Ahsante sana ndugu,yaani familia yako ina raha
Katika ulimwengu wa vyakula, inafahamika na kuaminika kuwa chakula ni dawa. Chakula unachokula leo ndicho kinachoamua hali yako ya kiafya kesho. Unaweza kuishi bila kuugua kama ukila vyakula vyote muhimu vinavyohitajika mwilini.
Leo nitakutajia orodha ya juisi zilizotengenezwa kwa matunda na mboga na fadia zake mwilini. Katika orodha hii, utaona kuna mchanganyiko wa matunda au mboga mbili hadi nne na kazi zake mwilini, zikitumika kama tiba au kinga ya magonjwa.
KAROTI, TANGAWIZI NA TUFAHA
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda hayo matatu huondoa sumu mwilini na kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili. Tufaha ndiyo apple kwa Kiingereza.
TUFAHA, TANGO NA FIGILI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya ni kinga dhidi ya saratani, huondoa lehemu (cholestrol) mwilini, husafisha tumbo na pia huondoa maumivu ya kichwa.
NYANYA, KAROTI NA TUFAHA
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya ngozi ya mwili mzima kuwa nyororo na huondoa harufu mbaya mdomoni.
TANGO CHUNGU,
View attachment 40769
TUFAHA NA TANGO LA KAWAIDA
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huondoa harufu mbaya mdomoni na hupunguza joto la mwili.
CHUNGWA, TANGAWIZI NA TANGO
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hungarisha rangi ya ngozi na kuifanya kuwa laini. Pia hupunguza joto la mwili. Kwa wale wenye matatizo ya kuwa na ngozi kavu, juisi hii itawasaidia sana.
NANASI, TUFAHA NA TIKITIMAJI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya kazi ya kuondoa chumvi nyingi mwilini, husafisha kibofu cha mkojo na figo. Juisi hii ni nzuri kwa wale wenye matatizo ya kibofu na figo au wanaotaka kujikinga na magonjwa hayo.
TUFAHA, TANGO NA KIWI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hungarisha rangi ya ngozi. Kiwi ni aina ya matunda ambayo hujulikana pia kama matunda-damu.
PEASI NA NDIZI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hurekebisha kiwango cha sukari katika damu. Inawafaa sana wagonjwa wa kisukari na inaweza kuwa sawa na kinga dhidi ya ugonjwa huo.
KAROTI, PEASI, TUFAHA NA EMBE
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huzuia athari ya sumu mwilini, hupunguza shinikizo la damu na kuondoa mlundikano wa uchafu mwilini.
MASEGA YA ASALI, ZABIBU, TIKITIMAJI NA MAZIWA
Juisi yenye mchanganyiko huu huwa na kiasi kikubwa cha Vitamin C na Vitamin B2 ambazo huimarisha chembechembe hai na kinga ya mwili.
PAPAI, NANASI NA MAZIWA
Juisi hii ina kiwango kikubwa cha Vitamin C, E na madini chuma. Huimarisha rangi ya ngozi na mfumo wa usagaji wa chakula tumboni.
View attachment 40770
NDIZI, NANASI NA MAZIWA
Juisi hii yenye kiasi kikubwa cha vitamini na virutubisho mbalimbali vyenye faida mwilini, huzuia tatizo la ukosefu wa choo.
Ili kupata faida hizo zilizoainishwa katika kundi la matunda hayo, usafi wa matunda yenyewe hauna budi kuzingatiwa wakati wa kutayarisha juisi yake. Vilevile hakikisha unatumia matunda yaliyoiva vizuri na uyatayarishe kwa kuzingatia kanuni ya mtu ni afya.
Unaweza kutumia mashine maalumu ya kukamulia matunda (blender) au kutumia njia ya asili ya kutwanga kwa kinu maalumu na kupata juisi hiyo. Kama utaongeza sukari, inashauriwa kuweka kiasi kidogo sana. Ni bora zaidi usipoweka sukari, kwa sababu matunda mengi yana sukari ya asili.
Asante Mkuu Ubarikiwe Kwa Jina la Mwenyeezi Mungu Muumba wa mbingu na Ardhi na vilivyomo ndani yake.Excellent.This is a very imformative and useful thread.Sio ngono,ngono, ngono na ujinga mwingine.Keep it up.
