Dunia sio Salama


Nilisikia kwenye radio jana kwamba miaka ya 70 kuna ndege ndogo ilipotea ikitokea DSM kwenda Zanzibar or vice verse. Mabaki ya ndege hiyo yalipatikana chini ya mlima Kilimanjaro baada ya wiki mbili. Inawezekana wanakoitafuta siko ilikoangukia na rubani mmoja inasadikika alichakachua mawasiliano ya radar.
 
Then heading ya hii habari????

 
Kuna ambao mnakumbuka kimwondo kilichoanguka huko mbeya miaka ya nyuma?
Kwa mfano kimwondo cha jinsi hiyo halafu kiwe kikubwa then kikaigonga ndege na kuizika chini ya bahari ni lini mabaki ya ndege yataonekana?
 

Attachments

  • asteroid-hurtling-towards-earth-640x353.jpg
    20.3 KB · Views: 149
Wakubwa wamepoteza ndege na abiria zaidi ya 200....wengine tukipoteza simu tunaonekana wazeeeembe.
 
Ni kweli hapo nyuma zimewahi kupotea ndege na hazikuonekana kabisa, au zilikuja kuonekana baada ya muda kupita.

lakini hii ndege ya malaysia ukilinganisha na hizo za zamani kuna tofauti kidogo.

1] dunia ya sasa na huko nyuma ni tofauti kwa maana ya maendeleo ya tekinolojia. maarifa ya dunia ya sasa na hapo nyuma ni tofauti,

2] umuhimu uliyopewa hii ndege wa kuitafuta ni mkubwa sana, na habari zimetangazwa karibu ya dunia nzima.

4] eneo wanalotafuta wanakadiria mafuta yaliyokuwa kwenye ndege na muda wa saa 8 ambao ilionekana angani kabla ya kupotea kwenye rada za kijeshi

5] inatafutwa na nchi zaidi ya 25 pamoja na meli, ndege, viona mbali,

kwa hiyo umakini mkubwa unaotumika kuitafuta hii ndege leo ni siku ya 11 na ukiongezea hawa vijana walioingia kwenye hiyo ndege wakitumia pasipoti za wizi , tena wakitokea kwenye taifa ambalo lina mashaka makubwa, na ambalo hapo nyuma lilishakaririwa likisema linataka kuiondoa israel kwenye uso wa dunia, kusema kweli ni lazima mataifa na hata dunia likiwepo taifa letu tuwe macho sana.

kwa sasa hatuwezi kujua hii ndege iko wapi, ni imetekwa? hakuna anayejua, imeanguka baharini hatujui, imepaa imeishia mawinguni hatuelewi. kwa hiyo chochote kinaweza kutokea sehemu yeyote ambayo hatujui. kwa sababu ndege inaruka juu na inaenda kwa kasi kubwa
 
Hii ni kalii kwelii hivi mkuu wa dunia Obama ameliongeleajee hiliii??
 
Waulize wa IRAN wanaitakia nini Ndege ya watu. Hakika Dunia si salama ukiwa unaishi na watu wenye akili za kiirani.
 
hapo umenena .sasa hawa wanaosema dunia si salama wanataka twende wapi.dunia ni dunia tu na ndio ilivyoumbwa ,tatizo likitokea ndio mwanzo wa kugundua teknolojia ya juu zaidi
 

Long ago Marekani waliamua ku-abandon research zao kuhusu UFOs baada ya kuwa wamejiridhisha kuwa UFOs hawapose any threat kwa maisha ya viumbe waliopo duniani. Nadhani kuna haja sasa wa-revisit decision yao kuhusu swala hili. Wasiendelee ku-rule out kuwa siyo threat rather watumie hypothesis ya kuonyesha kuwa hawajui kama UFOs ni threat ama siyo threat na hivyo waingie kazini tena wakishirikiana na mataifa mengine yenye uwezo wa kufanya hivyo. Still, mimi naamini kabisa kuwa bado tuko salama, na tutazidi kuendelea kuwa salama kadri siku zinavyozidi kwenda mbele kwa sababu only the living God rules the world, no more no less, hiyo ndiyo an undeniable fact ya kwanza na ya mwisho hapa duniani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…