Dr. Slaa hakuna kama wewe

Planner12

Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
76
Reaction score
59
Kwako Dr. Slaa,

Nimekufahamu kwa takribani miaka 6. Ninafahamu baadhi ya tabia zako, unavyovipenda na usivyopenda. Wewe ni mtu mzima sana kwa sasa na kila ufanyacho kinachukuliwa kuwa kimefanywa na mtu mzima mwenye maamuzi na tena maamuzi thabiti. Baadhi ya sifa ulizonazo ni pamoja na


1. KIONGOZI: Wewe ni kiongozi na hakuna anayeweza kubisha hili. Umekuwa kiongozi tangu shule ya msingi, sekondari, vyuo, kanisani na kwenye taasisi za umma. Wakiitwa viongozi ambao ni "Multisectoral" basi wewe umo. Umeweza kuwaunganisha watu wa kada zote. Umeongoza siasa za nchi hii kwenye mfumo wa vyama vingi na umefanya mabadiliko makubwa. Umeweza kukifanya chadema kuitwa kweli chama cha upinzani. Umejenga na kutetea hoja zako bungeni na zilikuwa ni kwa maslahi ya taifa na siyo chama. Dr. Slaa wewe ni kiongozi na utabaki na kuendelea kuheshimiwa sana.'

2. MCHA MUNGU: Dr. hakuna aliye na shaka hata chembe kwamba wewe ni mcha Mungu. Umekulia muda mrefu sana kanisani ukimtumikia Mungu na wanadamu. Unajua nini maana ya UTU na nini maana ya UBINADAMU. Umekuwa ukiwatumikia wananchi wa Tanzania na sio wa chadema. Utakumbukwa kwa hilo na hakuna wa kukuondolea hiyo karama.

3. MSEMA KWELI: Wewe umekuwa msema kweli pale panapohitajika kusema kweli una umesimamia ukweli. Wewe siyo mtu wa kuyumbishwa useme hili wala lile. Ukweli ni ukweli kwako na hauwezi kubadilika ukawa uongo

4. MSIMAMO: Wewe ni mtu mwenye misimamo. Ukisema hapana kwa jambo la hapana basi ndiyo itakavyokuwa na hakuna wa kukubadilisha. msimamo wako ndio uliofanya chadema ikasisima na kufika hapo ilipo sasa.

5. MAAMUZI: Umekuwa ni mtu mwenye maamuzi na kuyasimamia ili kuona mwisho wake. Maamuzi yako huwa unatumia busara kubwa na yanaheshimiwa.

Yako mengi ambayo naweza kuandika kitabu lakini kwa leo naomba niishie hapo niandike lile linipasalo kuandika:


Dr. Slaa kwa sasa nchi imefikia kiwango kikubwa cha demokrasia ambayo inahitaji watu makini, wavumilivu, wenye misimamo, na watakaotetea demokrasia ya kweli. Katika maandiko matakatifu kuna maneno ya kusamehe na kusamehewa. Binadamu kwa hulka yao ni watu wa kukosea, wanaombana msamaha na shughuli zinaendelea. Najua wewe ni Mkristo na unajua nini maana ya kusamehe.

Sasa Dr. Slaa, ninavyokufahamu wewe kubadilisha misimamo yako ni vigumu sana ila kwa hili nitakaloandika hapa tafadhali nisome kwa umakini mkubwa:

Chadema na UKAWA vinapita kwenye wakati mgumu sana kisiasa. Kuna watu ambao jamii imewaamini na kuwapa dhamana na wewe ukiwa mmoja wako. Pamoja na kwamba "inasemekana" mlihitilafiana kwenye baadhi ya mambo, kuna jambo moja kubwa sana umefanya ambalo linadhihirisha sifa za kiongozi aliyekomaa.

Dr. wewe ni MVUMILIVU, MSTAHIMILIVU, MKOMAVU na USIYEKURUPUKA. Ulishawahi kusema wewe siyo mtu wa kukurupuka na kwa kawaida huwa ukiongea unahesabu kila neno litokalo kinywani mwako.

Kwa waraka huu Mhe. Dr Slaa, nakuomba kwa UKOMAVU wa kisiasa ulioonyesha tangu kuanza kwa mchakato wa wagombea wa urais na hasa UKAWA tafadhali sana USITETEREKE na naamini mpaka sasa maneno yako ya kuwa HUKURUPUKI yametimia. Umekuwa kimya bila kusema lolote. Ni vema ukawa kimya hivyo ila nishauri UENDELEE NA SHUGHULI ZA CHAMA. Likishapita hili la uchaguzi basi mtakaa tena kama chama kuangalia mlikojikwaa.

Dr. naweza kuwa naandikia mwenyewe lakini wako wengi wenye mawazo na mwono kama wa kwangu. Dr. ninakujua, ninakufahamu, tunaomba kama utaongea na press hakikisha unatoa neno la kujenga na siyo kubomoa.

Prof. Lipumba amefanya ndivyo sivyo. Siyo kwa wakati huu alitakiwa kufanya alivyofanya. It is costful kwa chama cha CUF na UKAWA. Dr. endelea kumeza hizo shubiri Mungu atakurimu.


