataka ujasiri la sivyo unaweza kuyakatisha maisha yako kwa kuhofia aibu. Hivyo mwanangu chukua taadhari kabla ya hatari, nife unizike sio ufe uniache."
Mmh! Maneno ya mama yalikuwa mengi pia angejua huyo anayemzungumzia ni Anko sijui angesemaje. Ni kweli nilikuwa nimefanya makosa kutembea na mwanaume ambaye tayari ameisha tembea na mama yangu ambaye alikuwa sawa na baba yangu.
Lakini siku zote makosa ndiyo huzaa kosa, sikuwa na njia nyingine ya kunusuru uhai wa mama uliokuwa ukichungulia kaburi zaidi ya kujirahisi kwa Anko. Nilifanya siri kama tulivyo kubaliana na Anko kwa kuogopa domo la mama pale atakapojua tumeoga bwawa moja.
Hali ya mama ilitengamaa na kujikuta akirudi kilingeni kama kawaida, kwa kweli sikumchunguza ana fanya nini zaidi ya muda mwingi kujishughulisha na mambo yangu. Siku zilivyozidi kwenda ndivyo na mimi nilivyoondoa woga na kutembea na Anko popote alipotaka kwenda.
Safari zake nyingi za nje nilikwenda naye kama mkewe, huwezi kuamini nilinenepa na kupendeza hata mimi nililitambua hilo. Niliweza kuondoka na Anko na kwenda naye mikoani zaidi ya miezi miwili na kutumbua maisha. Kilichonifurahisha ni hali ya mama kuongezeka kuimalika na kuweza kufanya kazi zake kama zamani.
Mama naye baada ya kupata kurudi kwenye hali yake ya kawaida alirudia kazi yake ya ukahaba. Pamoja na kujua athari zake lakini moyo ulinisuta zaidi ya kumuacha afanye atakavyo. Ahadi ya Anko ilianza kukamilika pale aliponipeleka kwenye Site kunionesha ujenzi wa nyumba yangu.
Nilijikuta nikimshukuru Anko kwa kuonesha ananijali sikujutia uamuzi wangu wa kuchangia mwanaume mmoja na mama. Tokea hapo sikusikia ya mnadi swala msikitini au mgonga kengele kanisani. Siri siku zote ya mtu mmoja akizidi wa pili si siri tena.
Hilo sikuhofia kwa kujua hata mama aliipata nafasi kama ile na alijimwaga bila woga. Naikumbuka siku moja ambayo itakuwa vigumu kunitoka akilini na ndio mwanzo wa kuelewa nini nilichokuwa nikikifanya na kunipelekea kuandika walaka huu.
Nini kitaendelea?
 
Hadithi nzuri ila inasikitisha. Mambo kama haya yanatokea katika jamii
 
HADITHI: Msafara wa Mamba
SEHEMU: 08
MTUNZI: Ally Mbetu ‘DR AMBE’
SIMU: 0713646500
ILIPOISHIA:
Hilo sikuhofia kwa kujua hata mama aliipata nafasi kama ile na alijimwaga bila woga. Naikumbuka siku moja ambayo itakuwa vigumu kunitoka akilini na ndio mwanzo wa kuelewa nini nilichokuwa nikikifanya na kunipelekea kuandika walaka huu.
SASA ENDELEA…
Nina imani kila anaye soma asichukulie kama haditi tamu au kisa cha kusikitisha bali ni somo tosha maishani. Tatizo langu sipendi mtu mwingine limkute nitajisikia vibaya na kuona ujumbe wangu hukuwafikia walengwa. Elimu si darasani tu, la hasha elimu ni chochote kikutokeacho mbele yako chenye mafunzo kwa kuona au kusikia.
Ilikuwa siku ambayo iliniingiza dunia nyingine ambayo sikuitegemea kuuingia hata siku moja japo ndipo nilipokuwa nikielekea.