MziziMkavu;277859[URL="http://api.ning.com/files/KRg437MfHoy8TV4Dml010KR1l60M1hzzs5pJPSwOZGb2a7RzBf82w2yiRvFLOWireCFYKrLT9LuutAi8eX0IVSVLWHRv22lX/juices.jpg" said:[/URL]Katika ulimwengu wa vyakula, inafahamika na kuaminika kuwa chakula ni dawa. Chakula unachokula leo ndicho kinachoamua hali yako ya kiafya kesho. Unaweza kuishi bila kuugua kama ukila vyakula vyote muhimu vinavyohitajika mwilini.
Leo nitakutajia orodha ya juisi zilizotengenezwa kwa matunda na mboga na fadia zake mwilini. Katika orodha hii, utaona kuna mchanganyiko wa matunda au mboga mbili hadi nne na kazi zake mwilini, zikitumika kama tiba au kinga ya magonjwa.
KAROTI, TANGAWIZI NA TUFAHA
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda hayo matatu huondoa sumu mwilini na kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili. Tufaha ndiyo apple kwa Kiingereza.
TUFAHA, TANGO NA FIGILI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya ni kinga dhidi ya saratani, huondoa lehemu (cholestrol) mwilini, husafisha tumbo na pia huondoa maumivu ya kichwa.
NYANYA, KAROTI NA TUFAHA
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya ngozi ya mwili mzima kuwa nyororo na huondoa harufu mbaya mdomoni.
TANGO CHUNGU,
View attachment 40769
TUFAHA NA TANGO LA KAWAIDA
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huondoa harufu mbaya mdomoni na hupunguza joto la mwili.
CHUNGWA, TANGAWIZI NA TANGO
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hungarisha rangi ya ngozi na kuifanya kuwa laini. Pia hupunguza joto la mwili. Kwa wale wenye matatizo ya kuwa na ngozi kavu, juisi hii itawasaidia sana.
NANASI, TUFAHA NA TIKITIMAJI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hufanya kazi ya kuondoa chumvi nyingi mwilini, husafisha kibofu cha mkojo na figo. Juisi hii ni nzuri kwa wale wenye matatizo ya kibofu na figo au wanaotaka kujikinga na magonjwa hayo.
TUFAHA, TANGO NA KIWI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hungarisha rangi ya ngozi. Kiwi ni aina ya matunda ambayo hujulikana pia kama matunda-damu.
PEASI NA NDIZI
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya hurekebisha kiwango cha sukari katika damu. Inawafaa sana wagonjwa wa kisukari na inaweza kuwa sawa na kinga dhidi ya ugonjwa huo.
KAROTI, PEASI, TUFAHA NA EMBE
Juisi yenye mchanganyiko wa matunda haya huzuia athari ya sumu mwilini, hupunguza shinikizo la damu na kuondoa mlundikano wa uchafu mwilini.
MASEGA YA ASALI, ZABIBU, TIKITIMAJI NA MAZIWA
Juisi yenye mchanganyiko huu huwa na kiasi kikubwa cha Vitamin C na Vitamin B2 ambazo huimarisha chembechembe hai na kinga ya mwili.
PAPAI, NANASI NA MAZIWA
Juisi hii ina kiwango kikubwa cha Vitamin C, E na madini chuma. Huimarisha rangi ya ngozi na mfumo wa usagaji wa chakula tumboni.
View attachment 40770
NDIZI, NANASI NA MAZIWA
Juisi hii yenye kiasi kikubwa cha vitamini na virutubisho mbalimbali vyenye faida mwilini, huzuia tatizo la ukosefu wa choo.
Ili kupata faida hizo zilizoainishwa katika kundi la matunda hayo, usafi wa matunda yenyewe hauna budi kuzingatiwa wakati wa kutayarisha juisi yake. Vilevile hakikisha unatumia matunda yaliyoiva vizuri na uyatayarishe kwa kuzingatia kanuni ya mtu ni afya.
Unaweza kutumia mashine maalumu ya kukamulia matunda (blender) au kutumia njia ya asili ya kutwanga kwa kinu maalumu na kupata juisi hiyo. Kama utaongeza sukari, inashauriwa kuweka kiasi kidogo sana. Ni bora zaidi usipoweka sukari, kwa sababu matunda mengi yana sukari ya asili.
Huo mchanganyiko wa matunda unaweza kutia sukari kijiko kimoja kikubwa na maji kama glasi moja tu ili kuifanya iwe tamu au waweza kuachia bila ya kutia sukari itakuwa pia bora mkuu.Huo mchanganyiko wa matunda, unachanganya na maji na kuongeza sukari? au ni matunda pekeyake?
