Kuna jambo moja ambalo nalo ni muhimu hasa kwa wale wenye uwezo. Unapo-design nyumba yako siku zote tilia maanani suala la security hasa hasa wezi na moto. 1. MOTO. Kwa kuwa nyumba nyingi zinawekwa milango na madirisha yenye vyuma, kufuli na vitasa vya kuzuia wezi kuingia kwa urahisi jaribu ku-design system ambayo haichukui muda mrefu kutoka ndani ya nyumba kama moto umezuka. 2. WEZI. Jaribu kujenga kitu kinachoitwa ''panic room''. Hiki ni chumba cha siri ambacho kinakuwa na mlango imara sana na matundu/system ya siri ya kuweza kuona sehemu nyingine ndani/nje ya nyumba. Mlango wake unatakiwa uwe imara kiasi ambacho hata kama wezi wamefanikiwa kuvunja na kuingia ndani lakini itawawia vigumu kuuvunja. Unapokimbilia ndani ya hiki chumba hakikisha una silaha na mawasiano. Matundu utayatumia kuwatungua wezi mmoja mmoja!Silaha kubwa ya kumshinda Adui ni uwe wakwanza Kumuona adui, Hivyo usilale kama mfu, mbinu zingene ni kama ulivyoeleza na zile zitazojitokeza wakati wa tukio.
Asante
Sishauri sana nyumba kuweka milango ya chuma ajili ya kuimarisha ulinzi..
Wakati mwingine ni hatari sana hasa ikitokea ajali ya moto,rejea ajali ya moto iliyotokea Mwanza ,mwaka 1995 ikihusisha nyumba mmoja maeneo ya Bugando iliyokuwa inamilikiwa na mhandisi wa Jiji la Mwanza wakati huo Manispaa..
Iliyopelekea kupoteza watu zaidi ya 9 wa familia husika ..
Kwa sasa suala la usalama ni vizuri kuweka kamera za usalama ili kuwabaini Majambazi na watu wowote wabaya.
AsntenKuna jambo moja ambalo nalo ni muhimu hasa kwa wale wenye uwezo. Unapo-design nyumba yako siku zote tilia maanani suala la security hasa hasa wezi na moto. 1. MOTO. Kwa kuwa nyumba nyingi zinawekwa milango na madirisha yenye vyuma, kufuli na vitasa vya kuzuia wezi kuingia kwa urahisi jaribu ku-design system ambayo haichukui muda mrefu kutoka ndani ya nyumba kama moto umezuka. 2. WEZI. Jaribu kujenga kitu kinachoitwa ''panic room''. Hiki ni chumba cha siri ambacho kinakuwa na mlango imara sana na matundu/system ya siri ya kuweza kuona sehemu nyingine ndani/nje ya nyumba. Mlango wake unatakiwa uwe imara kiasi ambacho hata kama wezi wamefanikiwa kuvunja na kuingia ndani lakini itawawia vigumu kuuvunja. Unapokimbilia ndani ya hiki chumba hakikisha una silaha na mawasiano. Matundu utayatumia kuwatungua wezi mmoja mmoja!
Teh teh teh utakuwa unaigiza Bongo MovieUkipigwa kidogo jifanye umezimia
Hivi namba ya polisi ya dharura ni ipi na inafanya kazi? Nikiwapigia watakuja on time?Tafadhali chukua dakika chache kupitia maoni haya
1. Majambazi kwa kawaida huanzisha mashambulizi yao kupitia mlango wa nyuma (kawaida milango ya jikoni) kwa sababu kwa kawaida hawaonekani. Weka milango mizuri jikoni kwako. Tumia "chuma cha kukatisha" ama "Kizuiawezi" nyuma ya milango ndani ya nyumba. Kama una funguo "Kizuiawezi," kamwe usiache ndani ya kufuli. Kama inawezekana, tumia kufuli kwa kuongeza. lengo ni kuleta ugumu kadiri inavyowezekana kwa wezi kuingia ndani ya nyumba na kukuongezea wewe muda wa kuwaita watu kwa msaada.
2. Unaposikia mtu anavunja mlango wako, kama huna unahakika kabisa vitendo vyako vitazuia kuingia ndani ya nyumba, usijaribu kuwa shujaa kwa kusukuma nyuma ya mlango (Wanaweza kukupiga risasi kupitia mlangoni), au kuweka vitu vizito kama jokofu au makochi (Wanapatwa na hasira zaidi na kama watafanikiwa kuingia ndani wanaweza kufanya ukatili vibaya mno).
3. Kama unalala bila nguo au na nguo kidogo, Vaa haraka mara tu uwasikiapo. Kwa wanawake hasa, usijaribu kubaki na nguo za kulalia. Vaa suruali na blauzi isiyovutia.
4. Iwapo umepiga simu kwa mtu kwa msaada, weka simu mbali nawe kama vile huitaki ili usijulikane kuwa umepiga simu.
5. Angalia sehemu ya kukatia umeme kwenye nyumba yako kisha zima umeme iwe giza nyumba yote (hii itawachanganya na kusababisha wakimbie.