Ilikuwa ni siku ya jumamosi majira ya saa tatu usiku nakumbuka nilikuwa na wiki sijarudi nyumbani baada ya kuwekwa kwenye hoteli ya kifahari na Anko. Niliwasiliana na mama kwa njia ya simu na kunipa moyo kuwa hali yake ni mzima wa afya nje hofu kubwa ilikuwa kwangu.
Nilimtoa hofu kuwa yangu hali ilikuwa salama salimini, hakutaka kujua nipo wapi zaidi ya kuniombea dua niendelee kuwa salama. Siku hiyo baada ya kukaa upande wa baa na kunywa pombe ambazo nilimuona kama Anko zimemzidia. Nilimnyanyua ili nimrudishe chumbani.
Kwa kweli nilipata shida kumnyanyua na kuweza kumtembeza kwa shida, tulikwenda kwa shida sana huku tukiyumba kama gari umetatika senta bolti. Nilimtoa kwenye baa na kumpeleka kwenye vyumba vya kulala. Kutokana uzito nilimfikisha kwa shida hadi mlangoni na kuanza kufungua mlango kwa funguo.
Nilimzuia kwa mguu ili asiende chini na kujitahidi kufungua mlango.
Sauti ambaye haikuwa ngeni masikioni yangu lakini akili yangu haikukubali kama ni yenyewe iliniita nyuma yangu:
"Helena ni wewe?"
Niligeuka akili yangu asiamini ni kweli ile sauti ni ya mama yangu mzazi, haikuwa tofauti na mapokeo yangu kuwa ni kweli ni mama yangu mzazi mama Herana. Nilishindwa kumjibu haraka nilikuwa kama mwanga aliyeshikwa akiwanga mchana kweupe.
"Huyu nani?" aliniuliza ikionesha haamini macho yake.
"Anko."
"Imeanza lini? Helena mwanangu siamini nimekubali duniani hakuna kitu cha bure."
Mama alionekana amepagawa nina imani hakupenda nichangie mume mmoja na yeye. Wakati huo Anko alikuwa bado amelala chini sakafuni.
"Herena mwanangu kwa nini usiulize kabla ya kuingia kwenye msafara huu, mmh, kweli msafara wa Mamba haukosi kenge na mijusi. Siamini na sitaamini mpaka naingia kaburini kama mwanangu umeingia kwenye msafara wa Mamba usiokuhusu.
“Wasiwasi wangu umekuwa kweli, Herena kwa nini lakini umeingia kwenye msafara wa mamba?"
"Kwani mama tatizo nini, huyu si baba yangu mzazi pia mliisha achana na mwisho nilifanya hivi kuokoa maisha yako," nilimjibu mama huku nikijikaza kutokana na hali aliyoonesha mama yangu aliyekuwa akizungumza huku machozi yakimtoka.
"Herena huwezi kuniokoa huku akijiangamiza, nilikueleza mara ya mwisho kuwa sipendi uishi maisha yangu. Kwa nini mwanangu umechukua kila kitu kwangu, kwa nini hukutaka kuendelea na tabia yako ya awali ya msimamo leo hii umeingia kwenye msafara wa mamba.
“ Oooh! Mwanangu yaani leo nimesikia uchungu kama siku iliyokuleta duniani, uchungu huu ni wasiwasi kukupoteza duniani."
Maneno ya mama niliyaona kama uchuro, nilimweleza sehemu ile si muhimu muhimu ya kuyazungumza kwa kina ni nyumbani. Mama hata yule bwana aliyekuwa naye alimuacha na kuondoka huku akilia. Mwanaume aliyeongozana naye alibakia njia panda asijue nini kinaendelea. Nami nilitumia nafasi ile kumwingiza ndani Anko aliyekuwa hajitambui kwa pombe.
