'Golden Chance' kwa Samwel Sitta

'Golden Chance' kwa Samwel Sitta

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Samwel Sitta amepata nafasi adimu. Jana,Samwel Sitta amenukuliwa akisema kuwa kuna viongozi waandamizi Serikalini waliofanya usanii wakati wa ujio wa Obama na kutafuna shilingi bilioni 8 za kitanzania.

Waandamizi hao walianzisha kampuni 'hewa' na kuzoa tenda zote zilizohusu yote yaliyozunguka ujio wa Obama na mkutano wa Partnership.Malalamiko ya Sitta yameshatua TAKUKURU ambao wamesema kuwa wameanza kufanya uchunguzi juu ya tuhuma hizo. Huu ni wakati wa Waziri Sitta kuachia madaraka na kupata heshima.

Ni wakati wa Sitta kujitoa Baraza la Mawaziri ili awe na muda mzuri wa kushirikiana na TAKUKURU na hatimaye mafisadi yafikishwe mbele ya sheria. Waziri Sitta asithubutu kupoteza nafasi hii adimu.Akijitoa kwa wanaolalamikiwa na kujiunga nasi tunaolalamika,ataaminika.Ataheshimika.

Atajiweka pazuri.La sivyo,Sitta atapotezwa na malalamiko yake yasiyokwisha. Atadharauliwa kama mtu 'wa kulia lia' tu. Hatabaki hata na chembe ya heshima za kulalamika. Waziri Sitta ataamua moja sasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
......

.................................anaweza kuvumilia njaa kweli?
 
Thubutu Mh.Mrema pekee ndiye alifanya hilo,Six hawezi
 
Sitta ni mfamaji, anatapatapa. Haiba yake kwa jamii ilikwishaporomoka.
 
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Samwel Sitta amepata nafasi adimu. Jana,Samwel Sitta amenukuliwa akisema kuwa kuna viongozi waandamizi Serikalini waliofanya usanii wakati wa ujio wa Obama na kutafuna shilingi bilioni 8 za kitanzania.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Hapo kwenye red, Hiyo kesi hata wakikutikana na kosa. Kutakuwa na tofauti gani na zile ambazo juzi tu hapa Kamanda mwenyewe alikuwa analalamika zimekaliwa na DPP naye asiweze hata kuwaweka wazi watuhumiwa wake?

Nadhani ni stori za bunuasi zitaendelea
 
Bwana six. Alishajipoteza kwenye siasa za bongo kwa UNAFIK wake.
Sita na pinda ni wale wale kasoro majina tu
 
Wanajanvi, tusiruhusu matashi yetu ya kisiasa yatuzuie kupiga kelele dhidi ya wizi huu wa kimacho macho. Sitta kalianzisha, tumuunge mkono.
 
Wanajanvi, tusiruhusu matashi yetu ya kisiasa yatuzuie kupiga kelele dhidi ya wizi huu wa kimacho macho. Sitta kalianzisha, tumuunge mkono.

Sawa tunaweza kumuunga mkono lakini baadaye akatugeuka,Mimi sidhani kama 6 ana dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi!!! Mbona ishu ya Richmond alitugeuka dakika za mwisho??!!!!!
 
Thubutu. Sitta?? Hawezi na hataweza kamwe. Sitta ni mwanasiasa MWOGA na MNAFIKI sana. Hafai kabisa kuaminiwa kwenye ulingo wa siasa.
'Golden Chances' nyingi alizipata na akashindwa kabisa kuzitumia.
 
Back
Top Bottom