Yofav
JF-Expert Member
- Mar 12, 2021
- 4,309
- 7,857
Ni hivi wewe ni kijana upo kwenye umri wa 20's unaishi Dar wazazi wapo mikoani huko Kila mtu kivyake, Dar una miaka minne na huna mchongo wa maana (Namaanisha unaungaunga sana), Lakini bado una malengo ya kufika mahali fulani kwa mfano: Una mpango wa kumiliki Duka la bidhaa fulani ambazo kwa Sasa upo kama dalali kwenye Duka la watu.
Kama unavyojua maisha ya Dar yalivyo juu 5000 kwa siku Kutoboa kwenye kula tu lazima ujue kujibana haswa(Wanazengo wanajua Ile ya kuunganisha Break fast na Lunch) Yaani hauli kutwa mara tatu ni kutwa mara 2, 2500 mchana, 2500 usiku.
Katika harakati zako kuna Kipindi unabutua hata 30k kwa siku, ila siku nyingine unakosa hata 100 Yaani kiufupi bado sana ili utimize malengo yako maana hapo kati Kuna Kodi ya chumba, Umeme na makorokoro kibao Yani, Then Wazazi wako bado wapo na nguvu tu Mzee anacheza kwenye 40+ na Maza kwenye 30+....
Lakini simu zao nyingi za vizinga na ukisema huna Kila mmoja analalamika kivyake (namaanisha wazazi pia walishaseparate Baba kivyake na mama kivyake) So Kila mmoja akikuomba hela ukakuta huna ukimjibu kuwa huna analalamika au anakubali Ile kishingo upande, Ukicheki Elimu uliyokuwa nayo ni O-level Yaani kiufupi Ukizembea kidogo tu unarudi kimbiji..... Ila wazazi hawalioni Hilo wao wanaamini kwa kuwa upo Dar basi una hela sema unawabania tu.
Mtu Hadi unajishtukia kuwapigia Simu ya kuwajulia Hali wazazi kwa kuwa unajua kinachofuata ni kizinga, Basi siku mkiongea wanalalama mbona huwapigii kuwajulia Hali, Basi kutokana na uzoefu uliokuwa nao na uchovu w aswali Hilo la Kila wakati unaamua kuwachana kuwa huwapigii Simu kwa kuwa unaona aibu wakikuomba hela unawajibu huna Kila siku (Lengo la kuwaambia hivyo likiwa ni kuwataka wabadili fikra zao hizo na kuelewa kuwa ni kweli huna kitu),
Badala washuke ndo Kila mmoja anapanick hivi Yani mzazi anakuwa kama anakuachia laana hivi "Kwahio kumbe hunipigii simu ili nisikuombe hela, Sawa usipige Tena ishi Kama huna wazazi na Wala sitohitaji hela yako" unajaribu kumfafanulia vizuri kwanini umemuambia hivyo anakukatia Simu,
Sasa jamani Wanazengo embu Naombeni Ushauri Kwani wazazi wa kisasa wametuzaa watoto kuja kuwasaidia wao au wao kuwasaidia watoto kutimiza malengo ili kizazi kiendelee kudumu? Ninachojua Mimi ni kwamba mimi ndo ningetakiwa niwadai wao haki ya kutonisomesha au kunihakikishia nakuwa na kazi ya maana, Au ebu ninyi nisaidieni wakuu, Maana wazazi wao ambao ndo mababu zao atleast wamewaachia mashamba na nyumba hata kama ni za msonge.... Ila wazazi wetu Hadi leo asilimia kubwa ndo nyumba za kupanga alafu wanatufanyia hivi watoto wao je, ni Nini matokeo ya yote haya?
Kama unavyojua maisha ya Dar yalivyo juu 5000 kwa siku Kutoboa kwenye kula tu lazima ujue kujibana haswa(Wanazengo wanajua Ile ya kuunganisha Break fast na Lunch) Yaani hauli kutwa mara tatu ni kutwa mara 2, 2500 mchana, 2500 usiku.
Katika harakati zako kuna Kipindi unabutua hata 30k kwa siku, ila siku nyingine unakosa hata 100 Yaani kiufupi bado sana ili utimize malengo yako maana hapo kati Kuna Kodi ya chumba, Umeme na makorokoro kibao Yani, Then Wazazi wako bado wapo na nguvu tu Mzee anacheza kwenye 40+ na Maza kwenye 30+....
Lakini simu zao nyingi za vizinga na ukisema huna Kila mmoja analalamika kivyake (namaanisha wazazi pia walishaseparate Baba kivyake na mama kivyake) So Kila mmoja akikuomba hela ukakuta huna ukimjibu kuwa huna analalamika au anakubali Ile kishingo upande, Ukicheki Elimu uliyokuwa nayo ni O-level Yaani kiufupi Ukizembea kidogo tu unarudi kimbiji..... Ila wazazi hawalioni Hilo wao wanaamini kwa kuwa upo Dar basi una hela sema unawabania tu.
Mtu Hadi unajishtukia kuwapigia Simu ya kuwajulia Hali wazazi kwa kuwa unajua kinachofuata ni kizinga, Basi siku mkiongea wanalalama mbona huwapigii kuwajulia Hali, Basi kutokana na uzoefu uliokuwa nao na uchovu w aswali Hilo la Kila wakati unaamua kuwachana kuwa huwapigii Simu kwa kuwa unaona aibu wakikuomba hela unawajibu huna Kila siku (Lengo la kuwaambia hivyo likiwa ni kuwataka wabadili fikra zao hizo na kuelewa kuwa ni kweli huna kitu),
Badala washuke ndo Kila mmoja anapanick hivi Yani mzazi anakuwa kama anakuachia laana hivi "Kwahio kumbe hunipigii simu ili nisikuombe hela, Sawa usipige Tena ishi Kama huna wazazi na Wala sitohitaji hela yako" unajaribu kumfafanulia vizuri kwanini umemuambia hivyo anakukatia Simu,
Sasa jamani Wanazengo embu Naombeni Ushauri Kwani wazazi wa kisasa wametuzaa watoto kuja kuwasaidia wao au wao kuwasaidia watoto kutimiza malengo ili kizazi kiendelee kudumu? Ninachojua Mimi ni kwamba mimi ndo ningetakiwa niwadai wao haki ya kutonisomesha au kunihakikishia nakuwa na kazi ya maana, Au ebu ninyi nisaidieni wakuu, Maana wazazi wao ambao ndo mababu zao atleast wamewaachia mashamba na nyumba hata kama ni za msonge.... Ila wazazi wetu Hadi leo asilimia kubwa ndo nyumba za kupanga alafu wanatufanyia hivi watoto wao je, ni Nini matokeo ya yote haya?