DRC: Mtoto wa Tshisekedi ateuliwa kuongoza muungano wa Rassemblement

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,267
000f5e76831cf07413fb3ab8a3020f9a.jpg
Muungano wa Upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo hatimaye umepata kiongozi wake mpya baada ya kifo cha aliyekuwa kiongozi wa Muungano huo, Etienne Tshisekedi wa Mulumba aliyefariki dunia majuma kadhaa yaliyopita jijini Brussels, Ubelgiji

Majukwaa ya vyama 9 vinavyounda muungano wa Rassemblement, wamemchagua Felix Tshisekedi, mtoto wa Etienne Tshisekedi kuwa rais wa Muungano huo na pia kumteua Pierre Lumbi kama rais wa kamati ya mazungumzo

Uteuzi wake umekuja wakati huu bado kukiendelea kushuhudiwa mvutano kuhusu uteuzi wa jina la waziri mkuu wa mpito

Rais wa Muungano huo atakuwa na jukumu la kufuatilia utekelezwaji wa makubaliano ya Desemba 31 mwaka jana, nafasi ambayo alikuwa akishikilia marehemu Tshisekedi kabla ya kufariki dunia

Hata hivyo vyama vitatu vya kwenye muungano huo havikukubaliana na mabadiliko mapya yaliyotangazwa, ambapo wajumbe wake waliamua kutoka kwenye mkutano uliokuwa ukiendelea kupata viongozi

Watu wa juu kutoka kwenye muungano huo wanasema kuwa, mgawanyiko huo ulioshuhudiwa wakati wa mkutano huo, ulitokana na Felix kukosa uzoefu mkubwa kisiasa hali ambayo wanasiasa kadhaa wamehoji utendaji wake.
 
_94921892_c43e1b98-9805-4570-9de0-06eb5f40e5a9.jpg

Muungano mkuu wa upinzani nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo umemteua mwana wa kiume wa aliyekuwa kiongozi wa muungano huo Etienne Tshisekedi, ili kumrithi babake.

Felix Tshisekedi atakuwa rais wa muungano wa vyama tisa vinavyompinga rais Joseph Kabila.

Uteuzi wake ulitangazwa licha ya pingamizi kutoka kwa makundi mawili kwenye muungano huo.

Kiongozi wa muda mrefu wa muungano huo Etienne Tshisekedi, alikuwa ameuongoza kwenye mazungumzo ya mwezi Disemba kuhusu wadhifa wa urais.

_94921893_ebd1e9d9-be03-4b07-830e-3ec2aa0bdeea.jpg

Kwenye makubaliano yaliyoafikiwa, bwana Kabila ataondoka madarakani baada ya uchaguzi ambao utafanyika mwaka huu.

Muhula wake wa pili madarakani ulikamilika rasmi Disemba iliyopita.

Kifo cha bwana Tshisekedi kilizua ghasia za mwezi mmoja kati ya wafuasi wake na vikosi vya usalama mjini Kinshasa, na kusababisha taharuki ndani ya upinzani.

Kwenye makubaliano yaliyoafikiwa, bwana Kabila ataondoka madarakani baada ya uchaguzi ambao utafanyika mwaka huu.

Muhula wake wa pili madarakani ulikamilika rasmi Disemba iliyopita.

Kifo cha bwana Tshisekedi kilizua ghasia za mwezi mmoja kati ya wafuasi wake na vikosi vya usalama mjini Kinshasa, na kusababisha taharuki ndani ya upinzani.

Chanzo: BBC/Swahili
 
Back
Top Bottom