Down Memory Lane, Yaliyomkuta Uncle Wangu Nchi Hii

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Uncle wangu aliyekuwa Afisa Mwandamizi EAC walimtengenezea cheti feki cha kifo na wakakomba mafao yake na pensheni zote 100%.

Siku alipozuka kuzichukuwa mwaka 2012 baada ya Mahakama ya Tanzania kuamuru walipwe, wale staffs wa huduma kwa mteja baada ya kuangalia kwenye mfumo wa tarakilishi (computer) wakapiga ukunga/yowe/nduru kuwaita staffs wenzao eti wamezukiwa na mzimu.

Walipofika staffs hao na kuuliza mzimu upi, wakamwonyesha huyo hapo (yaani uncle wangu).

Uncle alipouliza ni kwa vipi wamnyanyapae kiwango hicho kwa kumuita mzimu wakati amekuja kudai haki zake?

Wakasema mfumo unaonyesha wewe ni marehemu tangu mwaka 1985 na kivuli cha cheti cha kifo hiki hapa kwenye tarakilishi na mafao uliishachukuwa ushahidi huu hapa na mwenzi wako alichukuwa nusu pensheni hadi 1986.

Wale staffs walioitwa kushuhudia mzimu wakayeyuka, uncle puuuuu.... chini, pepewa pepewa pale na walinzi, fahamu ziliporudi akaacha laana ya karne (kama serikali inalaanika sijui!?) na kuondoka hapo Hazina Makao Makuu hadi leo yuko hai Kijijini kama EL kule Peninsular; na akasusa kabisa kurudi Hazina.

Aina hii ya watumishi ndiyo wamejaa serikalini na ndiyo watafanya models kama za akina Makonda zisiishe nchi hii, zitakuja na kutoweka na kurudi tena na kutoweka tena na kurudi...

Yaliyopita si ndwele...
 
3048962_IMG_20211217_181857.jpg
 
Ila ningekuwa ni mimi ningehakikisha waliohusika wote wanakuwa accountable to what they did. Yaani miaka yote hiyo iwe nimewafanyia kazi wao maarabuku😭

Ila Nina swali uncle wako alikuwa wapi muda wote huo? How did this happen kuwa hajastaafu kazi akaacha kwenda na ikaaminika amekufa?
 
Dogo jikite kwenye mada iliyopi mezani.

Haya mambo siyo ya mzaha. Kuna watu wana roho mbaya sana. Yani kuna watu wana ishi kabisa kwa kupigia mahesabu na bajet hela na mali za wengine jasho la utumishi.

Bora tukomae huku huku ulaya kwenye haki ambapo hata ukibaguliwa kwa rangi unalipwa kulingana na kipato aliyekubagua iwe kazini nyumbani hata mtaani.
 
Dogo jikite kwenye mada iliyopi mezani.

Haya mambo siyo ya mzaha. Kuna watu wana roho mbaya sana. Yani kuna watu wana ishi kabisa kwa kupigia mahesabu na bajet hela na mali za wengine jasho la utumishi.

Bora tukomae huku huku ulaya kwenye haki ambapo hata ukibaguliwa kwa rangi unalipwa kulingana na kipato aliyekubagua iwe kazini nyumbani hata mtaani.
We mbusi kila siku nakuambia nipe mchongo huko yurop unajichekesha tu kifara.
 
Ila ningekuwa ni mimi ningehakikisha waliohusika wote wanakuwa accountable to what they did. Yaani miaka yote hiyo iwe nimewafanyia kazi wao maarabuku

Ila Nina swali uncle wako alikuwa wapi muda wote huo? How did this happen kuwa hajastaafu kazi akaacha kwenda na ikaaminika amekufa?
EAC ya 1977 ilisambaratika na Kenya na Uganda wakalipwa, Tz haikulipa, ela za kuwalipa zilizotolewa na Wascandinavia Mwl alizihawilisha (reallocate) kwenda kuanzisha TIB ambayo nayo ililiwa na mchwa.

Baada ya hapo 1977 kesi ilifunguliwa lakini serikali kibabe ikafanya case parking (ikapaki kesi) isiendelee kwa ahadi kwamba wanatafutiwa fungu walipwe.

Mwl akaondoka hakuwakipa, Ruksa akaondoka hakuwalipa, Big Ben akawatandika na FFU, Msoga akaruhusu kesi ianze upya, wakafika sehemu wanalala pale TRC Stesheni.

Wazee wakafika hatua wanafunga barabara wakiwa uchi wa mnyama siku kesi inatajwa/inasikilizwa. Walishinda lakini bado hawakulipwa.

Jembe akalipa kidogo baadaye akasema ana ela za miradi ya kimkakati tu hana ela za madeni ya wastaafu wa EAC.
 
Back
Top Bottom