6. Kama una bunduki, imesajiliwa au la, itumie lakini tu kama una unauhakika kuwa unaweza kuwasababishia madhara. Huu siyo muda wa kupiga risasi juu kuwatisha! Mauaji ya mvamizi katika eneo la nyumba yako wakati wa kujilinda mwenyewe na mali zako ni halali kisheria upande wa utetezi. Pia hata ukitumia silaha nyingine yoyoyte kama vile kisu.
7. Wakati Majambazi wamefanikiwa kuingia wape chochote wakitakacho. Usifiche chochote. Usijaribu kuwa Jasiri wala kujadiliana nao.
8. Usiwatazame moja kwa moja (au usiwafanye wajue kuwa unafanya hivyo). Kama unamfahamu yeyote kati yao usioneshe dalili zozote za kumtambua na wala usitaje jina lake. Hata hivyo kariri maumbile yoyote unaweza kusaidia na kutambulisha katika uchunguzi.
9.Wakati hatimaye wanaondoka katika nyumba yako usiwafukuzie ..
10. Kuwa mlinzi wa jirani yako kama utasikia uvunjaji katika nyumba zao, piga simu polisi kwa msaada.
11. Wakati Majambazi yanaingia kwenye eneo la nyumba yako, usiwashe taa yoyote katika chumba chako. Washa taa za nje lakini zima taa za ndani zote ili majambzi/wezi wasiweze kukuona.
Mbwa Walinzi wanakubalika sana majumbani kwa ajili ya kutoa taarifa mara kitu kigeni cha hatari kinapokuwa kwenye eneo.
Mwenye mawazo ya ziada anaweza kuongezea
Nyogeza,epuka kuweka karibu nguo zenu za ndani,yaani mwanaume na mwanamke,ili kuepuka kuchaganyana wakati wa uvamizi,na hii inawahusu sana wanaume waliozoea kuvaa kofia..Hapo kwenye kuvaa suruali ngumu na blauzi isiyovutia, naomba ufafanuzi
Hakuna haja ya ufafanuzi, wewe baki ulivyokuwa umelala halafu waingie ndani.rangi zote utaziona.Hapo kwenye kuvaa suruali ngumu na blauzi isiyovutia, naomba ufafanuzi
Wazo zuri ila inategemea na aina ya vitasa pia maana kuna vitasa vingine funguo inatakiwa iwepo kweny mlango ili mtu mwingine asiweze kuingiza funguo na kufungua akiwa njeUkifunga mlango hasa wa kitasa usiache ufunguo mlangoni. Huwa unatikiswa na kuanguka chni kisha unavutwa kwa nje na waya ikiwa mlango wako unaacha kamwanya kwa chini. Hapo utafunguliwa na wataingia kama kwao. Hoi ni kwa vibaka. Hutokea hasa kwenye nyumba ambazo hazina geti kabla ya mlango wa mbao.
Mwanasiasa mnyime tu kura yako, wengine wakimpa Shauri yao.Kwa sasa kuna majambazi wa kalamu.
Wanasiasa.
Hao wa kuvunja milango ni vibaka tu.
Hii imekaa vizuri ila majambazi ya siku hizi pamoja na kwamba mengi yanayokamatwa yana muonekano mzuri (wakiungwana) lakini yana roho mbaya kiasi kwamba yakikukosa yanaweza kuamua hata kuchoma nyumba tofauti na majambazi ya zamani yana sura nzito lakini yakishindwa kuingia yanasepa ama yakifanikiwa na ukaonesha ushirikiano hayakuigi hata panga (yatachukua yalichofuata na kuondoka zao)Kuna jambo moja ambalo nalo ni muhimu hasa kwa wale wenye uwezo. Unapo-design nyumba yako siku zote tilia maanani suala la security hasa hasa wezi na moto. 1. MOTO. Kwa kuwa nyumba nyingi zinawekwa milango na madirisha yenye vyuma, kufuli na vitasa vya kuzuia wezi kuingia kwa urahisi jaribu ku-design system ambayo haichukui muda mrefu kutoka ndani ya nyumba kama moto umezuka. 2. WEZI. Jaribu kujenga kitu kinachoitwa ''panic room''. Hiki ni chumba cha siri ambacho kinakuwa na mlango imara sana na matundu/system ya siri ya kuweza kuona sehemu nyingine ndani/nje ya nyumba. Mlango wake unatakiwa uwe imara kiasi ambacho hata kama wezi wamefanikiwa kuvunja na kuingia ndani lakini itawawia vigumu kuuvunja. Unapokimbilia ndani ya hiki chumba hakikisha una silaha na mawasiano. Matundu utayatumia kuwatungua wezi mmoja mmoja!
Kumnyima kura haisaidii..Mwanasiasa mnyime tu kura yako, wengine wakimpa Shauri yao.