****
Siku ya pili niliporudi nyumbani nilimkuta mama macho yamemuiva na kuvimba kuonesha amelia kwa muda mrefu. Hali ile ilinitisha na kujiuliza kuna kingine kilichomliza mama yangu au ni kilekile cha kunikuta na Anko. Niliamini kikubwa kilichomuumiza ni kuchangia mwanaume mmoja na mwanaye.
Lakini kwa upande wangu sikuona kosa kwa vile Anko hakuwa baba yangu wa kunizaa pia alikuwa ameachana na mama. Kingine nilichokiamini kuwa nipo sawa kilitokana na msaada mkubwa wa Anko uliosababisha hali ya mama kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Mama kuna nini?” nilimuuliza mama.
“Ina maana hujui?”
“La kunikuta na Anko?”
“Mwanangu kwa nini unajiua ukiwa bado maisha hujayajua.”
“Kivipi mama?”
“Umeingia kwenye msafara ya mamba bila kujijua wakati wewe ni mjusi.”
“Kivipi?”
“Leo mwanaume ni muuaji asikuue kama mimi mama yako.”
“Lakini mama Anko ndiye aliyeshikilia maisha yetu baada ya wewe kuugua.”
“Kivipi?” mama alitaka kujua.
Ilibidi nimweleze sababu ya kuwa na Anko na sababu kubwa alikuwa yeye baada ya kumtukana mbele ya mkewe na kuamua kukata misaada.
“Mama kuwa na Anko sikupenda bali ilibidi nikubali ili kuokoa maisha yako bila hivyo ningekupoteza. Pia Anko amekuwa na malengo makubwa kwangu kwa vile hakutaka kunichezea ameninunulia gari na sasa hivi na muda si mrefu nitaingia katika jumba la kifahari.”
“Mmh!” mama hakuwa na la kusema aliinama wakati huo nilikuwa nimemsogelea kwa vile kitendo cha kutoa machozi kiliniumiza sana.
“Mama najua kiasi gani nimekukosea adabu ya kutembea na mwanaume uliyewahi kuwa naye ambaye sawa na baba yangu. Lakini mama sikuwa na jinsi kuuvua utu wangu kwa ajili ya maisha yako mama yangu. Mama wewe ni kila kitu kwangu kama nitakupoteza nitakuwa mgeni wa nani.
“Hivyo basi mama naomba unisamehe nipo chini ya miguu yako, sikuwa na nia mbaya zaidi ya kutafuta njia ya kukomboa hali yetu ya maisha kibaya zaidi hali yako mama ilikuwa mbaya sana ya kutishia amani ya moyo wangu.”
“Herena mwanangu nakujua vizuri jinsi ulivyokuwa na msimamo, najua Mr Joel ametumia mwanya huo kunichanganya na mwanangu. Kwa vile mna malengo siwezi kuingilia. Vipi mkikutana mnatumia mpira?”
“Mpira kivipi?”
“Kondomu.”
“Ndiyo mama si unajua siwezi kumuamini mpaka tupime kwa vile anataka mtoto,” nilimdanganya mama kwa kujua lazima angenilaumu sana kama ningemwambia ukweli.
“Kama hivyo afadhali,” mama alishusha pumzi ndefu kitu kilichonishtua na kuuliza.
“Mbona hivyo mama?”
“A’aa kawaida, ila usikubali kufanya naye mapenzi mpaka mwenye mkapime.”
“Sawa mama.”
Maneno yangu kidogo yalimfanya mama arudi kwenye hali yake ya kawaida, japokuwa jioni ya siku ile nilitakiwa kukutana na Anko nimuomba radhi ili niwe karibu na mama. Siku ya pili mama aliamka katika hali nzuri kitu kilichonipa nafasi ya kuweza kutoka.
Mchana Anko alinipigia simu kuwa ana safari ya nje ya mkoa hivyo alinitaka mapema kwa ajili ya mipango ya safari. Nilimuaga mama ambaye muda huo alionesha hana kinyongo tena.
Nini kitaendelea?
Endelea kufuatilia.
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni EquatorStory
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom