KERO Foleni isiyo ya lazima makutano ya Barabara ya taa za Ubungo Maziwa (Kigogo road na Barabara inayotokea EXTERNAL)Eneo linaitwa Shungashunga

KERO Foleni isiyo ya lazima makutano ya Barabara ya taa za Ubungo Maziwa (Kigogo road na Barabara inayotokea EXTERNAL)Eneo linaitwa Shungashunga

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Chukwu emeka

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2018
Posts
25,203
Reaction score
40,641
Habari wanaJF,

Kuna foleni isiyokuwa na ulazima kwenye eneo hilo,sababu kubwa ni Bandari kavu iliyowekwa siku za karibuni,iitwayo BRAVO, hawa BRAVO hawana eneo la kuegesha malori yao (PARKING) na hivyo wanapark malori yao Barabarani katika eneo ambalo linataa pia na kusababisha foleni bila sababu.

Nchi yetu hii unajiuliza hawa Manispaa ya Ubungo wakipita hapo hawaoni? Kwasababu pamoja na kuleta kero ya foleni,yale malori yanaharibu Barabara,TANROADS inamaana hawaoni na ofisi zao zipo karibu kabisa pale GEREJI.Au ndiyo mpaka Kiongozi apite Wananchi walalamike,na amri itolewe.Kwanini nchi yetu inaendeshwa kiholelaholela tu,kila sehemu mtu anaweza kufanya lolote,au ndiyo RUSHWA watu hawajali.

Kuweka Bandari kavu pale si jambo baya lakini kuifanya Barabara eneo la kuegesha Malori si sawa,ni kero kwa usafiri wa umma na binafsi,watu wanachelewa maeneo ya kazi bila sababu,na jioni watu wanachelewa kurudi majumbani.

Nchi yetu mambo mengi ukiyaona yanachosha sana,tunahitaji reforms kubwa sana maana kila eneo limeoza.

Mfungo mwema 🙏
 
Ile bara bara haina heka heka sana ndo maana unaona kama hawako serious nayo sana. Magari yanayotumia sana ile bara bara ni haya Mbezi Mnazi mmoja Via Maji chumvi.
 
Wakati mwingine ukifikiria kwa kina viwango vya ufikiri vya hawa watawala wetu unapata kuona kuwa kwa asilimia kubwa tunaongozwa na wagonjwa wa akili kama sio wendawazimu...na hii inatokana na teuzi kujuana na kulipana fadhila......kwa hiyo mteuliwa anaona kama kapata zawadi badala ya uwajibikaji!!!!!!

Kila nikipita pale najiuliza maswali kuwa inakuwaje mtu anaruhusiwa kuweka bandari kavu pale sehemu kama ile yenye ufinyu wa nafasi.....kwa kuwa inajulikana bandari kavu na maroli ni kama uji na mgonjwa!!!!!

Mwisho wa siku unapata kugundua kuwa watawala wetu hawahangaishwi na kero na matatizo ya WANAOWATAWALA unless yawe yanagusa maslahi yao!!!!

Hawawezi kuona kero kwa kuwa wao wakipita pale wanakuta barabara nyeupe
 
Ile bara bara haina heka heka sana ndo maana unaona kama hawako serious nayo sana. Magari yanayotumia sana ile bara bara ni haya Mbezi Mnazi mmoja Via Maji chumvi.
Nikweli lakini foleni isiyokuwa na ulazima na usumbufu
 
Wakati mwingine ukifikiria kwa kina viwango vya ufikiri vya hawa watawala wetu unapata kuona kuwa kwa asilimia kubwa tunaongozwa na wagonjwa wa akili kama sio wendawazimu...na hii inatokana na teuzi kujuana na kulipana fadhila......kwa hiyo mteuliwa anaona kama kapata zawadi badala ya uwajibikaji!!!!!!

Kila nikipita pale najiuliza maswali kuwa inakuwaje mtu anaruhusiwa kuweka bandari kavu pale sehemu kama ile yenye ufinyu wa nafasi.....kwa kuwa inajulikana bandari kavu na maroli ni kama uji na mgonjwa!!!!!

Mwisho wa siku unapata kugundua kuwa watawala wetu hawahangaishwi na kero na matatizo ya WANAOWATAWALA unless yawe yanagusa maslahi yao!!!!

Hawawezi kuona kero kwa kuwa wao wakipita pale wanakuta barabara nyeupe
Inasikitisha sana,mambo mengi ya hovyo kwenye maeneo mengi sana,mpaka unakosa majibu
 
Tumelazimika kupaki hapo, tuvumilieni tu. Foleni daslamu ni za ulazima 🐼
 
Yaan hapo ulivyopaelezea hata sijapaelewa kabisa ukiwa unatoka Gereji kabla haujafika external au ukiwa unaelekea Gereji kutoka external? Ni wapi hapo? Ulivyoelezea hapaeleweki yaan hujaelezea vizuri hata layman's wakuelewe unamaanisha nini
 
Inasikitisha sana,mambo mengi ya hovyo kwenye maeneo mengi sana,mpaka unakosa majibu
Barabara ya taa za Ubungo Maziwa (Kigogo road na Barabara inayotokea EXTERNAL)

Fafanua vizuri hapo Mkuu maana umekoroga kidogo hapo au weka sawa
 
Barabara ya taa za Ubungo Maziwa (Kigogo road na Barabara inayotokea EXTERNAL)

Fafanua vizuri hapo Mkuu maana umekoroga kidogo hapo au weka sawa
Ukitoka stand ya mkoa zamani pale kama unaelekea Mabibo,mbele kidogo unakutana na njia inayotokea EXTERNAL...kuna taa........hapohapo ndiyo kuna malori kibao yamepaki hapo barabarani.........kuna Bandari kavu pale inaitwa Bravo
 
Wakati mwingine ukifikiria kwa kina viwango vya ufikiri vya hawa watawala wetu unapata kuona kuwa kwa asilimia kubwa tunaongozwa na wagonjwa wa akili kama sio wendawazimu...na hii inatokana na teuzi kujuana na kulipana fadhila......kwa hiyo mteuliwa anaona kama kapata zawadi badala ya uwajibikaji!!!!!!

Kila nikipita pale najiuliza maswali kuwa inakuwaje mtu anaruhusiwa kuweka bandari kavu pale sehemu kama ile yenye ufinyu wa nafasi.....kwa kuwa inajulikana bandari kavu na maroli ni kama uji na mgonjwa!!!!!

Mwisho wa siku unapata kugundua kuwa watawala wetu hawahangaishwi na kero na matatizo ya WANAOWATAWALA unless yawe yanagusa maslahi yao!!!!

Hawawezi kuona kero kwa kuwa wao wakipita pale wanakuta barabara nyeupe
ni hatari sana --- na kwa bahati mbaya nchi hii ukiamua kutenga muda utaona kwamba wanafunzi wanakwenda shule kwa sababu ya ratiba . na hata hao waliopo maofisi nao wengi wanakwenda kazini kukamilisha ratiba kwa sababu wameshaajiriwa --- mambo ya problem solving hawataki kuyasikia
 
Back
Top Bottom