Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,760
Inatakiwa kila Mtanzania afahamu ya kuwa Chama Cha CCM kimeshindwa kuongoza nchi kwa uadilifu na Mwenyezi Mungu hamfichi mnafiki ,kama wewe ni muumini wa dini ufahamu wa msemo huo utaufahamu pengine zaidi yangu.
CCM au niseme miCCM ilikuwa inatudanganya kwa muda wa miaka mingi sana ,wakidai ni viongozi waadilifu na wanaongoza bila ya kujali dini au rangi na wote ni wasafi katika ngazi ya uongozi ,lakini Mwenyezi Mungu amewaumbua mchana kweupe,amewaweka uwanjani na kila mtu mwenye akili timamu ,itabidi apambanue na aone amependwa na kuwekewewa siri ya maneno matamu ya miccm mbele ya akili na macho na masikio yake aone apime na aamue.
Wewe kama una akili ikiwa umeshaonyeshwa ubaya wa dhulma iliyofanywa na viongozi wakuu katika Taifa hili halafu ikawa bado unawakumbatia na kuwasifu na kuwatetea ,adhabu kuu itapokuja ujue hutaachwa na itakupata wewe na kukuumiza zaidi kuliko shida zilizopo sasa. Chukua uamuzi wa uhakika kwa kuikataa CCM moja kwa moja na muhimu ni kuiepuka kabisa usishirikiane nao.
Inatakiwa ujue aibu hii ilioikumba CCM si uhodari wa mtu yeyote yule bali hizi ni baraka kwako wewe Mtanzania ,ujue kuwa wakati wa kubadili nguo umefika ,una uhuru mkuu na mpana kabisa wa kuchagua nguo nyengine ,iwe inakupendeza au haikupendezi lakini nguo mpya ni mpya.
Tumia kura yako kama wewe ni mpiga kura ubadilishe upepo ,tubadilishe upepo ,usiwe mjinga usie na uelewa na kufika kujitoa fahamu na kujivalisha fahamu za upumbavu wakati Taifa linaangamia.
Leo tumepata kuyajua yaliyonyuma ya pazia la Uccm si vyema ukarudi na kubaki hukohuko CCM kama vile lililotokea si lolote si chochote ,unatakiwa upime kwa vizuri na utulize bongo lako,Miccm imetawala tokea uhuru hadi leo hakuna asiejua nini watoto wa kimaskini wanvyosota kwenye dongo,wazazi wanavyopata matatizo mahospitali,shida zisizomalizika za umeme na maji kodi inapandishwa ,umefika wakati ukitumia usitumie inakujia bili nono ,kichwa kinazunguuka ukiiona na unaambiwa uilipe,makodi yasiyo na kichwa wala miguu tunafukuzana na maaskari wa kukusanya kodi kama tupo utumwani ,michango mikubwamikubwa ya kuisaidia serikali ,wale wanaosababisha sisi kutoa michango ndio hao hao wanaozigeukia kodi tunazozitoa na kuzila ,utawala gani huu wa uwongo na ulaghai wa maneno.
Kama wewe bado una kadi ya ccm basi ichane kama huwezi kuirudisha na kama huwezi kufanya yote basi irudishe kwenye kabati uisahau humohumo,
Na kama wewe ni kiongozi mzalendo iwe mbunge au kiongozi yeyote yule ndani ya CCM basi kikimbie hicho chama na jiunge na vyama vingine vyama vipo tele na nafasi nyingi za kujazwa ili uungane na wengine.
Kwa wapiga kura wawe wastahamilivu na wanapopiga kura basi wainyime ccm kura kwani kura ni siri wala usikubali kutishwa kuwa utajulikana ,hakuna mwenye uwezo wa kukujua na hata akikujua atakufanya nini ?
CCM au niseme miCCM ilikuwa inatudanganya kwa muda wa miaka mingi sana ,wakidai ni viongozi waadilifu na wanaongoza bila ya kujali dini au rangi na wote ni wasafi katika ngazi ya uongozi ,lakini Mwenyezi Mungu amewaumbua mchana kweupe,amewaweka uwanjani na kila mtu mwenye akili timamu ,itabidi apambanue na aone amependwa na kuwekewewa siri ya maneno matamu ya miccm mbele ya akili na macho na masikio yake aone apime na aamue.
Wewe kama una akili ikiwa umeshaonyeshwa ubaya wa dhulma iliyofanywa na viongozi wakuu katika Taifa hili halafu ikawa bado unawakumbatia na kuwasifu na kuwatetea ,adhabu kuu itapokuja ujue hutaachwa na itakupata wewe na kukuumiza zaidi kuliko shida zilizopo sasa. Chukua uamuzi wa uhakika kwa kuikataa CCM moja kwa moja na muhimu ni kuiepuka kabisa usishirikiane nao.
Inatakiwa ujue aibu hii ilioikumba CCM si uhodari wa mtu yeyote yule bali hizi ni baraka kwako wewe Mtanzania ,ujue kuwa wakati wa kubadili nguo umefika ,una uhuru mkuu na mpana kabisa wa kuchagua nguo nyengine ,iwe inakupendeza au haikupendezi lakini nguo mpya ni mpya.
Tumia kura yako kama wewe ni mpiga kura ubadilishe upepo ,tubadilishe upepo ,usiwe mjinga usie na uelewa na kufika kujitoa fahamu na kujivalisha fahamu za upumbavu wakati Taifa linaangamia.
Leo tumepata kuyajua yaliyonyuma ya pazia la Uccm si vyema ukarudi na kubaki hukohuko CCM kama vile lililotokea si lolote si chochote ,unatakiwa upime kwa vizuri na utulize bongo lako,Miccm imetawala tokea uhuru hadi leo hakuna asiejua nini watoto wa kimaskini wanvyosota kwenye dongo,wazazi wanavyopata matatizo mahospitali,shida zisizomalizika za umeme na maji kodi inapandishwa ,umefika wakati ukitumia usitumie inakujia bili nono ,kichwa kinazunguuka ukiiona na unaambiwa uilipe,makodi yasiyo na kichwa wala miguu tunafukuzana na maaskari wa kukusanya kodi kama tupo utumwani ,michango mikubwamikubwa ya kuisaidia serikali ,wale wanaosababisha sisi kutoa michango ndio hao hao wanaozigeukia kodi tunazozitoa na kuzila ,utawala gani huu wa uwongo na ulaghai wa maneno.
Kama wewe bado una kadi ya ccm basi ichane kama huwezi kuirudisha na kama huwezi kufanya yote basi irudishe kwenye kabati uisahau humohumo,
Na kama wewe ni kiongozi mzalendo iwe mbunge au kiongozi yeyote yule ndani ya CCM basi kikimbie hicho chama na jiunge na vyama vingine vyama vipo tele na nafasi nyingi za kujazwa ili uungane na wengine.
Kwa wapiga kura wawe wastahamilivu na wanapopiga kura basi wainyime ccm kura kwani kura ni siri wala usikubali kutishwa kuwa utajulikana ,hakuna mwenye uwezo wa kukujua na hata akikujua atakufanya nini ?