GE2025 Gerson Msigwa: Wananchi mko salama, asiwatishe Mtu, hakuna mwenye mamlaka yakuzuia haki ya kuchagua au kuchaguliwa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema, "Wananchi asiwatishe Mtu yeyote, mko salama, Serikali na Vyombo vyake itafanya lolote linalowezekana kuhakikisha Watanzania hawabugudhiwi kupata haki yao ya kuchagua na kuchaguliwa"

"Tunafahamu hao wanaofanya Kampeni za kuvunja taratibu moja kati ya maeneo wanayotumia wanatisha watu hata wale ambao wameamua kuomba nafasi za kugombea, hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuzuia kupata haki yake ya Kikatiba"

Your browser is not able to display this video.
 
Too bad mabadiliko hayaji hivi hivi hadi watu waumie. Hatuko tayari kuumia kwa sasa.

Kama ukombozi hautaletwa na Wazalendo waliopo kwenye system tuna miaka mingine mingi ya kulia kilio cha kusaga meno.

Mungu ilinde Tanzania dhidi ya udhalimu.
Mungu ilinde Tanzania dhidi ya watu hawa.
Mungu wapige pigo takatifu wote watakaoshiriki October 29 kuhalalisha matendo ya kishetani yanayoendelea hapa nchini.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Na yeye pia atambue fika hana mamlaka ya kutulazimisha kumchagua mgombea tusiye mtaka.
 
Ukiona kila mtu anabwata ujue serikali imejawa na hofu
 
Wananchi wana haki pia ya kukaa nyumbani kutulia na kura zao. Kama wana haki ya kuchagua na kuchaguliwa wanayo haki pia ya kutokuchagua wala kuchaguliwa hawalazimishwi kuchagua.
 
Wananchi wana haki pia ya kutunza kura zao kama hakuna mgombea sahihi Gerson
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…