Makene hakikisha mzee anapata huu waraka wangu.



Naomba kutoa hoja.
 

Lipumba amefanya sehemu yake. Na sasa ni wakati wa awamu ya watu wengine kuanzia anapoishia. Ukumbuke wanadamu wote hawana permanency. Unajuaje kama hata asingeondoka kihivo angeondoka kivingine nje hata ya utashi wake?

Kikubwa ni kwamba UKaWA siyo mtu, UKAWA siyo kiongozi, UKAWA ni mkusanyiko wa nguvu za nia na mallengo toka watu mbali mbai ambao ni Watanzania wanaochukia uonevu na ubaradhurli wa ccm.

Huu siyo wakati wa kuwalaumu wanaoamua tofauti.

Vitani kuna watu wanaangukiwa na adui mpaka chini.

Vitani kuna majeruhi wanahitaji tiba na hawawezi kwenda front.

Vitani kuna deserters ambao lazima hawaepukiki. Ni wanadamu hawa.

Vitani kuna wapiganaji wasio na nia thabiti ila wanakwenda kwa mob psychology.

Vitani kuna matwaisii ambao mara nyingine huinuka na kuwa imara kuliko hata waliokuwa juu yao.

Yote haya tusije tukajisahau na kuona ni mambo mageni.

Lakini pamoja na yote, TUNASONGA MBELE. KAMANDA MTATIRO AMEKSHAKABA NAFASI. JESHI LINASONGA MBELE. DR. SLAA ANAONGEZA NGUVU NA SOON ATATUJOIN. LAKINI PIA BADO JESHI LETU LINAIMARIKA KWA KUPATA WAPIGANAJI WENGI WALIO TAYARI KUFUATA MPANGO WA VITA AMBAO HATA KAMA VIONGOZI WETU WANAATHIRIKA VITANI, MPANGO HUO UPO IMARA.

TUACHE KUSONONEKA NA KULAUMU YANAYOTOKEA AMBAYO NI YA KAWAIDA SANA VITANI. TUNASONGA MBELE CHINI YA MAKAMANDA WETU WALIOPO NASISI HADI UKOMBOZI UNAPATIKANA.

ALUTA CONTINIUA!!!!!!!!!!!!!!!!, MAPAMBANO YANAENDELEA!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!, USHINDI NI LAZIMA KWA SABABU MUNGU YUKO UPANDE WETU NA ANAZIDI KUTUIMARISHA KATIKA NIA NA MAARIFA!.

MSHINDI NI UKAWA!!!!!!!!!
 
Dr. sasa ndio muda wa kutoa uongozi.....malezeni uchaguzi then mtakutana kama chama kuongea but ikiwa chadema chama ninacho kiamini itashindwa kuongoza watz katika kuondoa ccm hakika heri mfe.Hii ni vita na tumia risasi na makombora...aliye kuwa adui yetu kaja kwetu hivyo tumeana kuwadhohofisha.....tunakutakia heri sana.
 
Dr yuko kwenye wakati mgumu sana
kwanza; anakipenda chama hivyo anaona akijiuzuru anaweza bomoa chama alichotumia nguvu kukijenga

pili ; hapati picha chama kitasimamia misingi ipi baada ya uchaguzi kupita

tatu ; hii kamari iliyochezwa ikitoa matokeo hasi nani atalaumiwa

ili chadema kiweze kusimama kinahitaji ushindi october na si vinginevyo na dr hataki kucheza kamari
 
Slaa kurudi CHADEMA lowasa atimke na mbowe afungwe.
 
Naona wote ni wa dini yetu.

Ritz,hii comment si nzuri,ingekuwa vyema kama unamjua kiongozi ambaye ni wa dini ya pili unamuongezea na hata kama hakumuweka inawezekana amemsahau au hamjui.

Mfano kwa Zanzibar hakutakuja kuwa na kiongozi kama Abeid Aman Karume,piga ua miaka mingi ijaya hakutakuwa kama yeye,nina uhakika na niachosema.
 

kwa vyovyote vile Dr is a mtured person.

i believe that he is just doing some meditations on the new Tanzania.

however, kwa vyoyote vile decision making heavily relies on the rule of give and take...

its just the matter of the post election agenda he had and still having in cdm and ukawa in general..

and these are NEW CONSTITUTIONAL....New Tanzania?...etc.etc.etc....
 
Dr slaa hanunuliki na hawezi kulamba matapishi yake
 

umeinna vizur hii kitu-
 
Yaan karne itawakumbuka hao.wengine wanajiita wana ndoto ila ni njaa tu. Viongo ni hao
 
umeinna vizur hii kitu-

Kigambonian, umepiga kichwa cha nyoka. Salama ya chadema ni kushinda mwezi oktoba. Endapo kitashindwa njia ya nccr au tlp inakikonyeza. Itakuwa vigumu sana watanzania kukiamini kwa sababu kimebomoa misingi iliyosababisha kipendwe achilia mbali nafasi ya slaa ndani ya chama. Baada ya zito, chadema imeweza kivuka dhoruba ya kisiasa lakini kuboma misingi yake na slaa kukaa pembeni havitakiacha salama asilani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…