DR Congo: Muasi Sultan Makenga auawa

Alice Gisa

Senior Member
Joined
Sep 6, 2014
Posts
172
Reaction score
417
Kumekuwa na uvumi wa muda mrefu kuwa Bri Gen Sultan Makenga kauawa vitani huko DRC.

Hatimaye Leo zimevujishwa picha za maiti ya Makenga kwenye mitandao ya kijamii.

Itoshe nisema hili ni pigo kubwa sana kwa M23 na kwa Rais Kagame bila kumsahau Lut Gen Kabarebe wa Rwanda.

Brig Gen Sultan Emmanuel Makenga. Ni mtutsi mzaliwa na DRC Jimbo la Kivu ya Kusini. Mji mdogo wa Minembwe.

Makenga ndiye punda wa M23 na CND enzi za Gen Kunda. Punda kwa maana ndiye aliyefanya kazi ngumu zote za uundaji wa CND baadae M23.

Ijapokua ni Mtutsi, Makenga hakupendwa na Kagame. Mtu pekee alikuwa akimpenda Makenga jikoni Rwanda ni Gen James Kabarebe. Na sababu ikiwa Makenga alikuwa msaada mkubwa kwa Kabarebe alipokuwa akiongoza ile Operation Kitona wakati wa vita ya pili Kongo.

Hili ni anguko kubwa sana kwani kwenye makamanda wa M23 ni Makenga ndiye alikuwa na ujuzi mkubwa wa kutumia topography ya Kivu kumanuva vita.

Labda nidokeze 2012 walipokosana Makenga na Bosco Ntaganda ilimchukua siku mbili tu kumuweka kati bw Ntaganda na Ntaganda akakimbilia ubalozi wa US huko Kigali


 
Siyo mara ya kwanza kuzushiwa.
 
Amepata alichokuwa anakitafuta huyu fala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…