Gawio kwa wanahisawa NICOL

Gawio kwa wanahisawa NICOL

Joined
Aug 26, 2022
Posts
64
Reaction score
119
■ Kiasi cha gawio kilichoidhinishwa ni TZS 70 kwa kila hisa.
■ Jumla ya fedha zitakazolipwa kama gawio ni TZS 4.3 bilioni.
■ Hii ni sawa na 40% ya faida halisi ya NICOL kwa mwaka 2024.

✅ Ratiba ya gawio ni kama ifuatavyo:

》 Biashara ya hisa zitakazohesabiwa kwenye gawio (cum-dividend): Kuanzia 1 Septemba 2024 hadi 19 Septemba 2025
》 Biashara ya hisa bila gawio (ex-dividend): Kuanzia 22 Septemba 2025 —hisa zitakazonunuliwa baada ya hii tarehe hazitahesabika kwenye gawio la mwaka huu.
》 Kufungwa kwa daftari la wanahisa: 24 Septemba 2025.
》 Malipo ya gawio: Kuanzia 30 Septemba 2025.

Kama ni mwekezaji mpya wa NICOL na hujajaza form au unataka ku-update taarifa hakikisha unajaza Form.

Je wewe ni mmoja ya wanaopata gawio?
 
■ Kiasi cha gawio kilichoidhinishwa ni TZS 70 kwa kila hisa.
■ Jumla ya fedha zitakazolipwa kama gawio ni TZS 4.3 bilioni.
■ Hii ni sawa na 40% ya faida halisi ya NICOL kwa mwaka 2024.

✅ Ratiba ya gawio ni kama ifuatavyo:

》 Biashara ya hisa zitakazohesabiwa kwenye gawio (cum-dividend): Kuanzia 1 Septemba 2024 hadi 19 Septemba 2025
》 Biashara ya hisa bila gawio (ex-dividend): Kuanzia 22 Septemba 2025 —hisa zitakazonunuliwa baada ya hii tarehe hazitahesabika kwenye gawio la mwaka huu.
》 Kufungwa kwa daftari la wanahisa: 24 Septemba 2025.
》 Malipo ya gawio: Kuanzia 30 Septemba 2025.

Kama ni mwekezaji mpya wa NICOL na hujajaza form au unataka ku-update taarifa hakikisha unajaza Form.

Je wewe ni mmoja ya wanaopata gawio?
Nilijiunga na NICOL zamani sana nikapotelea huku Kigoma, sijawahi fuatilia chochote kuhusu uanachama wangu. Kunauwezekano wa Hisa zangu bado zipo?
 
Nilijiunga na NICOL zamani sana nikapotelea huku Kigoma, sijawahi fuatilia chochote kuhusu uanachama wangu. Kunauwezekano wa Hisa zangu bado zipo?
Hisa zako bado zipo - tafuta CDS number yako (utaipata kwenye cheti chako cha mwanahisi, natumaini utakuwa nacho kwa sababu huko nyuma walikuwa wanatoa vyeti ila kwa sasa kila kitu kipo Digital).

Ukipata CDS, wasiliana na DSE au broker yoyote upate access ya DSE hisa kiganjani na pia ujaze form ili upate magawio ya nyuma kama ulikuwa hujawahi kupata.
 
Hisa zako bado zipo - tafuta CDS number yako (utaipata kwenye cheti chako cha mwanahisi, natumaini utakuwa nacho kwa sababu huko nyuma walikuwa wanatoa vyeti ila kwa sasa kila kitu kipo Digital).

Ukipata CDS, wasiliana na DSE au broker yoyote upate access ya DSE hisa kiganjani na pia ujaze form ili upate magawio ya nyuma kama ulikuwa hujawahi kupata.
Yap, cheti ninacho.
Nitafanya.
 
Hisa zako bado zipo - tafuta CDS number yako (utaipata kwenye cheti chako cha mwanahisi, natumaini utakuwa nacho kwa sababu huko nyuma walikuwa wanatoa vyeti ila kwa sasa kila kitu kipo Digital).

Ukipata CDS, wasiliana na DSE au broker yoyote upate access ya DSE hisa kiganjani na pia ujaze form ili upate magawio ya nyuma kama ulikuwa hujawahi kupata.
Kama cheti kimepotea na CDS namba hukumbuki itakuwaje ?
 
Mwaka 2003 marehemu mama yangu,alitununulia hisa za NICOL mimi na dada yangu,

Chaa ajabu nilienda mwaka juzi 2023 nikakuta hakuna faida yoyote tokea tulivyowekewa na mama,na hatukuwahi kuchukua gawio lolote..
Nilivunjika moyo sitaki kusikia kabisa hili swala
 
Kuna utaratibu wa kufata, wasiliana na aliyekuwa broker wake au wasiliana na CSDR — muhimu zaidi fika ofisi za DSE wakupe maelekezo.
 
Back
Top Bottom