Tiba ya juisi kwa mwathirika wa Ukimwi |
Juicer, Kifaa cha kusagia matunda (Blender), karoti nne (kwa ajili ya kuongeza nguvu ya kinga mwilini na kuongeza kiwango cha CD4 kutokana na viini lishe vya beta carotene). Robo ya kiazi kinachofahamika kama beetroot (ili kuongezea nguvu maini na kuzuia uwezekano wa kuzalishwa vitu visivyohitajika mwilini kwani kiazi hicho kina kiini lishe kiitwacho betane). Kipande cha tangawizi (kwani ina madini ya selenium ambayo hupunguza kuongezeka kwa virusi mwilini. Pia huhamasisha kuzaliana kwa kinga zaidi mwilini). Kiasi kidogo cha binzari (turmeric- kwani ina madini ya curcumin yenye uwezo mkubwa wa kupambana na sumu na kuzuia kuongezeka kwa virusi. Binzari ni rafiki mkubwa wa maini). Kipande cha kitunguu chekundu (kina madini viini lishe maalumu aquercetin- vinavyoongezea uwezo wa kuponya wa Vitamini C, mpambanaji muhimu wa virusi vya Ukimwi huku pia kikiwa na allicins inayozuia kuwapo na magonjwa nyemelezi). Vipande vinne vya vitunguu swaumu (hivi huondoa sumu kwenye chembe hai zote mwilini. Ni silaha zenye nguvu za allicins, selenium na chembe hai nyingine muhimu kupambana na virusi). Majani nane ya spinach (Haya yana utajiri wa chlorines ambayo huongeza kinga mwilini na kupambana na maradhi. Pia yana SOD au Super Oxide Dismutase, sterols na sterolins. Madini haya huongeza CD8 pamoja na CD3). 1. Vioshe vyema vitu hivi. 2. Osha mbogamboga vizuri kwa maji safi. 3. Weka mbogamboga hizo kwenye bakuli lisilopitisha hewa. 4. Tia maji safi ya kunywa hadi yafunike mbogamboga hizo. 5. Koroga na funika haraka kwa mfuniko thabiti. 6. Baada ya dakika tano ondoa kifuniko, toa maji na kamua mbogamboga kupata juisi yake. JINSI YA KUTENGENEZA 1. Weka juisi hiyo kwenye blender kisha ongeza: a) Vijiko viwili vya unga wa karanga za Brazil. Karanga hizo zina asili ya utajiri mkubwa wa selenium miongoni mwa vyakula vingi vikavu. Selenium huzuia kuongezeka kwa virusi na husaidia kuponya mgonjwa. (Vyakula vingine vyenye selenium ya kutosha ni mbegu za alizeti, samaki, maini na nyama ya nguruwe (bacon). Hivi unaweza kuvila tofauti kwani haviwezi kusagwa pamoja na juisi) b) Parachichi nusu. 2. Saga mara moja. Usitunze kwenye jokofu. Nyongeza: i. Kunywa juisi hiyo walau mara mbili kwa siku wakati tumbo likiwa halina kitu. Kadri ya kiwango utakachotumia ndivyo utakavyopata nafuu ii. Kama inawezekana pia kunywa juisi halisi ya nanasi kila siku kusaidia tiba hiyo ya maji ya matunda (juice therapy). Nanasi lina madini ya bromelain yenye uwezo mkubwa wa kupambana na virusi. iii. Juisi ya tikiti nayo ni nzuri kwa mgonjwa wa Ukimwi. Hii ni kwa sababu matikiti yana virutubisho viitwavyo glutathiones vinavyozuia kuongezeka kwa virusi. 3. Furahia maisha huku ukiusaidia mwili wako kupambana na wavamizi (virusi vya Ukimwi)! |
Asante Mkuu Ubarikiwe Kwa Jina la Mwenyeezi Mungu Muumba wa mbingu na Ardhi na vilivyomo ndani yake.oa
Dawaya kutibu ugonjwa wa kisukari ninayo ukiweza kunitafuta bonyeza hapa.MawasilianoShukuran bosi. Je unaweza nipa msaada kwa mtu mwenye kisukari atumie nini ili apone?
Shukurani
TUFAHA ni tunda gani? umeniacha mkuu!!
Tunda la Tufaha ni Tunda la Apple Tufaha ni neno la kiarabu.TUFAHA ni tunda gani? umeniacha mkuu!!