real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,302
Tunakumbuka wakati wa mchakato wa kura za maoni mgombea wa CHADEMA kabla hajahama kutoka CCM alisema kipaumbele chake cha kwanza hadi cha tatu ni elimu, pia alisema alifuatisha kutoka kwa aliyekua waziri wa uingereza kipindi fulani na akaifanikisha sana uingereza. Mimi ninachouliza ni kwamba matatizo ya elimu ni mengi hapa nchini kama vile...
1. Kukosekana kwa madarasa, nyumba za walimu pamoja na miundominu migine
2. Walimu wetu kuwa na uwezo mdogo ukizingatia ni wale watu waliopata madaraja ya chini ndio wanakua walimu
3. Walimu wetu kua na maslahi duni na kusababisha migomo ya mara kwa mara
4. Kukosekana kwa syllabus nzuri inayoendana na hali inavyobadilika kwa sasa
5. Kukosekana kwa maabara za kisasa na wataalamu wazuri katika masomo ya sayansi
6. Wanasayansi wetu hasa wahandisi na wakemia kutokua na masomo ya vitendo ya kutosha ili kutuwezesha kuwa na teknolojia ya kisasa alafu ndio tuwe na viwanda vyetu
7. Ukosefu wa utaalamu kwa wahitimu wetu wa vyuo kutokana na kulipua lipua kwa elimu yetu ya vyuo
8. Mengineyo mengiii...
Sasa huyu mzee wetu sijawahi kumsikia akiainisha matatizo gani yanayoikabili elimu yetu ili tusiendelee na ni jinsi gani atakavyoyatatua badala yake amekua akisisitiza ahadi nyingine za kusaidia machinga, bodaboda, mama ntilie ahadi ambazo haukati mzizi wa tatizo bali ni kupunguza tu majani yake.
Alitakiwa atuambie atafanyaje ili kuzuia vijana wengi kufanya bodaboda ndio kimbilio lao na umachinga kwa kutumia hii elimu
1. Kukosekana kwa madarasa, nyumba za walimu pamoja na miundominu migine
2. Walimu wetu kuwa na uwezo mdogo ukizingatia ni wale watu waliopata madaraja ya chini ndio wanakua walimu
3. Walimu wetu kua na maslahi duni na kusababisha migomo ya mara kwa mara
4. Kukosekana kwa syllabus nzuri inayoendana na hali inavyobadilika kwa sasa
5. Kukosekana kwa maabara za kisasa na wataalamu wazuri katika masomo ya sayansi
6. Wanasayansi wetu hasa wahandisi na wakemia kutokua na masomo ya vitendo ya kutosha ili kutuwezesha kuwa na teknolojia ya kisasa alafu ndio tuwe na viwanda vyetu
7. Ukosefu wa utaalamu kwa wahitimu wetu wa vyuo kutokana na kulipua lipua kwa elimu yetu ya vyuo
8. Mengineyo mengiii...
Sasa huyu mzee wetu sijawahi kumsikia akiainisha matatizo gani yanayoikabili elimu yetu ili tusiendelee na ni jinsi gani atakavyoyatatua badala yake amekua akisisitiza ahadi nyingine za kusaidia machinga, bodaboda, mama ntilie ahadi ambazo haukati mzizi wa tatizo bali ni kupunguza tu majani yake.
Alitakiwa atuambie atafanyaje ili kuzuia vijana wengi kufanya bodaboda ndio kimbilio lao na umachinga kwa kutumia hii elimu