Farsafa ya urusi kuhusu kutotegemea Marekani na Eu

Farsafa ya urusi kuhusu kutotegemea Marekani na Eu

mohamedidrisa789

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2015
Posts
5,571
Reaction score
23,671
Urusi imekuwa moja ya nchi katika dunia hii isiyotegemea mchango wa Marekani na Umoja wa ulaya(EU) katika katika maswala ya maisha.kutokana na upatikanaji wa madini mengi ya kila aina,warusi waliona ni njia sahihi ya kuwafanya wasiwe tegemezi kwenye sekta ya viwanda.waliweza kuzarisha viwanda vya kila aina ili kuepuka kutegemea bidhaa kutoka Marekani na EU.waliamua kuanzisha viwanda vikubwa vya kuunda magari kama vile AVTOVAZ,GAZ na KAMAZ .viwanda ivi kwa mwaka mzima uweza kuzalisha magari yasiyopungua 1,303,989 na pia vimeajiri wafanyakazi 600,000.
Pia waliamua kuanzisha viwanda vya kutengeneza treni ili sekta ya reli isiwe tegemezi,walifungua kampuni kubwa kubwa iliyoitwa TRASMASHHOLDING.kampuni hii ipo urusi na pia kuna branch ipo Ugeruman.
waliamua kuazisha viwanda vya kutengeneza meri ili sekta ya usafiri na usalama wa majini iwe rahisi,UNITED SHIPBUILD CORPORATION ni kampuni kubwa sana ya kutengeneza meri nchini urusi,na pia imeajiri wafanyakazi zaidi ya 100,000.
waliamua pia kutengeneza viwanda vya kuunda ndege ili sekta nzima ya usafiri isiwe tegemwzi kutoka nchi nyingine.viwanda kama SUKHOI,ILYUSHIN na TUPOLEV vilianzisha kwa maitaji ya watu wa urusi na mashirika wake.

pia waligundua kuwa kuna umuhimu wa kuanzisha viwanda vya kuunda mashine za migodini,mashine za ujenzi,mashine za kilimo na mashine zingine mzito.mashine katika sekta ya madini kiwanda kilitengenezwa na kikaitwa URALMASH,kazi yake kubwa ni kuunda mashine aina tofauti tofauti kama vile Blast furnace,Sintering machine,Rolling mills na Presses,pia utengeneza cranes.
ACGO-RM ni kiwanda kilichoanzishwa kwa ajiri ya kuunda mashine za kwenye kilimo
baada kuona kuwa sekta ya afya imekuwa na changamoto nyingi waliona ni wataki sahihi wa kuweka nguvu zao.walianzisha kiwanda cha kutengeneza mashine za hospitali kinachoitwa MEDEX achambo pia kina export mashine kwenda Canada,Kazakhstan,Ugerumani,USA,Israel,India,Latvia,Lithunia,kenya,ghana etc.pia walianzisha viwanda vya kuzalisha dawa.kampuni kama AKRIKHIN ambayo uzalisha zaidi ya dawa 200 tofauti tofauti,VEROPHARM ni moja ya kiwanda cha kuzalisha dawa,uzalisha dawa za chupa milioni 43 kwa mwaka mzima na pia uzalisha dawa za vidonge milioni 10 kwa mwaka mzima.uzalisha aina 300 tofauti tofauti za dawa.pia kuna viwanda vingine kama vile SOTEX,WERTEKS,GEROPHARM na VALENTA PHARM.

pia waliona ni muhimu kubolesha sekta ya mawasiliano,waliamua kuanzisha viwanda vya mawasiliano kama vile YOTA na HIGH SCREEN vyote viwili utengezeza simu za kawaida na smart phone.kampuni kama TEXET,GRESSO,MEGATON,MTS na SHRONICS nazo pia utengeneza vifaa vya simu.pia kuna kampuni zinazotengeneza vifaa vya Information technology(IT),security systerm na vifaa vya umeme.kampuni kama Ruselectronics yenyewe utengeneza vifaa vya kwenye minara,vifaa vya kuona sehemu yenye kiza(Night vision na pia solar systerm.kampuni ya LOMO yenyewe utengeneza vifaa kama vile Movie cameras,sound record for motion na lenses.Krasmogorsky zavod yenyewe utengeneza vifaa kama cameras,photosensitized materials,tasma na range finder.
waliamua kuanzisha kampuni inayoitwa VENTPROM ya kutengeneza vifaa kama heating equipment,refregeration,fentilation fans na contor systerm.

Itaendelea .....
 
Asee safi sana mleta uzi bila shaka kuna kitu cha kujifunza kwa nchi zetu hizi za ulimwengu wa tatu
 
european union wanategemea gas kutoka russia pipelina kutoka russia mpaka germany imepita Finland sweden denmark under water
 
Russia aiseeee, ndoo maana huwa hasiti kutoa maneno ya kibabe zidi ya NATO,,,,
 
Tuna maviwanda mazito ya ushonaji lakini tegemezi wa hadi underwear! Sijui ni poor management au tatizo nn.
 
Hii ndiyo ilikuwa akili ya Mwl. Nyerere tatizo akawa anawaongoza nywele ngumu waliorubuniwa na wazungu koko wa ulaya magharibi pamoja na USA mwisho tutakosa mwelekeo.

Mwenyezi Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya Hayati Mwl. JK Nyerere.
You lived as a blessing to Tanzania but, our fellow citizens betrayed you.
 
Sijaelewa hapo wanaeza amua wasinunue au wasizalishe wakati kudhalisha hutegemea mahitaji ya jamii
 
Back
Top Bottom