Edward Lowassa ni kipimo cha uadilifu ndani ya CCM

Edward Lowassa ni kipimo cha uadilifu ndani ya CCM

Miimo

Senior Member
Joined
Apr 7, 2012
Posts
106
Reaction score
49
JF

Leo ilikua siku kubwa sana kwa Mweshimiwa Edward, kutangaza nia. Kwa wale mnao mjua vizuri pamoja na rafiki zake tutakubaliana na jinzi pesa ilivyo na nguvu ya kuwatia upofu watu wasio weza hata kutafakari mbele kwa mita hata kumi.

nguvu kubwa iliyotumika kuandaa mkutano wa kutangaza nia inazihirisha hali halisi ya Mweshimiwa kuutaka uraisi kwa njia yeyote ile. Watanzani lazima mjue kuwa Ikulu si pango la wezi.

Kila rahia ana haki ya kutangaza nia ya kuwa kiongozi, kwangu mie ni mtihani mkubwa uliobaki kwa CCM kufanya maamuazi ambayo yatakua kipimo sahihi kujua kama chama ni cha mafisadi au cha wafanyakazi na masikini wakulima. Itashangaza sana endapo umakini wa chama utaamua bendera kufuata upepo kwa kuaangalia tu kukubalika kwa mtu bila kujali uadilifu na uwezo wa mgombea. Kwetu sisi tunahamu sana kusikia hatima ya mgombea wa CCM ili tuone kama mafisadi wameamuamua kumeza walio wengi wadilifu ndani ya chama chetu.

Ni lazima turuhusu bongo zetu zifanye kazi na wala tusifanye maamuzi kutokana na misukumo ya hisia au ya kutengenezewa mazingira ya kuaminisha umma kuwa fulani ndio chaguo bora.

Nawasilisha
 
Huyu jamaa anakubalika tu kwa hao wanaomlia hela zake,analazimisha kukubalika kwakutumia pesa,ingia mitaani uone kama anakubalika,kila mtu mitaani anajua gharama za maisha kupanda nchi hii ni kwasababu ya mafisadi na mmoja wao ni lowasa.
 
Hii nchi ni ya ajabu. Watu wake sielewi wameazima vichwa wapi? Lakini tusishangae sana. Tanzania ni taifa la itikadi ya wingi (quanity) na sio Ubora(quality)! Angalia kwetu msomi ni mtu mwenye shahada na vyeti vingi. Kielelezo cha kukua kwa uchumi ni wingi wa magari na foleni zake barabarani. Kwenye familia: harusi nzuri ni ile iliyoandaliwa kwa gharama kubwa ikiambatana na kurushwa na TBC katika kipindi cha Chereko Chereko.

Kwa hiyo hata katika suala la uongozi wa nchi watu wanaangalia nani kajaza watu na si ana hoja gani katika hilo kusanyiko! Maskini Tanzania!
 
Mimi sijui kwanini great thinkers wanajadili mtu wakati mikakati ya sisiem ni kuendeleza mfumo na siyo mtu!! Mzee Kingunge anajua wazi kuwa Lowasa akishibda maslahi ya wote walioiba fedha za walalahoi yatalindwa! hivyo wajinga waliounga mkono Mhe Lowasa jijinj ar lei nj kutokana na ujinga tu! Huwezj kumkubali Lowasa halafu ukaichukia sisiem! Lowasa hataongoza mwenyewe lazima arejeshe mafisadi katika serikali yake kwa kisingizio cha kuendeleza uzoefu!!! Yoooote kwangu ni batili! Kuliko sisiem afadhali jk aendelee tu kwani hakuna jipya
Hii nchi ni ya ajabu. Watu wake sielewi wameazima vichwa wapi? Lakini tusishangae sana. Tanzania ni taifa la itikadi ya wingi (quanity) na sio Ubora(quality)! Angalia kwetu msomi ni mtu mwenye shahada na vyeti vingi. Kielelezo cha kukua kwa uchumi ni wingi wa magari na foleni zake barabarani. Kwenye familia: harusi nzuri ni ile iliyoandaliwa kwa gharama kubwa ikiambatana na kurushwa na TBC katika kipindi cha Chereko Chereko.

Kwa hiyo hata katika suala la uongozi wa nchi watu wanaangalia nani kajaza watu na si ana hoja gani katika hilo kusanyiko! Maskini Tanzania!
 
kuiba ilikuwa utoto tu amekua ameacha. tumpe nchi afanye maamuzi ya kukamata mijizi yote kwani anaijua
 
Ni kichaa peke yake atakaeiamini hotuba "dhaifu" ya Lowassa aliowasomea watu pale Arusha!!

Na ni mwendawazimu peke yake atakaesema kwamba Lowassa ni msafi!!

Kwa mtanzania yoyote mwenye akili timamu ataungana nami kwamba, Lowassa hawezi kubadili maisha ya Watz, na kuwatoa kwenye huu mkwamo! Hayo matumaini mapya yanayokuja uzeeni ni ya namna gani?!

Watu wamebaka mpaka katiba ya wananchi, (Chenge), na wakaandika ya kwao binafsi! Leo hii hao hao ndo wanajiandaa kwenda Ikulu! Huu ni upunguan uliopitiliza... Ikulu wanaenda kufanya nini???


Lowasa anawahadaa watu na watu wanahadaika! Hii ni safari ya machungu imeanza rasmi!!! Let's wait and see!
 
Back
Top Bottom