Taborian
Senior Member
- Jan 1, 2018
- 192
- 222
Binafsi ni mpenzi sana wa muziki wa dansi. Iwe ni dansi ya Tanzania au nje ya Tanzania. Muziki wa dansi asili yake ni Kongo. Hii inahusisha rhumba(dansi ya taratibu) na pia soukous(au sebene ikiitwa Chemko).
Tanzania kuna bendi kadhaa kama msondo, sikinde, diamond sound, twanga na fm academia. Lakini kwangu mimi Fm Academia ndiyo band bora kabisa ya muziki wa dansi. Hizi ni sababu zangu.
1. WATUNZI BORA.
Muziki wa dansi silaha yake kuu mojawapo ni Utunzi wa nyimbo. Fm academia ni bendi yenye tungo zenye watunzi bora sana. Tungo hizi zinagusa nafasi mbalimbali za maisha ya mwanadant. Mf KUHESHIMIANA WANADAMU(Vuta nikuvute, Binadamu), NAFASI YA MWANAMKE(Heshima kwa wanawake, moise katumbi). MAPENZI(Anna, jasmine), UVUMILIVU KATIKA NDOA(Sintosahau).
2. UPIGAJI VYOMBO BORA.
Soukous/sebene inahitaji wapiga vyombo bora sana. Hapa fm academia inao wapiga vyombo bora sana. Mf mpiga guitar la solo Elombe kichinja katika Album ya Vuta nkuvute. Hakika solo limecharazwa ipasavyo.
3. RAPU ZA UBORA WA JUU KABISA.
Hiki ni kionjo cha juu kabisa katika muziki wa dansi. Fm academia wako bora sana katika eneo hili. 'utamu wa vanila eeh utamu'... 'najiuliza hili swali eeh, muzungu na muafrika nani mchawi eeh, mzungu anapaa kwa ndege muafrika anapaa kwa ungo'.
Hizi pia ni baadhi ya sababu kwanini fm academia itasurvive hata bila ya Nyoshi.
Nawasilisha.
Tanzania kuna bendi kadhaa kama msondo, sikinde, diamond sound, twanga na fm academia. Lakini kwangu mimi Fm Academia ndiyo band bora kabisa ya muziki wa dansi. Hizi ni sababu zangu.
1. WATUNZI BORA.
Muziki wa dansi silaha yake kuu mojawapo ni Utunzi wa nyimbo. Fm academia ni bendi yenye tungo zenye watunzi bora sana. Tungo hizi zinagusa nafasi mbalimbali za maisha ya mwanadant. Mf KUHESHIMIANA WANADAMU(Vuta nikuvute, Binadamu), NAFASI YA MWANAMKE(Heshima kwa wanawake, moise katumbi). MAPENZI(Anna, jasmine), UVUMILIVU KATIKA NDOA(Sintosahau).
2. UPIGAJI VYOMBO BORA.
Soukous/sebene inahitaji wapiga vyombo bora sana. Hapa fm academia inao wapiga vyombo bora sana. Mf mpiga guitar la solo Elombe kichinja katika Album ya Vuta nkuvute. Hakika solo limecharazwa ipasavyo.
3. RAPU ZA UBORA WA JUU KABISA.
Hiki ni kionjo cha juu kabisa katika muziki wa dansi. Fm academia wako bora sana katika eneo hili. 'utamu wa vanila eeh utamu'... 'najiuliza hili swali eeh, muzungu na muafrika nani mchawi eeh, mzungu anapaa kwa ndege muafrika anapaa kwa ungo'.
Hizi pia ni baadhi ya sababu kwanini fm academia itasurvive hata bila ya Nyoshi.
Nawasilisha.