Mwanantogakulya
Senior Member
- Mar 18, 2025
- 130
- 118
Fisi wameua kondoo 21 huku wengine tisa hawajulikani walipo tukio ambalo limetokea mtaa wa Mahina katika Kata ya Somanda mjini Bariadi mkoani Simiyu.
Mageni Maduhu amesema kuwa tukio hilo limetokea jana April 1,2025 nyumbani kwake majira ya saa 5:00 usiku.
Anasema kuwa alisikia sauti za kundi la fisi wakilia nje ya nyumba yake na alipoamua kutoka nje na kuwakuta na walipomuaona wakakimbia na akaanza kuwakimbiza wakatokomea gizani.
Anasema kwa kuwa yeye ni mfugaji wa kondoo ilimlazimu kuingia katika zizi la kondoo ndipo alipogundua ya kuwa kondoo hao wamekufa huku wengine tisa hawajulikani hawapo hadi sasa.
Matukio ya fisi kuvamia makazi ya watu katika mkoa wa Simiyu yamekuwa yakiripotiwa ambayo yalisababisha vifo kwa watoto tisa katika wilaya za Maswa na Itilima huku zikiwepo taarifa kuwa wapo wananchi wanaomiliki fisi majumbani mwao.
Mageni Maduhu amesema kuwa tukio hilo limetokea jana April 1,2025 nyumbani kwake majira ya saa 5:00 usiku.
Anasema kuwa alisikia sauti za kundi la fisi wakilia nje ya nyumba yake na alipoamua kutoka nje na kuwakuta na walipomuaona wakakimbia na akaanza kuwakimbiza wakatokomea gizani.
Anasema kwa kuwa yeye ni mfugaji wa kondoo ilimlazimu kuingia katika zizi la kondoo ndipo alipogundua ya kuwa kondoo hao wamekufa huku wengine tisa hawajulikani hawapo hadi sasa.
Matukio ya fisi kuvamia makazi ya watu katika mkoa wa Simiyu yamekuwa yakiripotiwa ambayo yalisababisha vifo kwa watoto tisa katika wilaya za Maswa na Itilima huku zikiwepo taarifa kuwa wapo wananchi wanaomiliki fisi majumbani mwao.